Thursday, October 23, 2014
|
Arsenal imejitutumua na
kuibuka na ushindi wa
mabao 2-1 ikiwa ugenini
katika mechi ya Ligi ya
Mabingwa Ulaya.
Arsenal imeichapa
Anderletch ya Ubelgiji
katika mechi hiyo
iliyoonekana itaisha kwa
wenyeji kushinda lakini
Arsenal ikafunga mabao
mawili katika dakika
mbili.
Keran Gibbs alifunga bao
la kusawazisha katika
dakika ya 89, kabla ya
Lukas Podolski kufunga la
pili katika dakika ya 90. |
0 comments:
Post a Comment