Sunday, October 12, 2014

HUU NDIO MKAKATIA ALOUPANGA MENINAH KUMSHUSHUA DIAMOND NA WEMA

Stori: Andrew Carlos BAADA ya kuandamwa na skendo kuwa anatoka kimapenzi na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, mkali wa Bongo Fleva, Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’ amesema yuko mbioni kumtambulisha mchumba wake.
Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’. Akipiga stori na gazeti hili, Meninah ambaye ni zao kutoka shindano la kuibua vipaji vya kuimba, Bongo Star Search ‘BSS’ 2012 alisema; “Nimechoshwa kila siku kusikia Diamond, sasa ni bora nimtafute mwanaume yeyote tu kisha nimtambulishe ili ijulikane siko na Diamond,” alisema Meninah ambaye yupo mbioni kuachia ngoma mpya ya Kaniganda.
Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’ akipozi. Hivi karibuni kulikuwa na tetesi kuwa Meninah anatoka kimapenzi na Diamond, pia Diamond ameshafika kwao kujaribu kutoa mahari ili amuoe.

JOKATE KUOLEWA NA MSANII HUYU WA MAREKANI

Jokate New buzz is that Jokate Mwegelo ambaye ni star mkubwa Tanzania amepata mpenzi mpya baada ya kuwa mpweke kwa mudamrefu sasa baada ya kuacahana na Diamond.

Gossip mpya zinasema kuwa mpenzi mpya wa Jokate ni msanii wa Marekani wa muziki na filamu ingawa bado sio maarufu sana kwani bado anapigana ili kuweka jina lake fresh katika entertainment industry ya Marekani na dunia kwa ujumla.

Chanzo kimoja kilicho karibu na Jokate kimesema kuwa Jokate na jamaa huyo ambaye kipesa sio haba walikutana takribani miezi miwili iliyopita katika studio zaTV moja nchini South Africa ambayo imemwajiri Jokate kama mmoja wa watangazaji wake(Vj) na mahaba yao kuanzia hapo, inadaiwa zaidi kuwa jamaa kamkubali Jokate na wana mipango ya kuishi pamoja kama mke na mume.

Kikizungumza na Swahiliworld jana chanzo hicho ambacho ni rafiki wa Jokate kilisema..

MBEBES MKALI AJIUA KWASABABU YA MAPENZI

MADEE ALAZIMIKA KULIPA FAINI ILI KUMALIZA KESI YA UTEKAJI MTU ILIYOKUWA INAMKABILI

Kesi ya utekaji iliyokuwa ikimkabili Madee imemalizika kwa kulipa faini ya shilingi 50,000. Madee alidaiwa kumteka kijana mmoja huko Kigamboni baada ya kumuibia simu. Hakimu ametoa hukumu ya kifungo cha jela miezi sita au kulipa faini ya kiasi hicho cha fedha. Madee alilipa faini. Madee amezungumza kwa mara ya kwanza tangu apatwe na mkasa huo. “Yule dogo baada ya kuniibia simu tulimgonga kwa nyuma akaanguka tukamwokota na kumbeba kwenye Noah yetu tukaondoka naye. Kesho yake nilikuwa na safari ya kwenda Mwanza kwahiyo nikaachia masela wampeleke polisi na hapo mimi nilishampigia simu mama yake ili aongee na mwanae aseme simu yangu iko wapi. Simu yangu yenyewe ndio ilikuwa kila kitu. Kwahiyo nilivyoondoka nikiwa sina hata mawasiliano, nikaenda Mwanza nimefanya show, nimerudi Jumatatu asubuhi nikaulizia mtuhumiwa wangu nikaambiwa yupo Magomeni. Nikaenda Magomeni polisi nikaambiwa dogo kahamishiwa Kigamboni,” amesimulia Madee. “Nikaamua kwenda Kigamboni, kwenda Kigamboni nikaambiwa ‘bwana wewe ndo unashtakiwa ukitaka kumteka huyu dogo’ ndio nikawekwa ndani, nikalala siku moja, asubuhi nikadhaminiwa nikatoka kesi ikaenda mahakamani. Mahakamani kesi ikaahirishwa siku ya kwanza siku ya pili ikapita, hukumu nikaambiwa kati ya kwenda jela miezi sita au kulipa faini 50,000. Nikalipa faini na kesi ikaisha. Yaani mimi ndo nimekuwa mwenye kosa, mimi ndo niliyelipa faini.”

