Thursday, October 23, 2014

KUBALI USIKUBALI, MWANA YA ALIKIBA NI DONGO KWA DIAMOND, USHAHIDI HUU HAPA

HUU HAPA UTHIBITISHO.
Mali ni nyingi nyumbani, kipi kimekukimbiza,
Hapa Alikiba, anamwambia Diamond, nyumbani ( SHAROBARO RECORDS) kuna kila kitu, beats kali, management nzuri and all that, kitu gani kilimkimbiza SHAROBARO RECORDS?

Ona babio mamio wote wanakulilia,
HAPA ALIKIBA ANAMAANISHA, SHAROBARO RECORDS, WAKIONGOZWA NA BOB JUNIOR, WOTE WANAMLALAMIKIA DIAMOND KWA KITENDO CHAKE CHA KUKIMBIA KUFANYA KAZI SHAROBARO. (BOB JUNIOR ALIPIGA KELELE SANA DIAMOND ALIPOKIMBIA SHAROBARO RECORDS )

Mtoto pekee ako nyumbani, kipi kimekukimbiza,
HAPA ALIKIBA ANASEMA, DIAMOND ALIKUWA NDO ARTIST PEKEE MKALI ALIYEKUWA CHINI YA SHAROBARO RECORDS. HAKUKUWA NA UPINZANI WOWOTE NDANI YA SHAROBARO, KITU GANI KILIMFANYA AONDOKE ?

Ona babio mamio wote wanakulilia

Ndani ya Dar es salame ulikuja bure
HAPA ALIKIBA ANAMKUMBUSHA DIAMOND, KUWA SIKU ALIPOKWENDA SHAROBARO RECORDS KWA MARA YA KWANZA, HAKUWA NA HATA SENTI TANO NA ALIREKODIWA WIMBO WAKE BURE KABISA.NENO DAR ES SALAME, LIMETUMIKA KUMAANISHA SHAROBARO RECORDS AU MUSIC INDUSTRY.
(KAMA ULIKUKUWA HUJUI, ALIKIBA NI MMOJA KATI YA WANAHISA WA SHAROBARO RECORDS, NA NDIO ALITOA IDHINI KWA BOB JUNIOR, AREKODI BURE WIMBO WA DIAMOND. ILIKUWA HIVI DIAMOND ALIENDA KWA BOB JUNIOR NA KUMWAMBIA ANA WIMBO WAKE ANAOMBA UREKODIWE LAKINI HANA UWEZO WA KIFEDHA, BOB JUNIOR AKAOMBA KUMSIKILIZA, ALIPOMSIKILIZA AKAGUNDUA KIPAJI CHA DOGO, BUT HAKUWA NA MAMLAKA YA KUREKODI WIMBO HUO BURE BILA IDHINI YA BOSS, ALIKIBA, SO IKABIDI AENDE KWANZA KUOMBA IDHINI KWA ALIKIBA, ALIKIBA AKAMWAMBIA BOB JUNIOR KAMA DOGO ANAJUA KUIMBA VIZURI, MREKODIE TU, HAKUNA SHIDA. ALIKIBA ALIYASEMA HAYA AKIWA ANAYAFANYA MAHOJIANO KWENYE KIPINDI CHA MKASI HIVI KARIBUNI.

Tena kimwana, kimwana hujui kuchuna
WAKATI DIAMOND, ANAENDA KUOMBA KUREKODI KWA BOB JUNIOR, ALIKUWA TAYARI KUFANYA SHOW ZAKE HATA BURE ILIMRADI TU AWEZE KUJITANGAZA..DIAMOND ALIWAHI KUMUOMBA ALIKIBA, APANDE NAYE KWENYE SHOW YA ALIKIBA, BILA MALIPO YOYOTE ILI WATU WAMUONE AKIWA NA ALI KIBA. SO ALIKIBA AMETUMIA NENO “KIMWANA ASIYE JUA KUCHUNA” AKIMAANISHA ‘MSANII UNDERGROUND ALIYE TAYARI KUIMBA HATA BILA MALIPO.

Na zile lawama za wale walokuzoeza,
HAPA ALIKIBA ANAZUNGUMZIA LAWAMA ZA MADEMU WANAO TOSWA NA DIAMOND

Ulikuja jana na leo tofauti sana.
HAPA ALIKIBA ANAZUNGUMZIA NAMNA AMBAVYO DIAMOND AMEBADILIKA KITABIA BAADA YA KUPATA MAFANIKIO KIMUZIKI.

. Tena bora Yule wa jana, wa leo tofauti sana,
HAPA ALIKIBA ANAWAZUNGUMZIA WEMA SEPETU NA PENNY, ANASEMA BORA HATA PENNY KULIKO WEMA AMBAYE NDIO YUPO NA DIAMOND KWA SASA

Dakika mbili mbele nyuma, kichwa kinauma
HAPA ALIKIBA ANAZUNGUMZIA TABIA TABIA ZA WEMA SEPETU. MKOROFI(DAKIKA MBILI MBELE NYUMA), NA MWINGI WA HABARI, AMA PASUA KICHWA ( KICHWA KINAUMA) AMA KICHECHE.

