Saturday, November 01, 2014

DE GEA MCHEZAJI BORA WA MWEZI MAN UNITED KWA ASILIMIA 70

MASHABIKI wa Manchester United
wamemchagua kipa David de Gea kuwa
Mchezaji Bora wa mwezi Oktoba wa klabu
hiyo, baada ya Mspanyola huyo kupata
asilimia 70 ya jura zilizopigwa kwenye
mtandao.
Licha ya kushindwa kuzuia nyavu zake
kutikiswa katika mchezo wowote mwezi huo,
De Gea alikuwa katika kiwango kizuri wakati
United ikiifunga Everton kabla ya kutoa sare
na West Brom ugenini na baadaye na vinara
wa Ligi Kuu England, Chelsea nyumbani.
Mlinda mango huyo mwenye umri wa miaka
23 alipangua mkwaju wa penalti Leighton
Baines na kuokoa michomo miwili ya hatari
ya The Toffees dakika za mwishoni,
kuiwezesha timu ya Old Trafford kupata
pointi moja, kabla ya kuokoa mchomo
mwingine wa Eden Hazard wakati Mbelgiji
hjuyo alipopata nafasi nzuri ya kufunga timu
hiyo ikitoka 1-1 na kikosi cha Jose
Mourinho.

ARSENAL YAUA 3-0 ENGLAND, SANCHEZ MBILI PEKE YAKE

ARSENAL imeng’ara katika Ligi Kuu ya
England kufuatia ushindi wa mabao 3-0
dhidi ya Burnley Uwanja wa Emirates,
London.
Hadi mapumziko hakuna bao lililokuwa
limepatikana na iliwachukia hadi robo ya
mwisho ya mchezo, The Gunners kuanza
kuhesabu mabao yao.
Alexis Sanchez alifunga bao la kwanza
dakika ya 70, kabla ya Callum Chambers
kuongeza la pili dakika ya 72 na Sanchez
tena kuwainua vitini mashabiki wa Arsenal
dakika ya 90.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa; Szczesny,
Chambers, Mertesacker, Monreal, Gibbs,
Arteta/Ramsey dk63, Flamini, Oxlade-
Chamberlain/Walcott dk80, Cazorla, Sanchez
na Welbeck/Podolski dk80.
Burnley; Heaton, Trippier, Duff, Shackell,
Ward, Arfield 6, Jones, Marney/Chalobah
dk80, Boyd, Ings na Sordell/Jutkiewicz d

RONALDO AFUNGA REAL MADRID IKISHINDA 4-0 LA LIGA NA KUPANDA KILELENI

REAL Madird imeichapa Granada mabao 4-0
katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania,
maarufu La Liga jioni ya leo Uwanja wa
Nuevo Los Carmenes.
Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano
Ronaldo aliifungia Real Madrid bao la
kwanza dakika ya pili, kabla ya James
Rodriguez kufunga la pili kipindi cha kwanza,
Karim Benzema kufunga la tatu dakika ya 54
na James Rodriguez kukamilisha ushindi huo
dakika za mwishoni.
Ushindi huo, unaifanya Real ipae kileleni
mwa La Liga kwa kufikisha pointi 24 baada
ya kucheza mechi 10, lakini imecheza mechi
moja zaidi dhidi ya Barca, wanaochuana nao
kwenye mbio za ubingwa.

Friday, October 31, 2014

TORRES AFUNGUKA RASMI KUHUSU MOURINHO JUU YA KUONDOKA KWAKE CHELSEA

Mshambuliaji nyota wa Chelsea anayekipiga AC Milan kwa mkopo amesema hakuondoka katika klabu hiyo ya London kwa kulazimishwa na Kocha Jose Mourinho. Torres raia wa Hispania amesema ulikuwa ni uamuzi wake kufanya na maneno yake yameondoa taarifa za utata kwamba Mourinho ndiye alimtaka kwenda Milan kwa mkopo wa miaka miwili.

RASMI ANGA FIFA YAACHIA NEMBO YA KOMBE LA DUNIA 2018, WANA ANGA WA WAITANGAZA

NEMBO ITAKAYOTUMIKA KWENYE KOMBE LA DUNIA MWAKA 2018 NCHII RUSSIA IMEANIKWA HADHARANI KUPITIA WANA ANGA WA NCHI HIYO. WALE JAMAA AMBAO HUENDA MWEZINI. SASA IKO WAZI NA INAJULIKANA IKIWA NI BAADA YA ILE YA ZAKUMI YA AFRIKA KUSINI MWAKA 2010 NA ILE YA BRAZIL 2014.