MANCHESTER UNITED HII AIBU SASA.

Kitengo cha uchapishaji cha klabu ya Manchester United kimeiingiza kwenye aibu kubwa klabu hiyo mara baada kuchapisha vibaya jina la mchezaji Angel Di Maria kwenye jezi zilizopelekwa dukani kwa madhumuni ya kibiashara. Katika makosa hayo jezi ya mchezaji huyo imekutwa imeandikwa ‘Da Maria’ baada ya Di Maria kama jina lake lilivyo wakati jezi ya mchezaji Radamel Falcao imekutwa ikiwa imeandikwa ‘Flacao’.

Saturday, October 11, 2014

TAARIFA YA KAMATI YA UTENDAJI YA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA ILIYOKUTANA OKTOBA 11, 2014- DAR ES SALAAM

KIKAO cha dharura cha Kamati ya Utendaji
ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) kimefanyika leo kujadili matukio ya
hivi karibuni, hasa mwenendo wa wadau wa
Bodi ya Ligi. Shirikisho linatoa tamko kwa
umma kama ifuatavyo: .

1.Kamati ya Utendaaji imesikitishwa na
taarifa za upotoshaji kuhusu kanuni mpya
za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), hivyo
inaomba radhi kwa wadau ambao
wameguswa na kusumbuliwa na matukio
hayo.

2.Kufuatia matukio hayo, Sekretarieti ya TFF
kwa niaba ya Kamati ya Utendaji, imefungua
mashtaka kwenye Kamati ya Nidhamu dhidi
ya Dk. Damas Ndumbaro ambaye ni mjumbe
wa Bodi ya Ligi na Mwenyekiti wa Kamati
ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba. Pia wadau
wote waliohusika na upotoshaji huo
wakiwemo wafanyakazi wa TFF na Bodi ya
Ligi watashughulikiwa kulingana na nafasi
zao.

3.Kutokana na madai ya klabu kuhusu
vipengele kadhaa vya Kanuni za Ligi Kuu
2014/15, Kamati ya Utendaji imepanga
kukutana na viongozi wa klabu za Ligi Kuu
siku ya Jumamosi, Oktoba 18 mwaka huu ili
kuwasikiliza na kushauriana kuhusu
changamoto za kikanuni na uendeshaji wa
mashindano kwa ujumla.

4.Kamati ya Utendaji itaendelea kuboresha
Kanuni za Uendeshaji Bodi ya Ligi
(Governing Regulations) ili kuweka uwiano
wa utendaji na kuepusha tofauti kati ya Bodi
ya Ligi, vilabu na TFF. Aidha Kamati ya
Utendaji itafanya kila linalowezekana
kuboresha ligi kwa kuijengea uwezo Bodi ya
Ligi kwa lengo la kuwa na ligi
zinazoendeshwa kisasa (Professional
Leagues).
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA
MIGUU TANZANIA (TFF).

KOCHA STARS ASEMA KIKOSI CHAKE KIPO TAYARI KUIVAA BENIN

Kocha wa Taifa Stars,
Mart Nooij amesema kikosi
kipo tayari kwa ajili ya
mechi dhidi ya Benin.
Lakini akasisitiza,
haitakuwa mechi laini kama
ambavyo wengi wanafikiri.
"Tumejiandaa vizuri,
tunataka kucheza mpira
mzuri na kushinda, hayo
ndiyo malengo.
"Lakini Benin si timu
laini, hivyo tayari
wachezaji wanajua
wanacheza na timu ngumu
lakini inafungika,"
alisema Nooij raia wa
Uholanzi.
Stars imekuwa kambini kwa
wiki moja sasa ikijiandaa
na mechi hiyo.
Kikosi hicho kitamkosa
Mbwana Samatta ambaye
aliumia katika mechi ya
Ligi ya Mabingwa Afrika
akiitumikia TP Mazembe ya
DR Congo ambayo ilitolewa
kwenye hatua ya nusu
fainali.
Nyota wa nje watakaokuwa
kwenye kikosi hicho ni
pamoja na Thomas Ulimwengu
(TP-DR Congo), Mwinyi
Kazimoto (Al Markhiya-
Qatar) na Juma Luizio
(Zesco-Zambia).