Tena bora Yule wa jana, wa jana leo wa jana,
HAPA ALIKIBA ANASISITIZA ANACHO KIMAANISHA, KWAMBA ANAMZUNGUMZIA WEMA, ” tena bora yule wa jana, wa jana leo wa jana ” YANI YULE AMBAYE UPO NAE LEO, NA AMBAYE ULIWAHI KUWA NAE ZAMANI. NI WA JANA, UPO NAE LEO, LAKINI ULIWAHI KUWA NAYE JANA. HUYO NI WEMA SEPETU, ALIWAHI KUWA NA DIAMOND, WAKAACHANA, WAMERUDIANA TENA. ( ‘WAJANA LEO WA JANA = WEMA SEPETU )

Dakika mbili mbele nyuma, kichwa kinauma
HAPA ALIKIBA ANAKUTOLEA UFAFANUZI ZAIDI KWAMBA, HUYU ” WA JANA LEO WA JANA” SI MWINGINE ILA NI WEMA SEPETU. ANAFANYA HIVYO KWA KUELEZEA TABIA YA WEMA SEPETU AMBAZO NI “UKOROFI” (DAKIKA MBILI MBELE NYUMA ), NA UKICHECHE A.K.A PASUA KICHWA (KICHWA KINAUMA)..KAMA UMESAHAU WEMA SEPETU ALIWAHI KUMTUKANA BOB JUNIOR MATUSI YA NGUONI, KESI IKAENDA MAHAKAMANI..UNAKUMBUKA HIYO?

Oyayee , mbona unawatesa sana,
HAPA ALIKIBA ANAMWAMBIA DIAMOND MBONA UNAWATESA SANA HAO WASICHANA UNAO WABADILISHA BADILISHA ?

Omamee, omame oya mame, omame oya mamee .

.. Mbona unajitesa sana

HAPA ALIKIBA ANAMWAMBIA DIAMOND “WHAT GOES AROUND COMES AROUND”. ANAVYO WATESA HAO WSICHANA, NI SAWA NA KUJITESA MWENYEWE TU. UKICHECHE WA DIAMOND UNAMTESA KIASI CHA KUMFANYA ASHINDWE KUJUA AMPENDE NANI KATIKA MAISHA YAKE, KWA SABABU WANAWAKE KARIBU WOTE ANAO TOKA WANAKUWA NA KASORO ZISIZO VUMILIKA.

Omamee, oya mame, omame oya mamee
Ukaanza kulewa, madawa kuvuta kwa sana.

HAPA ALIKIBA ANATHIBITISHA NAMNA AMBAVYO HALI YA KUWATESA WANAWAKE INAMRUDIA DIAMOND MWENYEWE. BAADA YA KUUMIZWA NA MWANAMKE/WANAWAKE, DIAMOND AKAONA HAKUNA NJIA NYINGINE YA KUPAMBANA NA MAUMIVU YA KUUMIZWA NA MWANAMKE, ZAIDI YA KULEWA. DIAMOND ALITOA WIMBO, ” NATAKA KULEWA” AMBAO ULIKUWA BASED ON TRUE STORY.

Ndani ya Dar Es salaam, mambo matamu hayakukwisha hamu

HAPA ALIKIBA ANAELEZEA NAMNA AMBAVYO DIAMOND HAJAISHIWA NA HAMU YA KUTEMBEA NA WANAWAKE AMBAO ANAWAPATA BAADA YA YEYE KUWA MAARUFU KUPITIA MUZIKI.

We bado mtoto wa mama hujayajua mengi

HAPA ALIKIBA ANAUA NDEGE WAWILI KWA JIWE MOJA., KWANZA ANATOA UFAFANUZI WA MTU ANAYE MZUNGUMZIA. ALIKIBA ANATAKA UJUE KUWA ANAMZUNGUMZIA DIAMOND NA SIO MTU MWINGINE YOYOTE YULE, SO ANAELEZEA JAMBO LINALO ASHIRIA MTU ANAYE MZUNGUMZIA HAPA ” we bado mtoto wa mama “ DIAMOND NI MTOTO WA MAMA, YUPO KARIBU ZAIDI NA MAMA YAKE NA HANA MAWASILIANO MAZURI NA BABA YAKE. ( UKISIKILIZA VIBAYA HAPO UNAWEZA KUDHANI ALIKIBA ANA MAANISHA “MTOTO KWA MAMA”, BUT KIUKWELI ANAMAANISHA “MTOTO WA MAMA” )
NA ANAPOSEMA HUJAYAJUA MENGI, ANAELEZEA MTAZAMO WAKE KUHUSU UPEO WA DIAMOND, KUHUSU MAISHA YA MWANADAMU. ALIKIBA ANA AMINI KUWA DIAMOND BADO HAJAJUA MENGI KUHUSU MAISHA, NDIO MAANA ALIWADHARAU SHAROBARO RECORDS WALIO MTOA PAMOJA NA BABA YAKE MZAZI.

.. Mwenda tezi na omo marejeo ngamani
HAPA ALIKIBA ANAMKUBUSHA DIAMOND ASISAHAU ALIPOTOKA.

