Wednesday, October 29, 2014
|
KLABU ya Liverpool imeichapa Swansea
mabao 2-1 katika mchezo wa Raundi ya
Nne ya Kombe la Ligi England, maarufu
kama Capital One Cup usiku huu Uwanja wa
Anfield.
Jordan Henderson alipewa beji ya
Unahodha, kocha Brendan Rodgers akifanya
mabadiliko ya wachezaji tisa katika kikosi
chake cha kwanza.
Winga wa Swans, Marvin Emnes aliifungia
timu yake bao la kwanza dakika ya 65, kabla
ya Mario Balotelli aliyetokea benchi
kuchukua nafasi ya Rickie Lambert
kusawazisha zikiwa zimesalia dakika tano.
Federico Fernandez alitolewa kwa kadi
nyekundu dakika za mwisho kwa kumchezea
rafu Philippe Coutinho kabla ya Dejan Lovren
kuifungia Liverpool bao la ushindi dakika za
majeruhi na kuwapeleka Wekundu hao Robo
Fainali. |
0 comments:
Post a Comment