Wednesday, October 22, 2014
|
BARCELONA imeshinda mabao 3-1 dhidi ya
Ajax katika mchezo wa Kundi F Ligi ya
Mabingwa Ulaya usiku huu wa Camp Nou.
Neymar alianza kuifungia Barcelona dakika
ya nane kabla ya Lionel Messi kufunga la
pili dakika ya 24, Muargentina huyo
akitimiza jumla ya mabao 69 aliyofunga
katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Messi alifunga bao lingine ambalo
lilikataliwa na refa kwa kuwa aliotea dakika
ya tatu ya kipindi cha pili, lakini Sandro
Ramirez aliyetokea benchi akaifungia Barca
bao la tatu dakika za majeruhi.
Bao pekee la Ajax lilifungwa na Anwar El
Ghazi aliyetokea benchi pia. Neymar na
Messi wote walipumzishwa kabla ya dakika
ya 66 kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi wa
El Clasico dhidi ya Real Madrid.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, PSG
imeifunga 1-0 APOEL Nicosia, wakati Kundi
H, Shakhtar Donetsk imeichapa 7-0 BATE
Borisov na FC Porto imeilaza 2-1 Athletic
Bilbao. |
0 comments:
Post a Comment