Amesema sana mama, dunia tambala bovu

Kuna asali na shubiri ujana giza na nuru

HAPA ALIKIBA ANAMSHAURI DIAMOND, ASICHEZE NA UJANA WAKE NA AKUMBUKE KUWA KUNA WAKATI WA KILA JAMBO, LEO YUPO JUU KIMUZIKI NA KIMAISHA LAKINI KESHO ATAKUWA CHINI. SO AKUMBUKE ALIPOTOKA, ASIJISAHAU.

We mwana wewe mwana, mbona jeuri sana

HAPA ALIKIBA ANA ELEZEA NAMNA AMBAVYO DIAMOND AMEKUWA JEURI BAADA YA KUPATA MAFANIKIO YA KIFEDHA NA KIMUZIKI.

Ulichokifata hukupata , umekosa ulivyo achaa

Kwa baba yako mwana, na mama yako mwana

Kwa vicheche ulivyo vitaka , ni vingi ulivyo achaa,

HAPA ALIKIBA ANAMWAMBIA DIAMOND ” UMEKIMBIA SHAROBARO RECORDS NA KWENDA KWINGINEKO ILI UPATE UPATE MAFANIKIO ZAIDI YA KIMUZIKI NA HATIMAYE UPATE FURSA YA KUN’GOA MADEMU, LAKINI UMEISHIA KUPATA VICHECHE TU KAMA AKINA WEMA SEPETU NA JOKATE. WAKATI VICHECHE KAMA HAO ULIKUWA NA NAFASI YA KUWAPATA HATA KAMA UNGEBAKI SHAROBARO RECORDS. MATOKEO YAKE SASA, WALE MADEMU AMBAO ULIKUWA UNAWATAKA WAKATI UPO SHAROBARO RECORDS ( AMBAO WALIKUWA NA AFFILIATION NA SHAROBARO RECORDS) UMEWAKOSA NA MADEMU AMBAO ULITARAJIA UNGEWAPATA UKIWA NJE YA SHAROBARO RECORDS HUJAWEZA KUWAPATA.

Oyayee, mbona unajitesa sana

Mbona unawatesa sana

( IMESHAELEZEWA JUU )

UNALETA LAWAMA, UNALETA LAWAMA X 2
Uchungu wa mwana aujuaye mzazi.
Uchungu wa mwana aujuaye mzazi, siku zote leilee
Analiaa oooh oooh oooh oooh
Kutwa nzima analalamika
Obaba baba na mama yako yako, oooh mwana rudi eeeh
Watafurahi wakikuona umerejea salama.

HAPA ALIKIBA AMEFANYA KAMA KUPOTEZA MABOYA VILE ILI ASIONEKANE KAMA ANAMPIGA MADONGO DIAMOND MOJA KWA MOJA.

SOURCE :LIKUD / JAMII FORUM

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BOFYA HAPA ILI HUPATE HABARI KIRAHISI PUNDE ZITUFIKIAPO 

KWELI NIMEAMINI HUYU MISS TANZANIA SIO HALALI.. NI MWONGO WA KUFA MTU...TAZAMA VIDEO ALIVYODANGANYA NA KUBWABWAJA MBELE YA WAANDISHI WA HABARI

Kwa sasa tuna miss Tanzania mpya aitwaye Sitti Mtemvu ambaye kwa maelezo yake anasema ana miaka 23 huku ushahidi mwingine ukionyesha kua ana zaidi ya miaka 23. Baada ya kuchaguliwa tu watu wengi walianza kulalamika kua Sitti alipewa ushindi huo kwa kupendelewa jambo ambalo hata mimi naona ni la kweli. Jana mwandaaji wa mashindano hayo Lundenga aliitsha mkutano na waandishi wa habari na kutoa ufafanuzi ya kua mshindi huyo hana miaka 18 kama watu wanavyosema na kuweka vithibitisho ya kua Sitti ana miaka 23 kama cheti chake kinavyosema. Uongo ambao nauona hapa tumedanganywa ni kuhusu hicho cheti ambacho mimi nakiona ni feki ni kua kilitengenezwa mda mfupi kabla ya kuanza mashindano huku cheti cha kwanza ambacho ndicho kilichotumika kutengeneza hadi Passport yake inayoonyesha kua kazaliwa mwaka 1989 kikiwa kimepotea. Na alipoulizwa kilivyopotea ulienda kutoa taarifa kituo gani cha polisi aligoma kutaja. Kwa nini agome na wakati ilikua rahisi tu kutaja jina la kituo cha polisi kama kweli alienda kutoa taarifa?? ni maswali mengi aliulizwa lakini akagoma hii ni dalili kua miss Tanzania wetu ni magumashi matupu. Haiwezekani mtu tunayemwamini akaiwakilishe Tanzania katika mashindano ya dunia ashindwe kujibu maswali muhimu kabisa kuhusu umri wake. Hii ni aibu kubwa kwa Lundenga na nahisi atakua amejifunza kitu na hatarudia kupitisha mamiss kimagumashi hivi, na naamini hata yeye roho inamuuma kwa alichokifanya. Unaweza tazama video ya mahojiano hayo hapa chini :

SHINJI KAGAWA ALIYEONEKANA'WA KAZI GANI' MAN UNITED AENDELEA KUNG'ARA NA UZI WA NJANO AKIINGOZA DORTMUND KUUA 4-0 ULAYA

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Shinji Kagawa (kulia) akigombea mpira na mchezaji wa Galatasaray, Felipe Melo katika mchezo wa Kundi D Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu nchini Uturuki. Borussia Dortmund imeshinda 4-0, mabao ya Aubameyang dakika ya sita na 18, Reus dakika ya 41 na Ramos dakika ya 83.

