Saturday, October 25, 2014
|
KOCHA Jose Mourinho ameghairi kumuweka
benchi mshambuliaji Diego Costa katika
mchezo wa Ligi Kuu England dhidi
ya Manchester United Jumapili.
Mshambuliaji huyo wa kati wa Hispania,
amekosa mechi mbili zilizopita katokana na
maumivu ya nyama na wiki hii alipelekwa
hospitali kwa tiba ya tatizo hilo.
Lakini Mourinho, ambaye amethibitisha Loic
Remy atakuwa nje kwa wiki tatu zijazo kwa
maumivu ya nyonga, amesema mshambuliaji
wake huyo nyota ana nafasi ya kwenda Old
Trafford.
Diego Costa ana nafasi ya kuivaa
Manchester United Uwanja wa Old Trafford,
amesema kocha wa Chelsea, Jose Mourinho
Alipoulizwa leo iwapo Costa atacheza,
Mourinho akasema: "Kuna nafasi, ana nafasi
ndogo. Diego ana nafasi kidogo, sawa na
Ramires na (John Obi) Mikel. Lakini Remy
yuko nje na hatacheza. Hana nafasi,".
"Kila kitu kilichotokea (kwa Costa). Alikuwa
majeruhi kama kawaida- hiyo ilikuwa ni
nyama. Ilibidi aende hospitali kwa matibabu,
tatizo ambalo tusingeweza kulitatua bila
kuwa hospitali kwa usiku mmoja- hiyo
ilikuwa kabla ya kucheza na
Maribor,"amesema. |
Borgata Hotel Casino & Spa - Trip.com
ReplyDeleteFind the 안양 출장샵 best prices for rooms at Borgata Hotel Casino & 동두천 출장샵 Spa in Atlantic City 용인 출장마사지 on Trip.com! Book the hotel with real traveler 광명 출장안마 reviews, ratings and latest 광양 출장마사지 Rating: 4.1 · 11 reviews