Sunday, September 28, 2014

EPL-Matokeo ya mechi zilizochezwa siku ya jumamosi.

Liverpool 1 - 1 Everton

Chelsea 3 - 0 Aston Villa

Crystal Palace2 - 0Leicester

Hull 2 - 4 Man City

Man Utd 2 - 1 West Ham

Southampton 2 - 1QPR

Sunderland 0 - 0 Swansea

Arsenal 1 - 1 Tottenham

DIEGO COSTA NI HABARI NYINGINE...THE BLUES KILELENI ENGLAND

Mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa
akishangilia jana baada ya kufunga katika
ushindi wa 3-0 wa timu yake dhidi ya
Aston Villa Uwanja wa Stamford Bridge,
London. Mabao mengine yalifungwa na
Oscar na Willian na sasa The Blues wapo
kileleni mwa Ligi Kuu England. Chelsea
ina pointi 16, ikifuatiwa na Southampton
pointi 13, Manchester City pointi 11,
Arsenal pointi 10 sawa na Swansea City
na Aston Vila baada ya kila timu kucheza
mechi sita.

Saturday, September 27, 2014

EXCLUSIVE: MAAJABU YA TFF, SASA INATAKA SIMBA&YANGA ZIKATWE FEDHA ZA VODACOM, AZAM TV IPEWE YENYEWE

Ukishangaa ya usiyemjua, utayaona ya TFF. Sasa imeibuka na jipya na kutaka Yanga, Simba na klabu nyingine 12 za Ligi Kuu Bara, zikatwe 5% ya fedha za udhamini, ziingie TFF. Uongozi wa TFF umeandika barua kwenye bodi ya ligi ukitaka ulipwe 5% ya fedha za udhamini kutoka Vodacom na Azam TV ipewe yenyewe. TFF imetaka fedha hizo ili izitumie kwa ajili ya maendeleo ya soka au timu ya taifa. Lakini hali imezishitua baadhi ya klabu ambazo zimeanza kuhoji chinichini kuhusiana na suala hilo. Suala hilo la kushangaza kama litapita litakuwa ni la aina yake kwa klabu kutoa fedha zao za udhamini na kulipa shirikisho. Suala hilo ambalo limeonekana litakuwa la kwanza kufanyika katika ulimwengu wa soka, bado haijajulikana kama limepitishwa. Barua hiyo ya Septemba 19 kutoka TFF ikiwa imesainiwa na Katibu Mkuu, Mwesigwa Celestine, imeitaka bodi ya ligi kupeleka fedha hizo za klabu 14 za ligi kuu kwenye akaunti ya shirikisho hilo. TFF imesema fedha hizo zitaenda kwenye akaunt ya Maendeleo ya Michezo Tanzania ambayo hushughulikia timu ya taifa. (Kimantiki Vodacom na Azam TV hazidhamini timu ya taifa, inadhaminiwa na Kilimanjaro Beer.)

BAADA YA MECHI YA SIMBA NA YANGA KUSOGEZWA MBELE HII NDO TAREHE MPYA

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM MECHI ya watani wa jadi, Simba SC na Yanga SC mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara itapigwa Oktoba 18, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam badala ya Oktoba 12. Mechi zote za Oktoba 11 na 12 zimesogezwa mbele kwa wiki moja kupisha mchezo wa kimataifa, kati ya Tanzania na Benin. Taifa Stars itashuka uwanjani Oktoba 12 mwaka huu kuikabili Benin katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Programu ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kwa ajili ya mechi hiyo itatangazwa baadaye na Kocha Mkuu Mart Nooij. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linaendelea na taratibu nyingine kwa ajili ya mechi hiyo ikiwemo usafiri wa Benin kuja nchini, ambapo timu hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Oktoba 10 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 28. Pambano la Stars na Benin litatanguliwa na mechi ya kudumisha upendo kati ya viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu. Na kwa sababu, TFF imesogeza mbele mechi zilizokuwa zichezwe wikiendi ya Oktoba 11 na 12 na sasa zitachezwa Oktoba 18 na 19. Oktoba 18, Polisi Morogoro itamenyana na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Ndanda na Ruvu Shooting Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, Kagera Sugar na Stand United Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, Coastal Union na Mgambo JKT Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Mbeya City na Azam FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Yanga na Simba Taifa. Mzunguko huo utahitimishwa na mchezo kati ya Prisons na JKT Ruvu Uwanja wa Sokoine, Mbeya Oktoba 19. Zaidi ya hapo, Ratiba ya Ligi Kuu inabaki kama ambayo ilitolewa awali na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