LIGI YA MABIGWA: ANGALIA LIVERPOOL ILIVOFANYWA KITU MBAYA NA REALMADRID KATIKA UWANJA WA NYUMBANI

Mambo yameendelea kuwa magumu baada ya Liverpool kuchapwa nyumbani kwa mabao 3-0 katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Real Madrid ndiyo walioingusha Liverpool ikiwa nyumbani na Cristiano Ronaldo akapiga bao la kwanza kabla Mfaransa, Karim Benzema kutupia mbili. Juhudi za Liverpool kutaka kusawazisha katika kipindi cha pili hazikuzaa matunda. Mshambuliaji wa Liverpool, Mario Balotelli alionekana kufanya juhudi, lakini hakufurukuta.

LIGI YA MABIGWA ULAYA: MATOKEO YA MECHI KATI YA ANDERLTECH YA UBELGIJI vs ARSENAL HAYA HAPA

Arsenal imejitutumua na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 ikiwa ugenini katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Arsenal imeichapa Anderletch ya Ubelgiji katika mechi hiyo iliyoonekana itaisha kwa wenyeji kushinda lakini Arsenal ikafunga mabao mawili katika dakika mbili. Keran Gibbs alifunga bao la kusawazisha katika dakika ya 89, kabla ya Lukas Podolski kufunga la pili katika dakika ya 90.

Wednesday, October 22, 2014

SIMBA SC YAINGIA KATIKA WAKATI MWINGINE MGUMU ZAIDI LIGI KUU

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM BAADA ya mechi nne mfululizo za nyumbani katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba SC itacheza mechi yake ya kwanza ugenini mwishoni mwa wiki. Simba SC itacheza na Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi, Ikitoka kutoa sare nne katika mechi zote za mwanzo, 2-2 na Coastal Union, 1-1 na Polisi Moro, 1-1 na Stand Unted na 0-0 na Yanga SC. Katika Ligi yetu, nyumbani ni sehemu nzuri ya kuvuna pointi kuliko ugenini, hususan timu za Dar es Salaam zinaposafiri mikoani na kwenda kukutana na viwanja vyenye hali isiyo nzuri sana katika eneo la kuchezea. Sasa Simba SC ndiyo wanaingia katika wakati huo, kwani baada ya mechi na Prisons Jumamosi, wiki inayofuata watakuwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro kumenyana na Mtibwa Sugar Novemba 1, kabla ya kurejea tena Dar es Salaam kucheza na Ruvu Shooting Novemba 9. Huo utakuwa mchezo wa mwisho kabla ya mapumziko marefu ya karibu mwezi mzima kupisha Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge na michuano ya vijana ya Kombe la Uhai, inayohusisha klabu za Ligi Kuu hadi Desemba 26 ligi hiyo itakaporejea tena. Simba SC haijashinda mechi kati ya nne ilizocheza nyumbani na katika mechi zake tatu zijazo, mbili itacheza ugenini tena dhidi ya timu ambazo zinapokuwa nyumbani kwao, hushinda mara nyingi. Tayari kuna shinikizo la mashabiki kutaka timu ishinde baada ya sare hizo nne za nyumbani- na bahati mbaya Simba SC inakwenda kwenye mchezo mgumu zaidi. Kipa Ivo Mapunda bado hajapona na anahitaji wiki mbili zaidi kabla ya kuanza mazoezi taratibu, Hussein Sharrif ‘Casillas’ naye si wa kumtarajia mwaka huu kucheza- maana yake klabu itacheza mechi hizo ikiwa na kipa mmoja tu, Peter Manyika. Huyo ni wa kumuombea naye asiumie na wala asipate adhabu ya kumzuia kucheza- wakati huo huo wachezaji wengine majeruhi akina Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Miraj Adam, Nassor Masoud ‘Chollo’, Paul Kiongera, Jonas Mkude na Amisi Tambwe mustakabali wao bado haueleweki. Wazi mashabiki wa Simba SC wanatakiwa kushikamana sana na timu yao kwa wakati huu mgumu, wakijua hali halisi kwamba wapo katika kipindi kigumu cha mpito.
Wachezaji wa Simba SC watakuwa na mechi mfululizo za ugenini kuanzia wikiendi hii

PICHA KUTOKA KWENYE MSIBA WA MSANII YP

Aliyekuwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, YP ambaye amefariki usiku wa jana katika hospitali ya Temeke wakati alipokuwa akitibiwa maradhi ya kifua kikuu (TB) anatarajiwa kuzikwa siku ya kesho katika makaburi ya Chang’ombe jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu, YP ambaye jina lake halisi ni Yessaya Ambilikile ameugua kwa kipindi cha takribani miezi 2 kabla ya kufikwa na umauti hapo jana.

