Wednesday, October 22, 2014
|
KOCHA mstaafu, Sir Alex Ferguson amesema
hakuwa na cha kufanya juu ya taratibu
zilizotumika kumfukuza David Moyes katika
klabu ya Manchester United Aprili mwaka
huu na kwamba alichanganyikiwa baada ya
kugundua hilo.
Ferguson alimchagua Moyes kuwa mrithi
wake Old Trafford mwaka uliopita baada ya
kustaafu na katika kitabu chake cha sasa
ameandika kwamba alikuwa kizani dhidi ya
uamuzi uliochukuliwa kumfukuza Mscotland
mwenzake huyo.
"Nilikuwa Aberdeen wakati hilo linatokea",
amekumbushia.
"Jumatatu, nilikuwa nasafiri kurudi
Manchester na aliyekaa pembeni yangu
alikuwa ni kijana ambaye anasoma gazeti
lenye habari: "David Moyes kufukuzwa".'
Sir Alex Ferguson (kushoto) alikabidhi
mikoba yake Manchester United kwa David
Moyes (kulia)
Moyes alifukuzwa baada ya kipigo cha 2-0
kutoka kwa Everton Aprili mwaka huu, akiwa
ameshinda asilimia 50 tu ya mechi zake
Ferguson akasema alichganyikiwa katika
ndege akiwa anarejea Manchester na
hakuwa na uhakika ajibu vipi meseji
aliyotumiwa na Moyes.
"Sikuwa na hakika mini kilitokea kwa wakati
huo haswa," ameandika akizungumzia
meseji hiyo.
Ferguson ameasema: "Nikazungumza na
(Mtendaji Mkuu) Ed Woodward niliporejea na
akasema uamuzi wa mwisho wa
waliochukua.'
Kwa Moyes, Ferguson pia amesema kwamba
kocha huyo wa zamani wa Everton ana
safari ndefu akiendelea kusaka kazi
mpya. "Katika rekodi yake itaonyesha
kwamba aliteuliwa kuwa kocha wa
Manchester United, kitu ambacho ni nadra,".
Moyes alimaliza katika nafasi ya saba akiwa
Manchester United msimu uliopita, na wakati
Mscotland huyo anaondoka United aliacha
rekodi mbaya zaidi ya mechi za nyumbani
tangu mwaka 1978 na pointi chache zaidi
katika historia ya Ligi Kuu ya England.
Bado alikuwa ana asilimia nzuri ya ushindi
zaidi ya Sir Matt Busby, lakini alipoteza
mechi 11 kama kocha wa United, akiruhusu
mabao 40 katika mechi 34, kabla ya
kufukuzwa siku mbili baada ya kipigo cha
2-0 kutoka kwa Everton, Aprili 22, mwaka
huu katika Ligi Kuu.
Ryan Giggs alikaimu nafasi yake kumalizia
msimu kabla ya Mholanzi, Louis Van Gaal
kuajiriwa msimu huu. Hata hivyo, bado
United haijawa na mwenendo mzuri chini ya
kocha mpya, licha ya kumwaha fedha nyingi
kusajili nyota kadhaa. |
0 comments:
Post a Comment