SHEPU YANGU NI KAMA ANDAZI LILILONONA NDIO MAANA NAPATA WANAUME

Mtangazaji wa kituo cha Redio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’.Aliweka bayana kwamba anaachika na kupata mwanaume mpya haraka kwa sababu ana shepu ya
kalimati (aina ya andazi linalonona).

MTANGAZAJI wa kituo cha Redio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’, juzikati aliamua kutoa siri yake ya moyoni na kuweka wazi juu ya tabia yake ya kuachika na kupata mume mpya mara kwa mara  SOMA ZAID> 

SAMATTA NA BOCCO WATAKOSEKANA KESHO STARS NA BENIN, NOOIJ ATATUMIA MABEKI WATATU…KWA MFUMO UPI?

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM WASHAMBULIAJI wawili, Mbwana Ally Samatta na John Raphael Bocco ambao Mholanzi Mart Nooij amekuwa akiwatumia katika mechi zilizopita kucheza pamoja na Thomas Emmanuel Ulimwengu watakosekana kesho kwa sababu wote ni majeruhi. Samatta amebaki Lubumbashi baada ya kuumia akiichezea klabu yake, Tout Puissant Mazembe katika Nusu Fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya ES Setif ya Algeria. Mazembe ilitolewa kwa mabao ya ugenini, baada ya sare ya jumla ya 4-4. Bocco wa Azam FC anaendelea kuuguza goti aliloumia Agosti kwenye Robo Fainali ya Kombe la Kagame, dhidi ya El Merreikh ya Sudan mjini Kigali, Rwanda. Azam ilitolewa kwa penalti. Maana yake, kama kocha huyo Mholanzi ataendelea kutumia mfumo wa 4-3-3 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa kesho dhidi ya Benin, atalazimika kuwa na wachezaji wa kuziba pengo la wawili hao. Ameonekana ni muumini wa wachezaji wenye maumbo makubwa- na katika kikosi alichoteua zaidi ya Ulimwengu, anabaki na washambuliaji wengine wawili, Mwegane Yeya wa Mbeya City na Juma Luizo wa ZESCO United ya Zambia. Ni hao ambao watachukua nafasi za Samatta na Bocco, au kocha Nooij atabadili mfumo? Tutajua kesho. Kwa kuwa tayari Nooij amesema katika mchezo huo atatumia mabeki watatu wa kati, ili kuwa na ukuta mgumu, mmoja wao akicheza kama kiungo mkabaji ili kuwapunguzia wenzake majukumu- maana yake kuna uwezekano akatumia mfumo wa 4-4-2 kesho. Kama atacheza na wachezaji saba katika ukuta, basi atahitaji japo wachezaji wawili katikati ili kutengeneza uwiano kati ya nyuma na mbele- jambo ambalo linaleta picha ya kutokuwa na washambuliaji watatu kesho. Kama