WENGER AWAANZISHIA TENA MAN CITY NA USAJILI WAO WA KIMAGUMASHI KWA FRANK LAMPARD

MPANGO wowote wa kuongeza muda wa Frank Lampard kuendelea kucheza kwa mkopo Manchester City unaweza kuibua maswali zaidi ya kimaadili juu ya uhamisho wake, kwa mujibu wa kocha Arsenal, Arsene Wenger. Lampard alisaini timu ya Ligi Kuu ya Marekani (MLS), New York City baada ya kutemwa Chelsea, kabla ya kurejea ghafla Ligi Kuu ya England kujiunga na mabingwa, ambao pamoja na kuinunua timu ya baseball ya nchini humo, wakanunua na hisa timu hiyo ya MLS. Kiwango kizuri cha mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 36, aliyefunga mabao mawili katika ushindi wa 7-0 Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup dhidi ya Sheffield Jumatano, kimeibua tetesi kwamba City itaangalia uwezekano wa kumbakiza ifikapo Januari. Frank Lampard alijiunga na Man City kwa mkopo wa muda mfupi baada ya kuondoka Chelsea msimu huu Msimu wa MLS 2015 unatarajiwa kuanza tena Machi, mwakani na Lampard amesema hajafanya majadiliano yoyote na City juu ya mustakabali wake mwishoni mwa mwaka. Wenger, ambaye alimrudisha kwa mkopo Nahodha wake wa zamani The Gunners, Thierry Henry kutoka New York Red Bulls Januari 2012, anaamini namna yoyote ya kuongeza mkataba wa mkopo wa Lampard kwa sasa haitakuwa nzuri, hata ikiwa ni ndani ya utaratibu wa Ligi Kuu. "Wakati wote una maamuzi ya aina mbili, moja ya kimaadili na pili ni ya kisheria na ni juu ya unavyochukulia,"amesema Wenger. "Nafikiri, hii ni sheria? lazima uheshimu hilo na kisha mchezaji lazima atazame uamuzi wake. Naheshimu ukweli kwamba anataka kucheza katika kiwango cha juu na labda hakuwa na nafasi zaidi Chelsea. Sijui haswa kilicho nyuma ya hili,". "Ulikuwa ni mpango wake kwenda New York na kwenda Man City? Sina uhakika. Nafikiri kabisa alitaka kwenda nje na kutua New York, na (kisha) kupewa ofa ya kurudi Ligi Kuu England na kuichukua. Anaweza kufafanua vizuri yeye mwenyewe kuliko ninavyofanya, sijui nini kipo nyuma ya hili,"amesema Wenger.