Wednesday, October 29, 2014

RONALDO APIGA HAT TRICK YA TUZO LA LIGA, MESSI AAMBULIA PATUPU

Cristiano Ronaldo amekomba zawadi tatu 'hat trick' za tuzo ya wachezaji bora Ligi ya Hispania maarufu kama La Liga. Huku mpinzani wake Lionel Messi akiambulia patupu, tuzo tatu alizobeba Ronaldo ni pamoja na Mchezaji Bora, Mfungaji Bora na Mshambuliaji Bora wa La Liga. Ilikuwa furaha kubwa kwa Ronaldo ambaye aliongozana na mpenzi wake Iryna Shayk, mwanamitindo kutoka Urusi. Pamoja na Ronaldo kubeba tuzo hizo, timu yake ya Real Madrid imetawala zaidi kuliko klabu nyingine ya Hispania. Zawadi ya kiungo bora imekwenda kwa Luka Modric huku Sergio Ramos akichukua tuzo ya beki bora. Kipa mpya wa Real Madrid, Keylor Navas amechukua tuzo ya mlinda mlango bora. Kabla ya kutua Madrid, Navas alikuwa akikipiga Levante. Barcelona pia imefanikiwa kupata tuzo tatu, Andrés Iniesta alitangazwa kuwa kiungo bora mshambuliaji, huku Ivan Rakitic na Rafinha wakitwaa tuzo mbili za Fair Play and Breakthrough. Kutokana na mafanikio makubwa msimu uliopita, Kocha wa Atlético, Diego Simeone alibeba tuzo ya Kocha Bora. Mshambuliaji nyota wa Sevilla, Carlos Bacca akachukua tuzo mchezaji Bora kutoka Amerika Kusini na Yacine Brahimi wa Granada akawa Mchezaji Bora kutoka Afrika.

RAY C AHAMUA KUMFUTIA KESI CHID BENZ KESI!

Rehema Chalamila ‘Ray C’. WAKATI nyota wa muziki wa Hip Hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’ akikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa na madawa ya kulevya akiwa njiani kuelekea Mbeya, Rehema Chalamila ‘Ray C’ aliyekuwa amemfungulia kesi ya kumpiga katika kituo cha Polisi cha Oysterbay, amefuta shauri hilo na kumsamehe. Akipiga stori na gazeti hili, Ray C alisema ameamua kumsamehe kwa sababu yeye ni mtu wa Mungu na anaamini yanayomtokea ni ishara ya kumtambulisha kuwa matumizi ya dawa za kulevya hayafai. “Mimi ni mtu wa Mungu, nimemsamehe na wala sitaki kesi naye, lakini kumsamehe mimi peke yangu hakusaidii, Watanzania wote kwa pamoja tumuombee ili jambo hili limalizike na likiisha, ninamuomba aje tushiriki pamoja katika tiba ya Methadone,” alisema. Ray C maarufu kama kiuno bila mfupa, alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuandika waraka katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram, akimsihi Chid Benz kuachana na matumizi hayo ya madawa ya kulevya.
Nyota wa muziki wa Hip Hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’. “Pole kaka yangu Chid Benz, naumia kuona tatizo ulilokuwa nalo bado haujalitafutia jibu, mimi ni dada yako na tumeshafanya kazi pamoja. Tatizo ulilonalo na mimi nilishakuwa nalo na niliweza kulitatua sababu nilijitambua na kutafuta suluhu, nimejaribu kila njia kukushauri badala yake ukaja na rungu la kimasai na kunitandika nalo nyumbani kwangu,” yalisomeka baadhi ya maandishi yake mtandaoni. Ray C aliendelea kuandika kuwa kitendo cha kukamatwa kwake na madawa hayo kitakuwa ni jibu zuri kwake kuwa anakoenda si salama na kumtaka abadili njia na kuungana naye kwenye tiba ya Methadone kwani ndiyo kiboko ya madawa ya kulevya.
Kamanda Nzowa. Chid Benz alikamatwa akiwa na kete 14 za madawa ya kulevya pamoja na misokoto miwili ya bangi hadi gazeti hili linakwenda mtamboni, alikuwa bado hajafikishwa mahakamani kukabiliana na tuhuma hizo.