baada ya ukuta wa watu saba atakuwa na viungo wengine wawili katikati- maana yake zitabaki nafasi mbili kwa ajili ya washambuliaji na viungo wa pembeni. Akiongeza kiungo mmoja atakuwa na nafasi tatu. Kuna shauku kubwa ya kutaka kujua kikosi cha Stars kitakuwaje kesho. Nooj amesema mpango wa kutumia mabeki watatu wa kati, unafuatia makosa yaliyofanywa na timu yake katika mechi ya mwisho dhidi ya Burundi ambayo ndani ya dakika 15 za kwanza walijikuta wanafungwa mabao mawili ya haraka haraka dakika ya kwanza na 12. Kwa ujumla, tangu ametua Stars Nooij ameiongoza Stars katika mechi nane na kati ya hizo, ameshinda mbili amefungwa tatu na kutoa sare tatu na katika mechi zote hizo nyavu za Stars zimetikiswa mara 12, huku yenyewe ikifunga mabao tisa. Bila shaka langoni ataendelea kusimama Deo Munishi ‘Dida’, beki ya kulia Shomary Kapombe, kushoto Oscar Joshua na katikati Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kevin Yondan. Nani atakuwa beki wa tatu wa kati? Hilo ndilo swali kwa sababu katika mechi zilizopita amekuwa akimtumia Erasto Nyoni katika kiungo mkabaji, lakini kwa kupona Jonas Mkude maana yake anaweza kufanya mabadiliko. Na yatakuwa mabadiliko ambayo yatamfanya Nyoni arudi benchi au ndiyo akawe beki wa tatu wa kati? Said Mourad amekuwa akiingia kwenye mipango ya Nooij anapoamua kuongeza idadi ya mabeki- maana yake naye kesho na anafasi ya kuanza katika 11. Salum Abubakar ‘Sure Boy’ amerudi katika fomu na viungo wengine Said Ndemla, Himid Mao na Amri Kiemba wote wapo vizuri, lakini Nooij amekuwa akimtumia Mwinyi Kazimoto kama kiungo mchezeshaji- kesho itakuwaje? Washambuliaji wa pembeni wote Mrisho Ngassa, Simon Msuva, Khamis Mcha ‘Vialli’ na Haroun Chanongo nao wapo vizuri maana yake katika mchezo huo wa kirafiki ulio kwenye kalenda ya FIFA wanaweza kucheza kwa zamu, lakini je akina nani wataanza? Katika jitihada za kuwa na kikosi cha uhakika, chenye wachezaji bora wa akiba, Nooij amewaita chipukizi beki wa kulia Miraj Adam, beki wa kushoto Edward Charles na beki wa kati Joram Mgeveke- nao bila shaka watapata nafasi kidogo kwenye mchezo wa kesho. Hivi sasa Nooij anajaribu kutengeneza timu ya kampeni za baadaye baada ya kukosa nafasi ya kwenda Morocco mwakani kwenye AFCON na mchezo wa kesho utakuwa hatua nzuri ya kuanzia.