Lulu Tisha Sana. Sasa Atembea na Bilionea Lililompangishia Jumba Laa Kifahari

Madai mazito ya kushtua mtaani yanasema kwamba staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mambo yake kwa sasa yapo juu ya mstari baada ya bilionea kutoka jijini Arusha (jina tunalihifadhi kwa sasa) kudaiwa kujitosa kumlea akianza kwakumpangishia jumba kubwa la kifahari.Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, akiwa na begi la fedha.TWENDENI USHUANIHabari hizo za mitaani zilidai kwambabilionea huyo amempangishia Lulu mjengo huo wa maana uliopo ushuani maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.Kimuonekano, nyumba hiyo iliyoshuhudiwa na wanahabari wetu mwanzoni mwa wiki hii haina tofauti na ile mijengo iliyozoeleka ya mastaawakubwa wa Marekani kwa maana yakujitosheleza kwa kila kitu ndani yake.Kwanza ni nyumba yenye fensi kubwa na kuingia getini lazima ujieleze ‘vizuri’ na ukiingia huufikii mlango wa nyumba kwani kuna ‘kamwendo’.Nje ya nyumba hiyo kuna ‘parking’ yamagari madogo zaidi ya kumi huku chini kukiwa na tarazo na pembeni kuna bustani nzuri iliyopandwa mauaya kuvutia.“Amehamia hivi karibuni, anaonekana muda wa kutoka na kuingia tu.
Nyumba anayoishi staa huyo.“Lulu ni binti mrembo mwenye mvutowake, ukizingatia ana nyota pia ya kupendwa, kwa hiyo siyo mtu wa kukaa uswazi,” alidai mtoa habari wetu na kuongeza:“Bidada kaula maana nasikia jamaa ameahidi kumpa matunzo ya nguvu.“Alianza kwa kumnunulia lile gari la kifahari la Toyota Rav4 New Model analotembelea Lulu, sasa naona kamuweka pazuri na kweli nyumba inaendana na hadhi yake.ADAIWA KUMPA JEURI YA KUWAFUNIKA KAJALA, WEMA“Nasikia jamaa amempa jeuri ya kuwafunika kabisa Kajala (Masanja) na Wema (Sepetu) ambao inasemekana wana mkwanja wa kumwagamwaga ovyo.”LULU LAIVU!Kupitia Kipindi cha Nirvana kinachorushwa na EATV, Lulu alionekana ndani ya mjengo huo uliojaa mazagazaga ya thamani.Mjengo huo una makabati makubwa ya nguo na viatu kiasi kwamba mtu unaweza ukahisi umeingia kwenye duka la nguo (boutique) na viatu kibao.Akizungumza kwa kujiamini Lulu alisema kuwa anapenda vitu vizuri hasa linapokuja suala la kupiga pamba ndiyo maana amejaza pamba kali kwenye makabati.“Kimsingi sipendi shida, napenda kuvaa vizuri, kula vizuri, kulala pazuri na mambo yote mazurimazuri,” alisema Lulu.
BILIONEA GANI?Ili kupata undani wa mwanaume huyo, gazeti hili lilichimba ambapo kwa mujibu watu wa karibu na Lulu, jamaa huyo ni mfanyabishara mkubwa wa madini jijini Arusha.“Kama mtakumbuka, huyo jamaa aliwahi kuwagombanisha Lulu na Husna (Maulid) kwani mwanzoni alikuwa mwanaume wa Husna.“Hivi unajua kabla ya ishu hiyo, Lulu na Husna walikuwa mashosti lakini baadaye wakawa kama paka na panya kisa tu ni huyo bilionea,” kilidaichanzo hicho.LULU ASAKWABaada ya kunyetishiwa habari hiyo yamtaani, gazeti hili lilimsaka Lulu hadi nyumbani kwake na lilipomkosa lilimtafuta kwa njia ya simu na alipopatikana alifunguka:“Kiukweli kabisa nyumba ninayoishi sasa mimi na familia yangu siyo kwamba nimepangishiwa wala kununuliwa na sijui bilionea au kigogo yeyote, hayo ni maneno ya watu tu. Unajua watu wanaongea sana, wanadhani mimi siwezi kujimudu,” alisema Lulu kwa kujiamini.

