Saturday, October 25, 2014

MOURINHO AELEZA KUHUSU DIEGO COSTA KUCHEZA AU KUTOCHEZA KWENYE MECHI DHIDI YA MAN UNITED JUMAPILI HII

KOCHA Jose Mourinho ameghairi kumuweka benchi mshambuliaji Diego Costa katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Manchester United Jumapili. Mshambuliaji huyo wa kati wa Hispania, amekosa mechi mbili zilizopita katokana na maumivu ya nyama na wiki hii alipelekwa hospitali kwa tiba ya tatizo hilo. Lakini Mourinho, ambaye amethibitisha Loic Remy atakuwa nje kwa wiki tatu zijazo kwa maumivu ya nyonga, amesema mshambuliaji wake huyo nyota ana nafasi ya kwenda Old Trafford. Diego Costa ana nafasi ya kuivaa Manchester United Uwanja wa Old Trafford, amesema kocha wa Chelsea, Jose Mourinho Alipoulizwa leo iwapo Costa atacheza, Mourinho akasema: "Kuna nafasi, ana nafasi ndogo. Diego ana nafasi kidogo, sawa na Ramires na (John Obi) Mikel. Lakini Remy yuko nje na hatacheza. Hana nafasi,". "Kila kitu kilichotokea (kwa Costa). Alikuwa majeruhi kama kawaida- hiyo ilikuwa ni nyama. Ilibidi aende hospitali kwa matibabu, tatizo ambalo tusingeweza kulitatua bila kuwa hospitali kwa usiku mmoja- hiyo ilikuwa kabla ya kucheza na Maribor,"amesema.

1 comment:

  1. Borgata Hotel Casino & Spa - Trip.com
    Find the 안양 출장샵 best prices for rooms at Borgata Hotel Casino & 동두천 출장샵 Spa in Atlantic City 용인 출장마사지 on Trip.com! Book the hotel with real traveler 광명 출장안마 reviews, ratings and latest  광양 출장마사지 Rating: 4.1 · ‎11 reviews

    ReplyDelete