King Majuto ajipanga kufanya filamu ya pamoja na Wema na Diamond

Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho nchini, King Majuto amesema hivi kariburi alimshawishi Wema Sepetu azungumze na mpenzi wake Diamond Platnumz ili wafanye kazi ya pamoja. Mzee Majuto ambaye ni mshindi wa Tuzo za Watu 2014 ya filamu inayopenda, ameiambia Mdadisiblog kuwa amemwachia kazi hiyo Wema ili azungumzee na mzee (Diamond). “Hivi karibuni nilikuwa na Wema, nimemwambia aongee na Diamond ili tufanye filamu ya pamoja,” amesema Majuto. “Mimi, Wema na Diamond, hata Diamond ninaweza kuzungumza naye sema nimeanza na Wema kwanza, akikubali mtasikia tu.” Kwa upande mwingine Majuto amesema ili acheze filamu anahitaji kulipwa shilingi milioni 3. “Umri unaenda sasa biashara za nisaidie nisaide hakuna, kama unanitaka ili tufanye kazi unatakiwa uandae milioni 3.”

MAUAJI YA KUTISHA NDANI YA KANISA LA PAG BUKOBA, TAZAMA PICHA ZA TUKIO HILO

Katika hali isiyo ya kawaida,watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo wamevamia Kanisa la PAG tawi la Kagemu kata ya Kitendaguro manispaa ya Bukoba na kumua muumini mmoja kwa kumcharanga mapanga hadi kufa na mwenzake kujeruhiwa ,hawakuiba chochote ikiwemo simu zao. Hata hivyo tukio hilo linahusishwa na imani za kidini kwamba waliohusika na tukio hilo ni wapinzani ya dini yao.
Mtoa habari aliyegoma kutaja jina amesema chanzo cha mgogoro huo na kifo cha muumini ambaye ni mwalimu katika shule ya sekondari KAGEMU ni baada ya marehemu kuoa mwanamke wa dini nyingine ( inaifadhiwa ) na kumbadilisha dini huyo mkewe na hapo waumini wa dini ya mkewe walianza vitimbwi kwa kanisa hilo na hadi mauaji hayo kumekuwa na vurugu za kila mara baina ya pande mbili.
Polisi bado wanachunguza na watatoa taarifa baadae ,mwili wa marehemu umeifadhiwa katika chumba cha maiti bukoba mjini ,majeruhi amelazwa hospital ya mkoa .

SUAREZ AREJEA RASMI UWANJANI HAPO JANA NA HATOA KALI NYINGINE KATIKATI YA MECHI BAADA YA .....

null
MSHAMBULIAJI Luis Suarez ameichezea tena kwa mara ya kwanza Uruguay baada ya miezi minne ya kutumikia adhabu ya FIFA kwa kumng'ata begani Giorgio Chiellini wa Italia- kufuatia kuiongoza Uruguay kupata sare ya ugenini 1-1 na Saudi Arabia. Mshambuliaji huyo mpya wa Barcelona mwenye umri wa miaka 27, alipiga shut zuri la mpira wa adhabu ambalo liligongwa mwamba kabla ya beki Hassan Muath Fallatah kujifunga dakika ya 47. Hata hivyo, bao la Suarez ambaye alipunguziwa adhabu na Mahakama ya Usuluhishi ya FIFA (CAS) na kuruhusiwa kucheza mechi zisizo za mashindano, bao lake halikudumu kufuatia Naif Hazazi aliyetokea benchi kuisawazishia Saudi Arabia dakika ya mwisho. Amerudi; Luis Suarez akipongezwa na wenzake jana baada ya kusababisha bao la kuongoza la Uruguay Baada ya mechi, mchezaji huyo aliyehamia Barcelona kutoka Liverpool msimu huu kwa dau la Pauni Milioni 75, alisema: "Furaha kuvaa jezi hii tena ambayo inanipa mimi raha mno. Huwei kupoteza mapenzi yako kwa jezi. Uruguay!' Suarez, ambaye katikati ya mchezo aliomba ruhusa kwenda chooni mara moja na akakubaliwa na refa, kwa ujumla alicheza vizuri kwenye mchezo huo kabla ya kumpisha mwenzake dakika ya 70.

YULE DEMU TRAFKI ALIYEPIGA PICHA AKIPIGWA MABUSU KICHAKANI HUYU HAPA SASA AKIWA HANA SARE..!

Wezee Nimekutana na Hiyo Picha Instagram, Yule Polisi wa Kike Traffic Watu wamechimba Mpaka Wamepata Picha zake
Akiwa Bila sare za Kazini....

Baadhi ya Comment ni Hizi Hapa :

-mwambie alete CV mi ntamwajiri

-Aje kwangu atalelewa kuliko alivyokuwa huko!Contact pls

-Kajazia Sana hata Ingekuwa Mimi Ningekula Mzigo, hiyo ni ajali kazini

“Nimechoshwa kila siku kusikia Diamond, sasa ni bora nimtafute..." MTOTO MZURI MENINA AFUNGUKA YA MOYONI!

Akipiga stori na gazeti hili, Meninah ambaye ni zao kutoka shindano la kuibua vipaji vya kuimba, Bongo Star Search ‘BSS’ 2012 alisema;


“Nimechoshwa kila siku kusikia Diamond, sasa ni bora nimtafute mwanaume yeyote tu kisha nimtambulishe ili ijulikane siko na Diamond,” alisema Meninah ambaye yupo mbioni kuachia ngoma mpya ya Kaniganda.

Hivi karibuni kulikuwa na tetesi kuwa Meninah anatoka kimapenzi na Diamond, pia Diamond ameshafika kwao kujaribu kutoa mahari ili amuoe.

