Tuesday, October 28, 2014
|
Mkali wa movie kutoka Hong Kong China,
Jackie Chan ameomba vyombo vya habari
‘vijichunge’ na namna vinavyoandika taarifa
kuhusiana na kitendo cha mtoto wake
kukamatwa na dawa za kulevya kwa kuwa
kufanya hivyo si kumuumiza yeye (Jackie
Chan) bali ni kumuumiza mama wa mtoto
huyo.
Jackie Chan amesema kupitia tukio hilo
amejifunza kuwa baba bora kitu ambacho
hakukijua siku za nyuma.
Mtoto wa staa huyo, Jaycee Chan alikamatwa
kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya aina
ya bangi zaidi ya gramu 100 ndani ya nyumba
yake, na baadaye kushitakiwa kwa kuuza dawa
hizo.
Jackie Chan ambaye amekuwa balozi wa
kupinga dawa za kulevya tangu mwaka 2009,
amesononeshwa na pia ameomba radhi kwa
kosa alilotenda mwanae ambapo hii imekuwa
mara yake ya kwanza kujibu swali
linalohusiana na kesi ya mtoto wake, akisema
kupitia hilo amejifunza kuwa baba bora. |
0 comments:
Post a Comment