 BOFYA HAPA KUTAZAMA PICHA 

LIGI YA MABIGWA: MATOKEO YA BARCELONA vs AJAX HAYA HAPA

BARCELONA imeshinda mabao 3-1 dhidi ya Ajax katika mchezo wa Kundi F Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu wa Camp Nou. Neymar alianza kuifungia Barcelona dakika ya nane kabla ya Lionel Messi kufunga la pili dakika ya 24, Muargentina huyo akitimiza jumla ya mabao 69 aliyofunga katika Ligi ya Mabingwa Ulaya. Messi alifunga bao lingine ambalo lilikataliwa na refa kwa kuwa aliotea dakika ya tatu ya kipindi cha pili, lakini Sandro Ramirez aliyetokea benchi akaifungia Barca bao la tatu dakika za majeruhi. Bao pekee la Ajax lilifungwa na Anwar El Ghazi aliyetokea benchi pia. Neymar na Messi wote walipumzishwa kabla ya dakika ya 66 kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi wa El Clasico dhidi ya Real Madrid. Mchezo mwingine wa kundi hilo, PSG imeifunga 1-0 APOEL Nicosia, wakati Kundi H, Shakhtar Donetsk imeichapa 7-0 BATE Borisov na FC Porto imeilaza 2-1 Athletic Bilbao.

HIVI NDO JINSI BAYERN MUNICH ILIVOIPIGA KIPIGO CHA MBWA MWIZI AS ROMA UWANJA WA OLIMPICO MJINI ROME

Home » Unlabelled » BAYERN MUNICH YAITANDIKA ROMA 7-1 NYUMBANI KWAKE BAYERN Munich imeifumua AS Roma mabao 7-1 katika mchezo wa Kundi E Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Olimpico mjini Rome, Italia. Thomas Muller aliifungia timu ya Pep Guardiola bao la kwanza dakika ya tisa, kabla ya Mario Gotze kufunga la pili dakika ya 23 na Robert Lewandowski kufunga la tatu baadaye kidogo. Arjen Robben akafunga la nne akimtungua kipa Morgan De Sanctis kabla ya Thomas Muller kufunga la tano kwa mkwaju wa penalti na Franck Ribery na Xherdan Shaqiri waliotokea benchi wakafunga bao la sita na la saba. Bao la kufutia machozi la Roma lilifungwa na Gervinho dakika ya 66. Mchezo mwingine wa kundi hilo, Manchester City ilitoa sare ya 2-2 ugenini dhidi ya CSKA Moscow.

DROGBA 'ACHEKA NA NYAVU' CHELSEA IKIUA 6-0 LIGI YA MABINGWA

CHELSEA imefanya kile kinachoitwa ‘mauaji’ baada ya kuifumua Maribor mabao 6-0 katika mchezo wa Kundi G Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Stamford Bridge, London. Loic Remy aliifungia bao la kwanza timu ya Jose Moutinho dakika ya 13 kabla ya kuumia na kumpisha mkongwe Didier Drogba aliyekwenda kufunga bao la pili kwa penalti dakika ya 23. John Terry akafunga bao la tatu kwa shuti la mbali dakika ya 30 kabla ya krosi ya Eden Hazard kutumbukizwa nyavuni na beki wa Maribor Mitja Viler katika harakati za kuokoa. Maribor ilipoteza nafasi ya kupata bao la kufutia machozi, baada ya mkwaju wa penalti wa Agim Ibraimi kugonga mwamba na Hazard akafunga bao la tano kwa penalti na la sita dakika ya 90. Katika mchezo mwingine wa Kundi G, Schalke O4 imeifunga 4-3 na Sporting.

SASA ALEX FERGUSON AHAMUA KUPASUA JIBU KUHUSU DAVID MOYES

KOCHA mstaafu, Sir Alex Ferguson amesema hakuwa na cha kufanya juu ya taratibu zilizotumika kumfukuza David Moyes katika klabu ya Manchester United Aprili mwaka huu na kwamba alichanganyikiwa baada ya kugundua hilo. Ferguson alimchagua Moyes kuwa mrithi wake Old Trafford mwaka uliopita baada ya kustaafu na katika kitabu chake cha sasa ameandika kwamba alikuwa kizani dhidi ya uamuzi uliochukuliwa kumfukuza Mscotland mwenzake huyo. "Nilikuwa Aberdeen wakati hilo linatokea", amekumbushia. "Jumatatu, nilikuwa nasafiri kurudi Manchester na aliyekaa pembeni yangu alikuwa ni kijana ambaye anasoma gazeti lenye habari: "David Moyes kufukuzwa".' Sir Alex Ferguson (kushoto) alikabidhi mikoba yake Manchester United kwa David Moyes (kulia) Moyes alifukuzwa baada ya kipigo cha 2-0 kutoka kwa Everton Aprili mwaka huu, akiwa ameshinda asilimia 50 tu ya mechi zake Ferguson akasema alichganyikiwa katika ndege akiwa anarejea Manchester na hakuwa na uhakika ajibu vipi meseji aliyotumiwa na Moyes. "Sikuwa na hakika mini kilitokea kwa wakati huo haswa," ameandika akizungumzia meseji hiyo. Ferguson ameasema: "Nikazungumza na (Mtendaji Mkuu) Ed Woodward niliporejea na akasema uamuzi wa mwisho wa waliochukua.' Kwa Moyes, Ferguson pia amesema kwamba kocha huyo wa zamani wa Everton ana safari ndefu akiendelea kusaka kazi mpya. "Katika rekodi yake itaonyesha kwamba aliteuliwa kuwa kocha wa Manchester United, kitu ambacho ni nadra,". Moyes alimaliza katika nafasi ya saba akiwa Manchester United msimu uliopita, na wakati Mscotland huyo anaondoka United aliacha rekodi mbaya zaidi ya mechi za nyumbani tangu mwaka 1978 na pointi chache zaidi katika historia ya Ligi Kuu ya England. Bado alikuwa ana asilimia nzuri ya ushindi zaidi ya Sir Matt Busby, lakini alipoteza mechi 11 kama kocha wa United, akiruhusu mabao 40 katika mechi 34, kabla ya kufukuzwa siku mbili baada ya kipigo cha 2-0 kutoka kwa Everton, Aprili 22, mwaka huu katika Ligi Kuu. Ryan Giggs alikaimu nafasi yake kumalizia msimu kabla ya Mholanzi, Louis Van Gaal kuajiriwa msimu huu. Hata hivyo, bado United haijawa na mwenendo mzuri chini ya kocha mpya, licha ya kumwaha fedha nyingi kusajili nyota kadhaa.

