Thursday, October 23, 2014

DIAMOND PLATNUMZ NDO HANZO CHA MSANII HUYU WA NYIMBO ZA INJILI KUITISHA MAANDAMANO, SOMA KISA HAPA…

Bongo kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasanii kua malipo wanayopata pale wanapopata show ni madogo zaidi ukilinganishwa na wanayopewa wasanii wa nje wanapokuja kupiga show Tanzania. Katika pitapita zangu katika website za Kenya nmekutana na picha za maandamano yaliyoandaliwa na msanii wa Kenya ajulikanaye kama Ringtone.
Lengo kubwa la yeye kuanzisha maandamano hayo ni kulalamikia pesa ndogo aliyolipwa katika tuzo za MCSK ambapo alilipwa sh 50,000 ya Kenya ambayo ni sawa na sh 950,000 za kibongo huku Diamond msanii kutoka hapa kwetu akilipwa 1,500,000 za Kenya ambazo ni zaidi ya 28,000,000 za kibongo. Msanii huyo wa nyimbo za injili alilalamikia mfumo mzima wa malipo katika tuzo hizo akisema ni wa Kinyonyaji na unawarudisha nyuma wasanii wa Kenya. Unaweza tazama picha za maandamano hayo hapa chini.

0 comments:

Post a Comment