Credit gpl

Exclusive: Diamond azungumziatetesi za kupanga kumuoa Meninah

Hatimaye Diamond Platnumz amefunguka kuhusu tetesi zinazoendelea kuwa ameachana na Wema Sepetu na kwamba ana mpango wa kufunga ndoa na Meninah Atick.Diamond ameiambia Bongo5 kuwa tetesi hizo zimekuwa zikimhuzunishakwa kiasi kikubwa.“Unajua hizi habari kiukweli zimekuwa zikinihuzunisha sana,” amesema msanii huyo. “Unajua mie ni mtu mmoja ambaye sipendi kuzunguzia mambo ya rumors, siju magazeti huwa sipendi kuzungumziakabisa, kwa kuwa najua kabisa siwezikubishana na media kwakuwa media ni kubwa, maana najua utaongea na huyu na yule siku ya siku utagombana na watu. Ndio maana huwa nakaa kimya,” ameongeza Diamond.
“Kusema ukweli hili suala limekuwa likiniumiza ‘eti sijui kuna vikao vya harusi mie nataka kumuoa Meninah’ Kusema ukweli sina mahusiano na Meninah. Kila mtu anajua mie nina mahisiano Wema. Wema ndo mpenziwangu, ila wakati mwingine nakuwa naelewa ile inakuwa ni trick ya kibiashara. Mtu anajua hata nikimuandika vipi ‘Diamond sijui kafanya nini watu hawawezi kumchukia! Kwahiyo wanaamua kunitengenezea chuki na maadui kwa watu kuwa nipo na mwanamke wangu halafu namsaliti.”
“Unajua kitendo hicho hatamaye kinaniudhi naona mtu yupo na mpenzi wake halafu anamsaliti. Najua hicho ni kitendo ambacho kila mtu hakimpendezi. Kwahiyo wanaamua kunitengenezea chuki na maadui kupitia njia hiyo. Labda wana wasanii wao, sasa wanaona tukiingiakwa njia hii tutaweza kuamharibia Diamond. Ndioa siku zote nimekuwa kimya tu ila sina mahusiano na Meninah. Mie nikiwa na mtu huwa sifichi naweka wazi kabisa. Hata kama leo nimeachana na Wema nasema tu, why nifiche? Mie katika mambo yangu huwa simuogopi mtu kama ningekuwa nataka kuoa basi ninge weka wazi why nifiche?”

Umeona Jumba la kifahari Diamond alilomjengea mama yake??? CHeki hapa

Leo kupitia akaunti yake ya Instagram Diamond ametupia picha ya ile nyumba aliyosema anamjengeamama yake. Katika picha hiyo aliambatanisha na maelezo haya"Had to visit mama Chibu's Village today.."Nyumba hiyo inaonekana ya kifahari hasa ukiangalia muundo na mabati yaliyotumika kujenga nyumbahuyo.

Credit bongoclantz

Friday, September 26, 2014

SIMBA NA YANGA YAAHIRISHWA, TAREHE MPYA KUTAJWA KESHO…WAPISHA MTANANGE WA STARS NA BENIN TAIFA OKTOBA 12

Na Dina Ismail, DAR ES SALAAM MECHI ya watani wa jadi, Simba SC na Yanga SC mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyokuwa ichezwe Oktoba 12, mwaka huu imefutwa na sasa tarehe mpya itatajwa kesho. Taarifa ya TFF leo imesema kwamba, hiyo iantokana na mchezo wa kirafiki wa kimataifa baina ya Taifa Stars na Benin ambao kwa ujumla utabadilisha ratiba ya Ligi Kuu na marekebisho hayo yatatangazwa kesho (Septemba 26 mwaka huu). Taifa Stars inashuka uwanjani Oktoba 12 mwaka huu kuikabili Benin katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Programu ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kwa ajili ya mechi hiyo itatangazwa baadaye na Kocha Mkuu Mart Nooij. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linaendelea na taratibu nyingine kwa ajili ya mechi hiyo ikiwemo usafiri wa Benin kuja nchini, ambapo timu hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Oktoba 10 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 28. Pambano la Stars na Benin litatanguliwa na mechi ya kudumisha upendo kati ya viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu. Wakati huo huo: Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi anatarajia kufunga mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa vyama vya mpira wa miguu wa wanawake vya mikoa ya Tanzania Bara. Hafla ya kufunga mafunzo hayo itafanyika kesho (Septemba 26 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Mafunzo hayo ya siku tano yalishirikisha viongozi 34 wakiwemo baadhi ya waandishi wa habari na Meneja wa Twiga Stars, na yaliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau.

DIAMOND AZIDI KUPAA, HILI NDIO SHAVU JIPYA ALILOPATA

Ingawa hajaweka wazi namna dili hii itakavyokuwa lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram,Diamond Platnumz amepost picha ambayo imebeba maandishi yasemayo ‘Ningependa kukutaarifu shabiki wangu pendwa kuwa kijana wako sasa ni balozi wa application mpya iitwayo Mziiki’. Hii ni application ambayo itatumiwa na watu wenye simu za androad kusikiliza muziki huu ndiyo muonekano wake utakapokuwa ume instal kwenye simu yako.
Maandishi ya Diamond pamoja na alichokipost ni hICHO

BARCA KWAWAKA MOTO, MESSI NA WENZAKE KUPIGWA FAINI

Hospitali imesemaje kuhusu mchezaji wa Uganda aliefariki baada ya goli la Lampard?