Tuesday, October 21, 2014

MSIBA MWINGINE TENA....! BAADA YA KUONDOKEWA NA YP HUYU NI MSANII MWINGINE ALIYEFARIKI SIKU YA LEO

Ni masaa machache tu yamepita tangu muziki wa kizazi kipya Tanzania, Bongo Fleva kumpoteza aliyekuwa staa wa muziki huo kutoka kundi la TMK Wanaume Family, aliyekuwa akifahamika kwa jina la YP, taarifa nyingine ya simanzi inahusu msiba wa aliyekuwa muigizaji wa Bongo Muvi. Katika ukurasa wake wa instagram, muigizaji na mchekeshaji maarufu anayefahamika kwa jina la Kitale ama Mkude Simba (@mkudesimbaoriginal), amepost picha ya muigizaji aliyefariki masaa machache yaliyopita pia. Shery Mwana Kwa mujibu wa Kitale, muigizaji huyo ambaye jina lake halisi ni , aliwahi kushiriki na Kitale katika movie mbali mbali ikiwemo Kipotabo na Nyumba Nne.

ANGEL DIMARIA AZUA HOFU KUBWA MANCHESTER UNITED

WINGA Angel di Maria alionekana hayuko vizuri akiwa ameketi kwenye benchi la Manchester United usiku wa jana, huku amekandamizia barafu katika nyonga yake kwenye mchezo huo ulioisha kwa sare ya 2-2 na West Bromwich Albion. Muargentina huyo, aliyesajiliwa kwa dau la rekodi United, alikuwa kivutio Uwanja wa The Hawthorns, lakini kulikuwa kuna wasiwasi juu ya kiungo huyo baada ya kutolewa dakika ya 76. Di Maria amekuwa katika kiwango babu kubwa tangu asajiliwe kwa Pauni Milioni 60 kutoka Real Madrid msimu huu na ameendeleza mwanzo wake mzuri usiku wa jana. Alimsetia Marouane Fellaini kufunga bao la kusawazisha kipindi cha pili, kabla ya kumpisha Ashley Young. Amecheza mechi tano hadi sasa Manchester United na amefunga mabao matatu na kusaidia manne.
Di Maria (aliyekaa chini kulia) akiwa amekandamizia barafu kwenye nyonga yake huku Chris Smalling, Ander Herrera na Ryan Giggs wakimuangalia kwenye benchi jana Uwanja wa The Hawthorns

