Saturday, October 25, 2014
|
Dar es Salaam.
Mwanamuziki Nassib Abdul, ‘Diamond Platnumz’
amesalimisha nguo zake za kijeshi kwenye Kituo
cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Diamond alisema kuwa juzi alipokea wito
uliomtaka afike kituoni hapo (Oysterbay) akiwa na
madansa wake pamoja na nguo hizo. Alisema
haikuwa rahisi kwake kutii amri ya vyombo vya
dola kwani alikuwa na woga kutokana na
kutokuwa na rekodi ya yoyote ya matukio ya
uhalifu. “Nisingeweza kukaidi amri ya dola, nilifika na yale
mavazi na nikahojiwa kwa saa kadhaa. Nikaeleza
kwamba yalikuwa yakifanana na ya jeshi na
hayakuwa sare rasmi za jeshi hilo, kikubwa
nilihitaji kumaliza tatizo,” alisema nyota huyo
aliyetajwa kuwania tuzo za MTV EMA
zinazotarajiwa kufanyika Novemba 9 mjini
Glasgow, Scotland.
Diamond alisema si kweli kwamba alichukuliwa
dhamana na Chifu Kiumbe, ila ukweli ni kwamba
alisindikizwa na mdau huyo wa sanaa nchini
kama kaka yake kutokana na woga aliokuwa nao,
lakini hakushikiliwa na kutakiwa dhamana yoyote. |
0 comments:
Post a Comment