Saturday, November 01, 2014

RONALDO AFUNGA REAL MADRID IKISHINDA 4-0 LA LIGA NA KUPANDA KILELENI

REAL Madird imeichapa Granada mabao 4-0
katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania,
maarufu La Liga jioni ya leo Uwanja wa
Nuevo Los Carmenes.
Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano
Ronaldo aliifungia Real Madrid bao la
kwanza dakika ya pili, kabla ya James
Rodriguez kufunga la pili kipindi cha kwanza,
Karim Benzema kufunga la tatu dakika ya 54
na James Rodriguez kukamilisha ushindi huo
dakika za mwishoni.
Ushindi huo, unaifanya Real ipae kileleni
mwa La Liga kwa kufikisha pointi 24 baada
ya kucheza mechi 10, lakini imecheza mechi
moja zaidi dhidi ya Barca, wanaochuana nao
kwenye mbio za ubingwa.

0 comments:

Post a Comment