Picha: Sitti Mtemvu akanusha kuwa na mtoto, asema ana miaka 23, hatovuliwa taji

Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu amevilaumu vyombo vya habari kwa kueneza habari za uongo kuhusiana umri na maisha yake binafsi. Mtemvu amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. “Ukweli ni kwamba nina miaka 23 na cheti hicho hapo kinajielezea, mkitaka mnaweza kwenda hizo sehemu wanazotoa vyeti mkawauliza,” alisema Sitti. Mtemvu alisema cheti chake cha zamani cha kuzaliwa kilipotea akidai kuwa ni kutokana na maisha yake ya kusafiri mara kwa mara.
Sitti Mtemvu na mama yake wakiondoka baada ya kukutana na waandishi wa habari “Kwahiyo ilibidi pale walipohitaji cheti nilete kingine,” alijitetea. “Sikutegemea hayo maswali leo kwahiyo sikuja nimejiandaa kihivyo,” alijibu mrembo huyo baada ya waandishi wa habari kumtaka awape ripoti yoyote ya polisi kuhusiana na kupotea kwa cheti chake cha mwanzo. Cheti cha kuzaliwa alichonacho sasa kinaonesha kuwa kilitolewa September 9 mwaka huu.
Hashim Lundega akionesha cheti cha kuzaliwa cha Sitti Mtemvu Sitti alitumia pia fursa hiyo kukanusha tetesi kuwa ana mtoto. “Sina mtoto, na mkitaka tunaweza kwenda hospitali sababu naona kama mmekuwa mkiniandama kwa vitu ambavyo si vya kweli,” alisema. Akijibu swali la kuonekana kwa passport yake inayoonesha kuwa alizaliwa mwaka 1989 na huku kwenye cheti alichoonesha kikionesha amezaliwa May 31, 1991, Sitti alisema: Sitogusia hilo suala kwasababu mimi nilivyokuwa nakuja kuomba ‘Umiss Tanzania’ niliombwa cheti cha kuzaliwa sasa hivyo vitu vingine ni personal life, kwahiyo sidhani hata nyie kama kuna mtu atakuja anachukua passport yetu, ama driving licence ya kweli au feki na kuiweka kwenye mtandao kama ni kitu ambacho mngependelea.” Kwa upande wake Mkurugenzi wa Lino International Agency Limited Hashim Lundenga alisema kuwa nafasi ipo wazi kwa wale wenye mashaka na umri na maisha ya Sitti kupeleka vielelezo halisi ambavyo watavifanyia kazi.
Mkurugenzi wa Lino International Agency Limited Hashim Lundenga akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari, kushoto ni Miss Tanzania, Sitti Mtemvu “Tukishapata proof tutazifanyia kazi vizuri sana na mwenye haki atapata. Sisi hatuwezi kumvua taji, vitahusika BASATA na wizara husika,” alisema Lundenga. Kuhusu Sitti kudanganya kuwa na umri wa miaka 18 kama watu walivyodai ndivyo alivyosema, Lundega alidai kuwa hayo yamezushwa mtandaoni na kwenye shindano hilo hakuna aliyesema hivyo. “Unaamini kwamba Sitti ana miaka 18?” alihoji Lundenga. “Sasa kama huamini yote yametoka kwenye vyombo vya habari. Sisi tunaamini cheti cha kuzaliwa, sasa kama kuna mtu ana doubt na cheti cha kuzaliwa aende RITA akafanye uchunguzi wake.”

HILI NI PIGO LINGINE KUBWA LILILOPATA SANAA YA MUZIKI TANZANIA

Msanii wa kundi la TMK Wanaume Family, YP amefariki dunia usiku wa jana katika hospitali ya Temeke baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kifua. YP Akizungumza na mdadusiblog leo, kiongozi wa kundi hilo, Said Fela, amethibitisha msiba huo na kusema ratiba kamili itatoka leo mchana. “Mpaka sasa hivi bado hatujaandaa ratiba, tunasubirika kaka yake kwa sababu huyo mtu kafariki usiku hospitali. Kwahiyo ndugu zake wakishakuja ndo watasema tunazikaje, kwa sababu alikuwa mkristo. Kwahiyo kwenye saa 7 mchana ratiba itakuwa tayari,” amesema Fela. “Tatizo alikuwa anaumwa kifua muda tu, lakini alishaanza kunywa dozi lakini majuzi akazidiwa na tukampeleka hospitali. Jana ndo mwenyezi Mungu kampenda zaidi akamchukua. Wazazi wa marehemu wapo Keko pale, lakini wazazi wake baba na mama walifariki ila ndugu zake wapo, na kuna kibanda waliachiwa na wazazi wake, kwahiyo msiba utakuwa Keko.”

KOCHA WA SIMBA PATRICK PHIRI ANUNUA STAA WA JAGWANI

KOCHA wa Simba, Patrick Phiri, amepanga kufumua kikosi chake katika usajili wa dirisha dogo hapo Desemba ambapo ametamka kuwa anahitaji kuwa na makipa wanne wenye ushindani mkubwa na kusisitiza ni lazima afanye uamuzi mgumu juu ya hilo huku akitaka uongozi umnunulie kipa wa Yanga, Juma Kaseja. Kwa sasa Simba ina makipa watatu; Ivo Mapunda, Hussein Sharif ‘Casillas’ na Manyika Peter ambaye usajili wake ni wa U-20. Hiyo inamaanisha kwamba Kaseja akitua Simba uwezekano wa Mapunda kurejea Ligi Kuu Kenya ni mkubwa kama ilivyoanza kuvumishwa kwani Simba itakuwa na makipa wanne na nafasi yake kucheza itakuwa finyu. Phiri ameliambia Mwanaspoti kuwa alipatwa na wakati mgumu baada ya makipa wake wawili kuumia Ivo na Casillas na kubakiwa na mmoja tu Manyika ambaye hata hivyo alionyesha kiwango cha juu katika mechi yao na Yanga iliyochezwa Jumamosi iliyopita na kutoka suluhu. Baada ya mechi hiyo, Phiri alisema kuwa Manyika ana kiwango kikubwa lakini anahitaji awepo na kipa mbadala huku akitamani kumnasa Kaseja ambaye aliwahi kuidakia Simba kwa miaka 10. “Binafsi huwa namkubali Kaseja kuwa ni kipa bora kutokana na uwezo wake wa kudaka, ningependa kuwa naye kwani nimewahi kumfundisha na ninajua uwezo wake, nina makipa watatu ambao ni wazuri lakini kuelekea mechi ya Yanga wawili walikuwa na majeruhi, nilikuwa katika wakati mgumu ingawa nilimwamini Manyika,” Phiri alisema. “Nikisajili kipa mzoefu itanibidi niwe na uamuzi mgumu katika upangaji kwani ni lazima nikimtumia Manyika kutokana na uwezo aliokuwa nao, nikimkalisha benchi nitaua kiwango chake, atakuwepo kipa namba moja lakini wote watadaka kulingana na mechi zilivyo.” Kaseja kwa sasa hapati nafasi ya kudaka katika kikosi cha Yanga kwani kocha Marcio Maximo amemwamini kipa Deo Munishi ‘Dida’. Kuhusu safu ya ulinzi, Phiri alisema: “Pale kati Joseph Owino na Hassan Isihaka wanatosha sina haja ya kusajili, lakini beki wa pembeni ndio kuna tatizo kwani wapinzani wetu wamegundua tatizo hilo, hivyo nitaimarisha pembeni, kiungo mkabaji ambapo kwa sasa namtegemea sana Jonas Mkude. Nitaongeza na straika mmoja.” Kwa hesabu za Phiri basi uongozi wa Simba ambao msimu huu umesajili wachezaji 29 na kubakiwa na nafasi moja ili wafike 30 watalazimika kupunguza baadhi ya wachezaji wao ili wasajili wachezaji ambao kocha atapendekeza katika nafasi husika. Phiri aliongeza: “Matokeo haya (mfululizo wa sare) sio mazuri kabisa kwetu, tunahitaji ushindi, lakini pia ni bora tumetoka sare na Yanga kuliko wangetufunga maana ingeleta shida zaidi, tunaenda kucheza na Prisons ambao sijawaona uwezo wao hivyo lazima niongeze mbinu za kiufundi kuhakikisha ushindi ugenini unapatikana.” Simba ilianza mazoezi yake jana Jumatatu jioni, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

