Wednesday, October 29, 2014
|
KLABU ya Chelsea imetinga Robo Fainali ya
Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One
Cup baada ya kuichapa mabao 2-1
Shrewsbury usiku huu.
Chelsea ilipata bao la kwanza mapema tu
kipindi wakati mkongwe, Didier Drogba
alipomalizia pasi maridadi ya mwanasoka
wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah.
Lakini Shrewsbury ikapata bao la
kusawazisha kupitia kwa Andrew Mangan
aliyetokea benchi dakika ya 77, kabla ya
Jermaine Grandison kujifunga dakika nne
baadaye kuipa ushindi timu ya Jose
Mourinho. |
0 comments:
Post a Comment