Tuesday, October 21, 2014

MSIBA MWINGINE TENA....! BAADA YA KUONDOKEWA NA YP HUYU NI MSANII MWINGINE ALIYEFARIKI SIKU YA LEO

Ni masaa machache tu yamepita tangu muziki wa kizazi kipya Tanzania, Bongo Fleva kumpoteza aliyekuwa staa wa muziki huo kutoka kundi la TMK Wanaume Family, aliyekuwa akifahamika kwa jina la YP, taarifa nyingine ya simanzi inahusu msiba wa aliyekuwa muigizaji wa Bongo Muvi. Katika ukurasa wake wa instagram, muigizaji na mchekeshaji maarufu anayefahamika kwa jina la Kitale ama Mkude Simba (@mkudesimbaoriginal), amepost picha ya muigizaji aliyefariki masaa machache yaliyopita pia. Shery Mwana Kwa mujibu wa Kitale, muigizaji huyo ambaye jina lake halisi ni , aliwahi kushiriki na Kitale katika movie mbali mbali ikiwemo Kipotabo na Nyumba Nne.

0 comments:

Post a Comment