Marehemu ni huyu alievaa jezi ya njano
Kabla ya kifo chake Musana alifanya mazoezi na timu yake Jumapili asubuhi na kula chakula cha mchanana mmoja wa marafiki aitwae Gerald Bagoole na kisha wakati wa mpira alikwenda kutazama jirani na anapoishi.Habari za kuhuzunisha za mashabiki wa soka Uganda zimekua na mfululizo wake kwenye hii miaka miwili huku wengine wakijiua baada ya kushindwa mechi na mmoja akiwana majonzi ya nyumba yake baada yakuiweka rehani akishadadia kutabiri ushindi wa timu yake.

Ni taarifa ambayo ilitolewa na vyombo mbalimbali vya habari kwamba mchezaji wa club ya Simba ya Uganda Fahad Musana amefariki kutokana na mshtuko wa goli alilolifunga Frank Lampard wa Manchester City wakati wakicheza naChelsea juzi.

Pamoja na hayo, taarifa kutoka hospitali kuu Uganda ya Mulago zinasema Fahad alifariki kutokana na ugonjwa wapnemoniana sio mshtuko uliotangazwa awali ambapoFahad aliezikwa September 24 2014 baada ya kufia kwenye hospitali ya Bombo Barracks alikua shabiki mkubwa wa Chelsea.

Rais Kikwete akikasirika au mtu akimuudhi nyumbani huwa inakuwa hivi….

Labda inawezekana hii ikawa mara yetu ya kwanza kusikia upande wa pili wa President wetu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete ambae tumezoea tu kumuona akihutubia, akijumuika na watu mbalimbali kwenye matukio ya furaha na huzuni lakini kuna menginehatuyajui kuhusu yeye.Mtoto wake Ridhiwani Kikwete ambae ni mbunge wa Chalinze ameongea kwenyeExclusivenamillardayo.comna kueleza ni jinsi gani inavyokua pale ambapo baba yake anakasirika au anapokasirishwa akiwa nyumbani.
>>> ‘Jambo akiwa halitaki mara nyingi hupenda kusema achana na hilo lakini kama ni mtu kafanya jamboflani sio zuri utamsikia mzee tu anasema huyu mtu bwana achana nae….. maarifa yake madogo, naweza kutoa ushuhuda mbele za watu mzeewangu mimi sio mtu ambae ameishi kwenye mazingira yanayotoa fursa yamatumizi ya lugha ngumungumu kama matusi‘‘Yani mtu akimuudhi… huwezi kusikia amefikia hatua ya kutamka labda huyu mshenziiii…. sina kumbukumbu ya mimi kumsikia akitamka neno kama hilo, mara nyingi ukikosea anasema huyu maarifa yake madogo kwelikweli‘ – Ridhiwani

Credit millardayo

Wema Sepetu Afunguka Sana: Awaponda Watumiaji Wa Tecno Na Huawe

Katika hali iliyoshangaza wengi,beautiful onyinye mwenye endless fame mnyange Wema Sepetu amesema watu wengi wanaomsema kwenye mtandao they don’t have life na wengi wao wanatumia Tecno na Huawei kulog inkwenye mitandao ya kijamii na kuanza kumponda, akichezesha taya na Ephraim Kibonde katika kipindi cha jahazi amesema watu hao hawampi shida hata kidogo kwani wamepigika na yupo juu zaidi yao.My Take:Hivi Sister wema hizo simu ulizozidharau unazijua vizuri kweli? Hivi unaweza ku-compare features za Huawei Ascend P7/Tecno H7 na Samsung Gallaxy S4?

Thursday, September 25, 2014

DOGO AVAMIA UWANJANI, APATA ZAKE SELFIE NA LAMPARD, POLISI WAMZOA

Shabiki mmoja wa Manchester City ameshindwa kujizuia baada ya kuvamia uwanjani wakati wa mechi ya Capital One kati ya timu hiyo dhidi ya Sheffield Wednesday. Dogo huyo alishindwa kujizuia kuonyesha mapenzi yake kwa mkongwe Frank Lampard na kwenda moja kwa moja kupata naye selfie (kujipiga picha kwa kutumia simu). Hata hivyo, baadaye Polisi walimdaka dogo huyo na kuondoka naye uwanjani hapo, hata hivyo alionekana kutojali kiivyo.