BAADA YA TRAFIKI SASA NI ZAMU YA POLICE...ANGALIA PICHA ALIOPIGA ASKARI HUYU AKIWA AMELEWA CHAKARI

Jamani sidhani kama kuna haja hata ya kutia neno hapa, picha yenyewe inajieleza! Wadhani hali hii inaashiria nini katika suala zima la nidhamu jeshini?!
Shuka hapo chini utoe maoni yako tafadhali!

BATA BATANI: MAISHA YA INSTAGRAM NI ZAIDI YA MAIGIZO..WATU WANAJUA KULA RAHA ASIKWAMBIE MTU!

Instagram ni zaidi ya uionavyo, watu wanajua kula raha asikwambie Mtu jionee mwenyewe… maisha mazuri hadi unashawishika kutaka kujua zaidi wanafanya nini…ntajaribu kuwatafuta hawa watupe siri ya mafanikio yao. 1. Vera Sidika anapenda clubs yaani mdada yeye ni full ku party. What I like from her she has a talent ni mchoraji balaa anaonekana msomi pia alisema karudi shule big up @queenveebossette naomba tuongee zaidi kuhusu vipaji vyako naamini watu watabaki vinywa wazi.. 2. Starlisha huyu naye ni mrembo wa instagram yeye anapenda kula sehemu nzuri, kupiga picha akiendesha magari mazuri na selfie za kumwaga. Mungu ni mkubwa kapunguza mabifu, sikuhizi yeye ni mshauri na mhamasishaji wa masuala mbali mbali ya maendeleo, hii inampa heshima safi sana @chaggabarbie naomba nijue siri ya utulivu wako, inapendeza sana. 3. Huddah kama hayuko airport, hotelini basi swimming pool @huddahthebosschick unapenda kuogelea we mtoto, umekaa kibiashara tu mara photo shoot, lebel yako ya mavazi iko hewan na mengine atleast unaonekana unafanya kazi. Hizo bikini ukiziweka sokoni utauza sana. Hongera 4. Masogange, picha nyingi yuko kitandani, kama sio kitandani bafuni kama sio nje ya nyumba then anarudi kitandani anajipiga mapicha weee hadi analala. Hongera nawe @officialagnes Mungu kakupendelea sana. Kuna wengine humu nashindwa kuwaelezea kwakweli…sitaki kujua sana maisha binafsi ya mtu ila natamani kujifunza au tujifunze kupitia hao “mastaa” Hakuna asiyependa kupiga mapicha all the time kalala, anaogelea, kwenye mahoteli makubwa na maboti anaenjoy maisha kama mnaweza kupiga mapicha hayo jamani tuonesheni na kazi zenu nasi tutamani kufikia huko??

MWALIMU APIGANA NGUMI NA MWANAFUNZI WAKE DARASANI, WANAFUNZI WAREKODI VIDEO BADALA YA KUAMULIA

Mwalimu wa sayansi katika shule ya Santa Monica High School alimstukia mwanafunzi huyu akijaribu kuuzia wanafunzi wenzake bangi darasani. Alipomkabili kuhusu tendo hilo, mwanafunzi huyo alimsukuma mwalimu huyo na ghafla ngumi zikaanza kurushwa hewani. Mwanafunzi huyo, Blair Moore, alikamatwa na polisi na kufunguliwa mashitaka ya kuingiza madawa, na kisu shuleni.
Wanafunzi wengi walikuwa upande wa mwalimu huyo, ikiwemo kuanzisha

HII NDIYO ARSENAL ILIYOITWA 'ARSENAL KWELI'

Hii ilikuwa Arsenal kweli; Wachezaji wa zamani wa Arsenal, kutoka kulia Thierry Henry, Robert Pires na Patrick Vieira na Ashley Cole aliyeipa mgongo kamera walioiwezesha The Gunners kushinda taji la mwisho la Ligi Kuu ya England mwaka 2004, tena wakiweka rekodi ya kutofungwa. Arsene Wenger kwa miaka sasa anapambana kurudisha enzi za mafanikio haya Arsenal.

