Wednesday, October 29, 2014
|
Cristiano Ronaldo amekomba
zawadi tatu 'hat trick'
za tuzo ya wachezaji bora
Ligi ya Hispania maarufu
kama La Liga.
Huku mpinzani wake Lionel
Messi akiambulia patupu,
tuzo tatu alizobeba
Ronaldo ni pamoja na
Mchezaji Bora, Mfungaji
Bora na Mshambuliaji Bora
wa La Liga.
Ilikuwa furaha kubwa kwa
Ronaldo ambaye aliongozana
na mpenzi wake Iryna
Shayk, mwanamitindo kutoka
Urusi.
Pamoja na Ronaldo kubeba
tuzo hizo, timu yake ya
Real Madrid imetawala
zaidi kuliko klabu
nyingine ya Hispania.
Zawadi ya kiungo bora
imekwenda kwa Luka Modric
huku Sergio Ramos
akichukua tuzo ya beki
bora.
Kipa mpya wa Real Madrid,
Keylor Navas amechukua
tuzo ya mlinda mlango
bora. Kabla ya kutua
Madrid, Navas alikuwa
akikipiga Levante.
Barcelona pia imefanikiwa
kupata tuzo tatu, Andrés
Iniesta alitangazwa kuwa
kiungo bora mshambuliaji,
huku Ivan Rakitic na
Rafinha wakitwaa tuzo
mbili za Fair Play and
Breakthrough.
Kutokana na mafanikio
makubwa msimu uliopita,
Kocha wa Atlético, Diego
Simeone alibeba tuzo ya
Kocha Bora.
Mshambuliaji nyota wa
Sevilla, Carlos Bacca
akachukua tuzo mchezaji
Bora kutoka Amerika Kusini
na Yacine Brahimi wa
Granada akawa Mchezaji
Bora kutoka Afrika. |
0 comments:
Post a Comment