HIKI NDO KITU KIKUBWA ALICHOKIFANYA BALOTEL AKITOKEA BENCHI USIKU HUU DHIDI YA SWANSEA

KLABU ya Liverpool imeichapa Swansea mabao 2-1 katika mchezo wa Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Capital One Cup usiku huu Uwanja wa Anfield. Jordan Henderson alipewa beji ya Unahodha, kocha Brendan Rodgers akifanya mabadiliko ya wachezaji tisa katika kikosi chake cha kwanza. Winga wa Swans, Marvin Emnes aliifungia timu yake bao la kwanza dakika ya 65, kabla ya Mario Balotelli aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Rickie Lambert kusawazisha zikiwa zimesalia dakika tano. Federico Fernandez alitolewa kwa kadi nyekundu dakika za mwisho kwa kumchezea rafu Philippe Coutinho kabla ya Dejan Lovren kuifungia Liverpool bao la ushindi dakika za majeruhi na kuwapeleka Wekundu hao Robo Fainali.

CPL:MATOKEO YA CHELSEA vs SHREWBURY HAYA HAPA

KLABU ya Chelsea imetinga Robo Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup baada ya kuichapa mabao 2-1 Shrewsbury usiku huu. Chelsea ilipata bao la kwanza mapema tu kipindi wakati mkongwe, Didier Drogba alipomalizia pasi maridadi ya mwanasoka wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah. Lakini Shrewsbury ikapata bao la kusawazisha kupitia kwa Andrew Mangan aliyetokea benchi dakika ya 77, kabla ya Jermaine Grandison kujifunga dakika nne baadaye kuipa ushindi timu ya Jose Mourinho.

Tuesday, October 28, 2014

Kingine alichozungumza Jackie Chan kuhusiana na mtoto wake kukamatwa na dawa za kulevya.

Mkali wa movie kutoka Hong Kong China, Jackie Chan ameomba vyombo vya habari ‘vijichunge’ na namna vinavyoandika taarifa kuhusiana na kitendo cha mtoto wake kukamatwa na dawa za kulevya kwa kuwa kufanya hivyo si kumuumiza yeye (Jackie Chan) bali ni kumuumiza mama wa mtoto huyo. Jackie Chan amesema kupitia tukio hilo amejifunza kuwa baba bora kitu ambacho hakukijua siku za nyuma. Mtoto wa staa huyo, Jaycee Chan alikamatwa kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi zaidi ya gramu 100 ndani ya nyumba yake, na baadaye kushitakiwa kwa kuuza dawa hizo. Jackie Chan ambaye amekuwa balozi wa kupinga dawa za kulevya tangu mwaka 2009, amesononeshwa na pia ameomba radhi kwa kosa alilotenda mwanae ambapo hii imekuwa mara yake ya kwanza kujibu swali linalohusiana na kesi ya mtoto wake, akisema kupitia hilo amejifunza kuwa baba bora.

Monday, October 27, 2014

NUH MZIWANDA AHAMUA TENA KUWANYAMAZISHA WANAFKI KWA KUCHORA TATOO NYINGINE YENYE PICHA YA MPENZI WAKE SHILOLE

Wakati Nick Cannon ametoka kufunika Tattoo yenye jina la mke wake Mariah Carey ambaye wametengana kwa kuongeza mchoro mwingine juu yake hivi karibuni, msanii wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda ameongeza Tattoo ya pili ya mpenzi wake Shilole kwenye mkono wake. Nuh amesema mchoro huo wa pili kwenye mwili wake una sura ya Shishi baada ya ile ya kwanza ambayo ni jina la ‘Shishi Bybee’. “Tattoo ya pili ni sura aisee sura ya mpenzi wangu Shishi,” ameiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm. “nimetaka kuweka maana ya jina pamoja na sura yake unajua jina tu lilikuwepo kukamilisha upendo ule na thamani na shkurani kwake so nilichora ile Shishi Bybee ya maneno halafu baadae nimechora sura yake, nimechora mkono ule ule, so hii shishi Bybee iko nyuma ya mkono wangu halafu hii sura yake iko mbele.”
Mziwanda ameongeza kuwa mchoro huo umegharimu shilingi laki nne na nusu. “Tattoo nimechora juzi, tumetumia kama laki nne hivi nne na nusu ukijumlisha na usafiri sababu jamaa alikua katoka Arusha. Ile ya mwanzo iligharimu kama laki mbili mbili na nusu”.