THIERRY HENRY KUREJEA ARSENAL JANUARI...AMA ATAKWENDA PSG AU MONACO, AKIMALIZA MKATABA NEW YORK DESEMBA ....! JIBU LIPO HAPA

DESEMBA GWIJI wa Arsenal, Thierry Henry anavitoa udenda vigogo vya Ufaransa, Paris Saint- Germain na Monaco kwa mujibu wa taarifa nchini humo kwamba klabu hizo zinamtaka kumng'oa mshambuliaji huyo New York. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 37, ambaye amekuwa akiichezea New York Red Bulls tangu mwaka 2010, atamaliza Mkataba wake na timu hiyo ya MLS mwishoni mwa mwaka na atakuwa tayari kurejea Ulaya Januari. Tetesi zimetawala kwamba Henry anajiandaa kustaafu, lakini Mshika Bunduki huyo wa zamani anaweza kurudi Arsenal kwa mara ya tatu au gazeti la Le10 Sport limesema Henry anaweza kujiunga na moja ya vigogo vya Ligue 1. Tetesi zinasema Henry anaweza kurejea tena Arsenal, ama akaenda kujiunga na PSG au Monaco Januari Mkuu wa Idara ya kabumbu wa New York, kocha wa zamani wa Liverpool, Gerard Houllier, amezungumzia tetesi kwamba Henry anaweza kucheza Ligi Kuu ya Ufaransa. "Ikiwa bado ana uwezo wa kucheza katika Ligue 1? Ndiyo, hakuna tatizo," Houllier ameliambia Le10 Sport. "Hadi sasa hakuna uamuzi uliochukuliwa, kwa namna moja au nyingine. Thierry bado hajaamua kuacha soka,"amesema Houllier.

Friday, October 10, 2014

BREAKING: Msanii wa bongofleva Baba Levo amepata ajali… maelezo yako hapa

Ni saa tisa kasoro mchana Msanii wa bongofleva Baba Levo anaipiga simu millardayo.com na kuongea kwa tabu kwenye usikivu ulio mdogo na kusema kwamba amepata ajali kwenye pori karibu na eneo linaitwa Uluwila akiwa anatokea Tabora kwenda Mpanda. Alikua kwenye Basi liitwalo AM ambapo ghafla wakiwa kwenye kona ilitokea Coaster ikiwa na abiria ambayo dereva wake alikua akikwepa barabara mbovu hivyo ikabidi ahamie kwenye upande wa pili wa barabara ambako ndiko lilikua linapita basi la kina Baba Levo ambalo hakuliona sababu ni kwenye kona. Dereva wa basi la kina Baba Levo ilibidi ahame upande wake ili ahamie kwenye upande wa magari yanayopanda ambao ndio upande sahihi wa ile Coaster kupita ambapo juhudi zake hazikufanikiwa kwani wote walikua kwenye spidi na yule dereva wa Coaster alihama kwenye ule upande baada ya kuona atagongana uso kwa uso na basi la kina Baba Levo ila bahati mbaya wakawa wote wamejikuta upande mmoja na wakagongana uso kwa uso. Mwenye makosa anatajwa kuwa ni mwenye Coaster ambapo pamoja na Baba Levo kuumia usoni na mwilini kwa kuchanwachanwa na vioo vya mbele vilivyopasuka kwenye basi, ameweza kuona kuna baadhi ya watu wamefariki ambapo kati yao ni waliopasuka vichwa na shingo. Dereva wa basi la kina Baba Levo hajaumia sana wala basi halijaumia sana, Coaster ndio imefumuka upande wa juu wote na kuharibika sehemu nyingine pia huku kilichosababisha Baba Levo kuumia ni kwamba alikua amekaa pale juu ya Injini ya Basi kwenye kigodoro kutokana na basi hilo kujaa. Baba levo anajisikia vibaya kiasi na kwa sasa yuko na wenzake kama 20 pamoja na Askari mwenye silaha waliekua pamoja kwenye Basi…. wanatembea kutafuta kijiji chenye network ili kuomba msaada manake baadhi ya abiria wamebanwa kwenye hiyo Coaster na hawajatolewa.

CRD MILLARDAYO