Tuesday, October 21, 2014
|
WINGA Angel di Maria alionekana hayuko
vizuri akiwa ameketi kwenye benchi la
Manchester United usiku wa jana, huku
amekandamizia barafu katika nyonga yake
kwenye mchezo huo ulioisha kwa sare ya
2-2 na West Bromwich Albion.
Muargentina huyo, aliyesajiliwa kwa dau la
rekodi United, alikuwa kivutio Uwanja wa
The Hawthorns, lakini kulikuwa kuna
wasiwasi juu ya kiungo huyo baada ya
kutolewa dakika ya 76.
Di Maria amekuwa katika kiwango babu
kubwa tangu asajiliwe kwa Pauni Milioni 60
kutoka Real Madrid msimu huu na
ameendeleza mwanzo wake mzuri usiku wa
jana. Alimsetia Marouane Fellaini kufunga bao la
kusawazisha kipindi cha pili, kabla ya
kumpisha Ashley Young. Amecheza mechi
tano hadi sasa Manchester United na
amefunga mabao matatu na kusaidia
manne. |
|
Di Maria (aliyekaa chini kulia) akiwa
amekandamizia barafu kwenye nyonga yake
huku Chris Smalling, Ander Herrera na Ryan
Giggs wakimuangalia kwenye benchi jana
Uwanja wa The Hawthorns |
0 comments:
Post a Comment