Sunday, October 26, 2014

HII NDO TIMU ANAYOTARAJIA KUTUA DAVID MOYES

KOCHA David Moyes yumo kwenye orodha fupi ya mwisho ya makocha wanaotakiwa na Inter Milan ya Italia inayotaka kumtimua kocha wake wa sasa, Walter Mazzarri. Kocha huyo wa zamani wa Manchester United na Everton anapewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya Mazzarri, ambaye timu yake inacheza na Cesena leo akiwa katika shinikizo baada ya mwanzo mbaya unaoifanya Inter iwe katika nafasi ya tisa kwenye msiamo wa ligi hivi sasa. Moyes mwenyewe amekua akiamini akipata nafasi ya kufundisha klabu nje ya Uingereza itakuwa ni fursa nzuri kwake kurejesha heshima yake- hivyo akifanikiwa mpango huo atakuwa ametimiza ndoto zake kwa sasa.

Saturday, October 25, 2014

JE UNAFAMAMU NI WASANII GANI WA BONGO WALIMSHTUA SANA DAVIDO KWENYE FIESTA 2014 DAR

Unaambiwa weekend iliyopita kwenye Fiesta ya Dar es salaam mwimbaji Davido wa Nigeria alitumia dakika zake zote kutazama screen zilizokua zimewekwa nyuma ya stage ya Fiesta baada ya kusikia shangwe zilizokua zinapigwa baada ya Wakali wengine kupewa time ya kumiliki stage. Alilazimika kutazama TV hizo kwa umakini baada ya kuona shangwe walilopata WEUSIambapo mashabiki walikua wanaimba nyimbo zao kwa muda mrefu ambapo Davido kabla ya kuuliza alitumia muda mrefu kuwatazama kwa makini baada ya kushangazwa na shangwe walilokua wanapata WEUSI hawa.
Baada ya Wakali hawa kumaliza show Davido alianza kuuliza ni kina nani na wana umaarufu kiasi gani ambapo mmoja wa marafiki zake amesema stori hazikuishia uwanjani kwenye Fiesta bali mpaka Hotelini Davido alionyesha kushangazwa na shangwe la WEUSI na kuwaongelea tena. Hii itafanya idadi ya Wasanii wa bongo wanaofahamika na Davido iongezeke manake alipokuja juzi Tanzania alihojiwa muda mfupi tu baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege na kusema msanii pekee wa Tanzania anaemfahamu ni Diamond Platnumz. Mengine aliyoyasema ni kwamba kwenye album yake mpya inayotoka mwanzoni mwa 2015 wameshirikishwa wasanii wachache kutoka Afrika ambao ni pamoja na Diamond na Mafikizolo na kwamba kuna wasanii wawili wakubwa wa kimataifa aliowashirikisha ambao hatowataja kwa sasa

HII NDIO HISTORIA YA MZIKI YA MAREHEME YP KUTOKA TMK WANAUME FAMILY

Wiki hii hapa tasnia ya bongofleva ilimpoteza msanii maarufu YP pichani ambaye anaunda kundi la TMK Wanaume Family.Msanii huyo ambaye jina lake halisi ni Yessaya Ambikile alifariki usiku wakuamkia Jumanne katika hospitali ya Temeke.
Said Fella ambaye ni meneja wa kundi hilo amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kifua kwa muda mrefu na ndo kitu ambacho kimechukua uhai wake.
Historia yake katika muziki:
Saidi Fella anasema kuwa alikutana na marehemu YP kwa mara ya kwanza mwaka 2004 katika ukumbi wa King Palace huko Temeke.Baadae kulikuwa na shoo ya TMK Wanaume Family katika ukumbi wa Luxury Pub marehemu akamfata akaomba amsaidie kimziki, ndipo Fella akamwambia amwimbie, akamwimbia wimbo wake uliokuwa unaitwa ‘Saidali’ na huo ndo ukawa mwanzo wakuitwa kwenye kundi hilo. Alivyofika kwenye kundi baada ya kumwambia Juma Nature kuhusu kipaji cha marehemu, Nature akamwambia kama yeye Fella ameona marehemu ana uwezo basi ni sawa apewe nafasi katika kundi hilo.