LA LIGA: MATOKEO YA BARCELONA vs MALAGA HAYA HAPA

Wakati Real Madrid wameibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Elche, Barcelona mambo yamekuwa si safi kiivyo baada ya kulazimishwa sare ya suluhu dhidi ya Malaga. Wakiwa ugenini, Barcelona walifanya kila juhudi huku mshambuliaji wao nyota Lionel Messi akihaha kila idara ili kupata bao angalau moja, lakini mambo yalishindikana. Wakati fulani, Malaga walikuwa wakali kama nyuki katika mechi hiyo ya La Liga lakini kipa wa Barcelona akawa imara kuokoa michomo ya hatari.

BAAADA YA KIONGERA KUHUMIA HILI NI PIGO LINGINE KUBWA WALILOPATA TIMU YA SIMBA

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM KIPA namba moja wa Simba SC, Ivo Philip Mapunda amevunjika kidole mazoezini Zanzibar leo asubuhi na anatakiwa kuwa nje kwa wiki nane- maana yake hataweza kusimama langoni timu hiyo ikimenyana na watani, Yanga SC Oktoba 12. Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe ameiambia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba, Ivo aliumia wakati anachupia mpira katika mazoezi ya asubuhi na kwa bahati mbaya ukamgonga kwenye kidole kidogo cha mwisho mkono wa kulia.

SIMBA SC ITAMTIBU KIONGERA KWA GHARAMA ZOZOTE AWE FITI AFANYE KAZI, YAJALI KIPAJI CHAKE…HANS POPPE ASEMA NI MKALI KWELI WA MABAO

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM SIMBA SC imekiri mshambuliaji wake, Paul Raphael Kiongera ana matatizo ya goti, lakini mpango wao si kumtema, bali kumtibu vizuri apone kabisa na kucheza tena. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema kwamba mchezaji huyo amefanyiwa vipimo jana na anahitaji tiba pamoja na mapumziko ya wiki sita, lakini baada ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara atapatiwa tiba zaidi. “Tumelijua hilo tatizo, na sisi hatutaki kuwaumiza wachezaji, sisi tutamtibu kwa gharama zozote, kwa sababu tunathamini kipaji chake. Atatusaidia hata msimu ujao,”.
hatuna tatizo la mshambuliaji, kama utakumbuka hadi dirisha la usajili linakaribia kufungwa tulikuwa hatuna Okwi (Emmanuel), ni mchezaji aliyekuja kwetu kwa bahati tu, sasa huyo ataziba pengo la Kiongera wakati huu,” amesema Poppe. Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) amesema kwamba tatizo kubwa la wachezaji wengi wanapoumia wakishauriwa kupumzika huwa hawataki kwa sababu wanapata riziki yao kwa kucheza. “Lakini sisi tumejifunza sana matatizo ya wachezaji, mfano Owino (Joseph). Aliumia akaenda kutibiwa India akaambiwa apumzike miezi sita, yeye akaenda kusaini Azam FC akacheza akaumia tena. Ia aliporudi tena India na kutibiwa, akaambiwa apumzike miezi sita, akapumzika. Akapona na sasa yuko fiti kabisa,”ameongeza Poppe. Amesema watawekeza kwa kumtibu mchezaji huyo kwa matumaini ya kumtumia baadaye kwa manufaa zaidi. “Huyu mchezaji ni mfungaji hodari, sisi tunajua uwezo wake, sasa tunachokifanya kwa sasa, faida yake itaonekana baadaye,”amesema. Kiongera aliumia katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Jumapili Uwanja wa Taifa, Simba SC ikilazimishwa sare ya 2-2 na Coastal Union, licha ya kuongoza kwa 2-0 hadi mapumziko. Kiongera alitokea benchi dakika ya 67, lakini dakika mbili kabla ya filimbi ya mwisho akampisha Amri Kiemba baada ya kuumia, kufuatia kugongana na kipa wa Coastal Union, Shaaban Kado.

