Wednesday, October 22, 2014
|
Aliyekuwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, YP
ambaye amefariki usiku wa jana katika hospitali
ya Temeke wakati alipokuwa akitibiwa maradhi
ya kifua kikuu (TB) anatarajiwa kuzikwa siku ya
kesho katika makaburi ya Chang’ombe jijini Dar
es Salaam.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu, YP ambaye
jina lake halisi ni Yessaya Ambilikile ameugua
kwa kipindi cha takribani miezi 2 kabla ya
kufikwa na umauti hapo jana. |
BOFYA HAPA KUTAZAMA PICHA
0 comments:
Post a Comment