Mwaka 2005 marehemu pamoja na msanii mwingine wa kundi hilo Y Dash akatoa wimbo wao wa kwanza ‘Shemsa’ ambao ulifanya vizuri na kumtambulisha msanii huyo kwenye tasnia ya muziki.Kutokana na sauti ya marehemu kuendana na msanii mwenzake Y Dash wakatoa wimbo mwingine uliokuwa unaenda kwa jina la ‘Pumzika’.

Said Fella aliendelea kueleza kuwa marehemu alitoa wimbo ulioenda kwa jina la ‘Mapengo matatu’ ambao ni wimbo alioimba kutokana na kufiwa na baba yake,mama yake na mdogo wake.Mwaka 2006 marehemu pamoja na Y Dash ambaye kwasasa yuko nchini Afrika Kusini wakatoa album ya pamoja waliyoipa jina la ‘Mapengo matatu’.
Baada ya hapo marehemu akaendelea kushiriki kwenye kazi zingine za wasanii wa kundi la Tmk Wanaume Family na kazi za kundi kama ‘Twende zetu’ , ‘Dar mpaka Moro’, ‘Kichwa kinauma’ na nyingine nyingi.

Mwaka 2008 marehemu aliamua kuondoka katika kundi hilo na msanii mwenzake Y Dash pamoja na Jebby wakaenda kundi lingine ambalo walilipa jina la TMK Unity.Said Fella anasema mwaka 2010 msanii huyo alimtafuta nakumuomba kurudi katika nafasi yake tena ndipo alipomkubalia nakuwa kwenye kundi hilo mpaka kifo chake.Baada yakurudi TMK Wanaume Family nyimbo ambazo alizoshiriki marehemu nakufanya vizuri ni ‘Kichwa kinauma’, ‘Tunafurahi’ ya Mh Temba na Chegge.

Meneja huyo wa kundi hilo anasema kuwa kundi hilo limepata pengo kwasababu toka mwanzo kabla wakati TMK Wanaume Family kuvunjika msanii huyo alikuwa ni kati ya wale wasanii 11 wa mwanzo.Said Fella alifanunua kuwa alikuwa akianza Juma Nature,Chegge,Kr,Mh Temba na wengine na yeye YP anakuwa na namba.Kitu kingine alisema kuwa watamkumbuka YP kwa ucheshi na ubunifu wa staili za kucheza. “Yaani zile staili zote za TMK Wanaume Family kama mapangashaa nyingi alikuwa akizibuni marehemu pamoja na Kr, alikuwa ni mtu anayependa kucheza, mtu wakutengeza step”, Said Fella.Alieleza kuwa kazi ya mwisho ya kundi marehemu kurekodi ilikuwa ni mwezi uliopita katika studio za Sound Crafters.

Marehemu,Mh Temba na Chegge
Pia msanii wa kundi hilo Chegge alimzungumzia marehemu nakusema kuwa alipatwa na uchungu hadi anajikuta analia kwasababu watu wengi walikuwa wakizifananisha sauti zao na ndo maana alipenda kumshirikisha kwenye nyimbo zake.Msanii mwingine wa kundi hilo Mh Temba alisema kuwa atakumbuka ucheshi wa marehemu na pia ubunifu wake katika kutunga viiitikio(chorus) za nyimbo. “Kwakweli TMK Waunaume Family tumepoteza jembe.

Marehemu Yessaya Ambikile alizikwa jUZI katika makaburi ya Chang’ombe Maduka mawili alizaliwa tarehe 10 November mwaka 1986 jijini Dar es salaam akiwa ni mtoto wa kwanza, kisha akapata elimu ya msingi katika shule ya msingi Keko Magurumbasi.Baada yakumaliza elimu ya msingi marehemu hakuendelea na masomo akaanza kujishughulisha na muziki mpaka kifo chake.Marehemu ameacha mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miaka 8 pamoja na mzazi mwenzake ambaye alikuwa ana mpango wakufunga ndoa hivikaribuni.
Mungu ampuzimshe kwa amani YP.

HAYA NDIO MAKOSA MATATU MAKUBWA DIAMOND ALIYOWAKOSEA WATANZANIA HADI WANAMZOMEA NA KUMCHUKIA….

Katika pitapita zangu Instagram nkakutana na picha na maneno yaliyoandikwa na mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Bikira Wa Kisukuma. Baada ya kusoma nkasema sio mbaya kama ntashea kilichoandikwa na Bikira kwa wasomaji wangu wa Bongoclan. Hebu soma na kisha tupe maoni yako je ni kweli kua Diamond kafanya makosa haya??????