ALIYEBANWA NA CANNAVARO, YONDANI AWAPIGA MAN UNITED BONGE LA BAO

Yule mshambuliaji wa timu ya taifa ya Benin aliyeshindwa kufurukuta mbele ya mabeki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani jana amepiga bonge la bao akiichezea timu yake dhidi ya Manchester United. Stephane Sessegnon amefunga bao hilo kwa shuti kali la kasi ya kilomita 91 kwa saa na kuifanya West Bwrom iongoze kwa bao moja dhidi ya Man United. Mshambuliaji huyo alitua jijini Dar es Salaam na kuingoza Benin iliyotandikwa kwa mabao 4-0 dhidi ya Taifa Stars. Bao lake lilikuwa moja ya mabao manne bora kwenye mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya bao 2-2.

DUNIA INA MAMBO: DAWA YA KUKAMATA WEZI YAZUA BALAA...

Watu saba kati ya 100 Kijiji cha Kenyamanyori, Kata ya Turwa, Wilaya ya Tarime walioshiriki kunywa dawa ya mganga wa kienyeji aliyeletwa kutoka Busia nchini Kenya wameingia kwenye wakati mgumu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya kulipa Sh3 milioni kila mmojaWanakijiji hao walikusanyika juzi asubuhi baada ya kengele ya kijiji kugongwa na uongozi, huku wakieleza kwamba ilikuwa siku ya nne kwa kengele hiyo kugongwa lengo likiwa ni kuzungumzia wizi unaoendeshwa na watu wasiojulikana.Inadaiwa wizi wa kuvunja maduka umekithiri kijijini hapo, baada ya wanakijiji hao kuwasili eneo la mikutano, walielezwa kusudio la kengele kuwa ilikuwa ni kutokana na kukithiri kwa matukio ya uhalifu. Miongoni mwa waliovunjiwa duka ni Ayubu Wambura, anayedaiwa kuleta mganga kutoka Busia nchini Kenya kuwabaini wahusika, hivyo kila mmoja aliombwa kunywa dawa ya mganga huyo au kuacha maana ni hiyari.

 BOFYA HAPA KUSOMA ZAID 

NDOA YA RAIS WA DUNIA MATATANI SOMA HAPA HABARI KAMILI LIVE!!

WASHINGTON -Michelle Obama has had enough. According to a bombshell new report, the First Lady and Barack Obama are sleeping in separate White House bedrooms. Michelle is also preparing to boot her hubby of 21 years out of their ritzy Chicago home - and seriously discussing divorce. “The smart money says the marriage is doomed,” a source told the National Enquirer. “Barack and Michelle have had a rocky go for years and mainly stayed together for their daughters and his political career. “But now Michelle is mad AS hell. She feels violated in front of the whole world, and screamed at him, ‘I’ve had enough.’ “She’s met with divorce lawyers and told Barack that she wants a life apart from him. “Michelle will stay in the White House for the rest of Barack’s term for appearances’ sake, but she made it clear they’ll be leading separate lives. “She’s moving into one of the vacant bedrooms in the family’s private living quarters, and she’s preparing to move his clothes and personal things out of their million-dollar house in Chicago.” Michelle was left furious after Barack was photographed brazenly flirting with Denmark’s dishy female prime minister, Helle Thorning-Schmidt, during the service for former South African president Nelson Mandela. Obama, 52, laughed and whispered with the 46-year-old Danish beauty throughout the solemn ceremony, at one point cavalierly caressing her shoulder. “Barack already had enough headaches with his public approval rating plummeting after the disastrous rollout of his ‘Obamacare’ health plan. Now he’s walked smack into the worst marital crisis of his life,” said the White House insider.

PERUZI KURASA ZA MBELE NA NYUMA ZA MAGAZETI MBALIMBALI YA LEO JUMANNE ...HAPA