CPL: HIKI NDO KIPIGO CHA MBWA MWIZI WALICHOKIFANYA MAN CTY DHIDI YA SHELFFIED

MANCHESTER City imesonga mbele katika Kombe la Ligi England, maarufu kama Capital One Cup kufuatia kuichapa mabao 7-0 Sheffield Wednesday usiku huu Uwanja wa Etihad. Dakika 45 za kwanza zilimalizika ubao wa matokeo ukisomeka 0-0, lakini dakika ya pili tu ya kipindi cha pili, Frank Lampard akafungua karamu ya mabao. Lamprad alifunga mawili, dakika ya 47 na 90, sawa na Edin Dzeko aliyefunga dakika ya 53 na 77. Mabao mengine ya mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England yalifungwa na Yaya Toure dakika ya 60 na kinda Angel Pozo dakika ya 88. Kikosi cha Manchester City kilikuwa: Caballero, Sagna, Demichelis, Mangala, Kolarov, Fernandinho/Boyata dk69, Navas, Toure/Pozo dk63, Lampard na Milner/Sinclair dk72, Dzeko. Sheffield Wednesday: Kirkland, Buxton, Lees, Zayatte, Mattock, Coke/Dielna dk60, Maguire, Palmer/Helan dk69, Maghoma, May na Madine/Nuhiu dk60.

RONALDO SI WA KAWAIDA, HIZO REKODI ANAZOVUNJA NI BALAA! ZIONE HAPA

MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amezidi kuweka rekodi ngumu katika ulimwengu wa soka, baada ya jana kufunga mabao manne katika ushindi wa 5-1 dhidi ya Elche katika La Liga.
Katika mabao hayo manne, mawili yalikuwa ya penalti na hiyo inamaanisha Ronaldo anawea kufunga kila wakati Real Madrid ikizawadiwa tuta.
Unaweza kutundika matairi kadhaa ya gari pembezoni mwa lango na umuambie bao litahesabiwa pale tu atakpopitisha mpira katikati yake mojawapo, na kisha uweke makipa wawili kwenye mstari, na bado atafunga.
"Si kawaida" hivyo ndivyo makocha wengi wa timu pinzani wamekuwa wakisema kuhusu yeye tangu aibuke mfungaji bora wa jumla wa Real Madrid miaka mitano iliyopita. Na hapana, si kawaida,".

RONALDO THE RECORD-BREAKER
Zifuatazo ni baadhi ya rekodi ambazo Cristiano Ronaldo anazoshikilia:
Mabao mengi aliyofunga msimu mmoja kwenye Kombe la Ulaya: 17
Mchezaji pekee kushinea kiatu cha dhahabu Ulaya katika ligi mbili tofauti (Ligi Kuu England akiwa na Manchester United na La Liga akiwa na Real Madrid)
Mchezaji wa kwanza kufunga dhidi ya timu kila timu katika msimu mmoja La Liga
Mabao mengi aliyofunga kwenye mashinano yote Real Madrid kwa msimu: 60
Hat-trick nyingi alizofunga kwa msimu mmoja Real Madrid: 7
Mchezaji aliyefunga mabao 250 kwa haraka zaidi Real Madrid
Mfungaji bora wa kihistoria Ureni kwa mabao yake 50

MABAO YA RONALDO KWA UJUMLA
Mwaka           Timuu                      Mechi  Mabao
2002-2003     Sporting Lisbon       31      5
2003-2009     Manchester United  292    118
2009-             Real Madrid             254    264
2003-             Ureno                       114    50
REKODI ZAIDI ZA RONALDO ZINAKUJA...
Mabao tisa aliyofunga Ronaldo katika mechi tano za La Liga ni moja zaidi ya Lionel Messi wakati nyota huyo wa Barcelona alipofikisha mabao 50 katika La Liga msimu wa 2011-12
Akiwa na mabao 264 katika miaka yake mitano ya kucheza Real Madrid, Ronaldo anahitaji manbao 59 kumfikia Raul aliyefunga mabao 323, kwa zaidi ya miaka 16.
Ronaldo sasa amefikisha hat trick 21 katika La Liga, mbili zaidi ya Messi na moja nyuma ya anayesukilia rekodi, Alfredo Di Stefano