“DIAMOND ANA MAKOSA 3 MAKUBWA ALIYOTUTENDEA WATANZANIA:

1.Kosa la kwanza ni KUWA NA BIDII KWENYE MUZIKI WAKE…Hili ni kosa kubwa sana kwa Watanzania..Hakupaswa kuwa na bidii hivi..Angekuwa tu wa KAWAIDA kama wenzake waliopita ili AFULIE awaachie na wengine waje kwenye chati arudi Tandale kuuza Wali..

2.Kosa la 2 ni KUJITAMBUA YEYE NI NANI..Kwanini ajitambue wakati wenzie wenye majina walishindwa??Kwani yeye nani awe tofauti??Hii ni DHARAU KUBWA sana kwa Watanzania na Wanamuziki wenzie na inaonyesha ana KIBURI..Diamond kujua yeye ni Mwanamuziki mahiri na kutumia VALUE yake aliyoipata kwa mbinde kuiletea sifa Tanzania nje ya Mipaka ni KOSA KUBWA!

3.Kosa lake la 3 ni KUUHESHIMU MNO MUZIKI UNAOMPA HELA…Kwanini asiwe kama wakina Mr nanihii tu,kwani wao hawakuhit kama yeye?Mbona waliishi kawaida tu na kuuchukulia muziki poa hadi walipofulia na leo hata wakiingia Masai Club nobody cares..Kwani kufulia kitu gani?Diamond hakupaswa kuuheshimu Muziki kama kazi..Angefanya bora liende tu aimbe imbe yaishe..Sasa kujifanya Anatoa Collabo mara Davido mara Mafikizolo mara Trey Songs na K’Cee na Yemi Alade AMETUMWA NA NANI??Huku ni kutafuta sifa tu alipaswa awe mdogo milele awaachie na wenzie.. Kwa makosa haya ma3 WATANZANIA wameamua kumuadhibu..Diamond Anaringa…Ana dharau sana..Anaupenda sana Muziki uliompa JINA..HESHIMA..PESA..na ametafutiwa REPLACEMENT kwa sababu tu ANAHESHIMU MUZIKI KAMA KAZI na sio JUST SINGING FOR FAME…Watanzania tumeamua kuadhibu MTU ANAYEHESHIMU KAZI YAKE iliyomtoa from Zero to Hero na tutamshusha kwa lazima taji apewe mwingine..Watanzania tunataka Diamond awe another Mr Nice ili tupate kitu cha KUCOMPARE…Shida yetu kuu wala sio dharau ila ni KWANINI DAI HASHUKI???? Hardwork Pays! Respect Pays! Knowing Your Value Pays! Kama alimpandisha MUNGU…Hakuna wa kumtoa pale… Nasibu..wakomeshe..Toa ule wimbo na MAFIKIZOLO wiki ijayo tuone kama watazomea Spika za redio zao…

CRD BONGOCLAN

DIAMOND AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KILE KILICHOMKUTA KIWA POLISI, SOMA HAPA…..

Dar es Salaam. Mwanamuziki Nassib Abdul, ‘Diamond Platnumz’ amesalimisha nguo zake za kijeshi kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Diamond alisema kuwa juzi alipokea wito uliomtaka afike kituoni hapo (Oysterbay) akiwa na madansa wake pamoja na nguo hizo. Alisema haikuwa rahisi kwake kutii amri ya vyombo vya dola kwani alikuwa na woga kutokana na kutokuwa na rekodi ya yoyote ya matukio ya uhalifu. “Nisingeweza kukaidi amri ya dola, nilifika na yale mavazi na nikahojiwa kwa saa kadhaa. Nikaeleza kwamba yalikuwa yakifanana na ya jeshi na hayakuwa sare rasmi za jeshi hilo, kikubwa nilihitaji kumaliza tatizo,” alisema nyota huyo aliyetajwa kuwania tuzo za MTV EMA zinazotarajiwa kufanyika Novemba 9 mjini Glasgow, Scotland. Diamond alisema si kweli kwamba alichukuliwa dhamana na Chifu Kiumbe, ila ukweli ni kwamba alisindikizwa na mdau huyo wa sanaa nchini kama kaka yake kutokana na woga aliokuwa nao, lakini hakushikiliwa na kutakiwa dhamana yoyote.

