Thursday, October 23, 2014
|
Bongo kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa
baadhi ya wasanii kua malipo wanayopata pale
wanapopata show ni madogo zaidi ukilinganishwa
na wanayopewa wasanii wa nje wanapokuja
kupiga show Tanzania. Katika pitapita zangu
katika website za Kenya nmekutana na picha za
maandamano yaliyoandaliwa na msanii wa Kenya
ajulikanaye kama Ringtone. |
|
Lengo kubwa la yeye kuanzisha maandamano
hayo ni kulalamikia pesa ndogo aliyolipwa katika
tuzo za MCSK ambapo alilipwa sh 50,000 ya
Kenya ambayo ni sawa na sh 950,000 za kibongo
huku Diamond msanii kutoka hapa kwetu akilipwa
1,500,000 za Kenya ambazo ni zaidi ya
28,000,000 za kibongo.
Msanii huyo wa nyimbo za injili alilalamikia
mfumo mzima wa malipo katika tuzo hizo
akisema ni wa Kinyonyaji na unawarudisha
nyuma wasanii wa Kenya. Unaweza tazama picha
za maandamano hayo hapa chini. |
0 comments:
Post a Comment