ALIKIBA AFUNGUKA KUHUSU TUHUMA ZA KUKODI WATU WA KUMZOMEA DIAMOND FIESTA

Alikiba ameiambia Bongo5 kuwa hajui uvumi huo umeanza vipi. “Hamna ukweli wowote, naanzaje?,” amehoji. “Siwezi kufanya kitu kama hicho. Kikubwa ni kuwashukuru wana Dar es Salaam walivyonipokea, nimefurahi sana. Hii imenitia moyo na kunifanya niongeze bidii kuwaandalia vitu vizuri zaidi.” Katika hatua nyingine, msanii huyo amesema mashabiki wa muziki wake

 BOFYA HAPA KUSOMA ZAID 

MOURINHO AELEZA KUHUSU DIEGO COSTA KUCHEZA AU KUTOCHEZA KWENYE MECHI DHIDI YA MAN UNITED JUMAPILI HII

KOCHA Jose Mourinho ameghairi kumuweka benchi mshambuliaji Diego Costa katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Manchester United Jumapili. Mshambuliaji huyo wa kati wa Hispania, amekosa mechi mbili zilizopita katokana na maumivu ya nyama na wiki hii alipelekwa hospitali kwa tiba ya tatizo hilo. Lakini Mourinho, ambaye amethibitisha Loic Remy atakuwa nje kwa wiki tatu zijazo kwa maumivu ya nyonga, amesema mshambuliaji wake huyo nyota ana nafasi ya kwenda Old Trafford. Diego Costa ana nafasi ya kuivaa Manchester United Uwanja wa Old Trafford, amesema kocha wa Chelsea, Jose Mourinho Alipoulizwa leo iwapo Costa atacheza, Mourinho akasema: "Kuna nafasi, ana nafasi ndogo. Diego ana nafasi kidogo, sawa na Ramires na (John Obi) Mikel. Lakini Remy yuko nje na hatacheza. Hana nafasi,". "Kila kitu kilichotokea (kwa Costa). Alikuwa majeruhi kama kawaida- hiyo ilikuwa ni nyama. Ilibidi aende hospitali kwa matibabu, tatizo ambalo tusingeweza kulitatua bila kuwa hospitali kwa usiku mmoja- hiyo ilikuwa kabla ya kucheza na Maribor,"amesema.

Thursday, October 23, 2014

DIAMOND PLATNUMZ NDO HANZO CHA MSANII HUYU WA NYIMBO ZA INJILI KUITISHA MAANDAMANO, SOMA KISA HAPA…

Bongo kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasanii kua malipo wanayopata pale wanapopata show ni madogo zaidi ukilinganishwa na wanayopewa wasanii wa nje wanapokuja kupiga show Tanzania. Katika pitapita zangu katika website za Kenya nmekutana na picha za maandamano yaliyoandaliwa na msanii wa Kenya ajulikanaye kama Ringtone.
Lengo kubwa la yeye kuanzisha maandamano hayo ni kulalamikia pesa ndogo aliyolipwa katika tuzo za MCSK ambapo alilipwa sh 50,000 ya Kenya ambayo ni sawa na sh 950,000 za kibongo huku Diamond msanii kutoka hapa kwetu akilipwa 1,500,000 za Kenya ambazo ni zaidi ya 28,000,000 za kibongo. Msanii huyo wa nyimbo za injili alilalamikia mfumo mzima wa malipo katika tuzo hizo akisema ni wa Kinyonyaji na unawarudisha nyuma wasanii wa Kenya. Unaweza tazama picha za maandamano hayo hapa chini.

MSANII MIKE TEE AVAMIWA NA AJAMBAZI, ATANGAZA DONGE ONO KWA ATAEIONA GARI HII.

Msanii Mike Tee anaumaliza mwaka vibaya baada ya leo kuvamiwa na watu wenye silaha na kumpora mali zake zenye thamani kibao, Mike Tee ameandika kwenye account yake ya Facebook maneno yafuatayo: “Leo hii asubuhi majira ya saa 05:30 nikiwa naelekea ofisini , nimevamiwa na watu watano wenye mapanga wakiwa na gari aina RAV4 ya silver no. T280AZQ wamechukua laptop yangu MacPro, External HDD 4, Headphones za Sony na Modem . Nnachoshukuru nimepona ila nnachoomba atakayeiona gari hii popote atutaarifu kwa number +255754310202 / na ntampatia cash 300,000 then ntadeal nao mwenyewe”