Tuesday, October 21, 2014
HUYU NDO MCHEZAJI ALIYEFARIKI AKIJARIBU KUSHANGILIA BAO KAMA MIROSLAV KLOSE
EPL: HIKI NDO KILICHOIPATA MANCHESTER UNITED DHIDI YA WEST BROM USIKU HUU
HIKI NDICHO ALICHOKISEMA MSANII DAVIDO ALIVYOKUA AKIONDOKA TANZANIA!
Monday, October 20, 2014
Ommy Dimpoz atoboa siri ya picha anayoonekana akishuka kwenye treni ‘tusiamini kila tukionacho mtandaoni’
TEAM DIAMOND YAZUNGUMZIA SUALA LA KUZOMEWA KWA DIAMOND KWENYE FIESTA
MILIONI 58 ZAFUTA BAO TATU ZA WAZI SIMBA
CRD:Mwanaspoti
HILI NI PIGO LINGINE KUBWA LILILOIPATA TASNIA YA FILAMU TANZANIA MCHANA WA LEO
Mdogo wa aliyekuwa muigizaji na muongozaji wa filamu marehemu George Otieno ‘Tyson’ aitwaye Benson Okumu Otieno 'Benii' enzi za uhai wake.
Mdogo wa aliyekuwa muigizaji na muongozaji wa filamu marehemu George Otieno ‘Tyson’ aitwaye Benson Okumu Otieno 'Benii' amefariki dunia ghafla katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar mchana leo. Msiba upo Sinza Vatican
Benii alikuwa muigizaji na muongozaji wa filamu mbalimbali nchini. Mipango ya mazishi ya kumpeleka kwao Kenya
GPL
HESHIMA: WEMA SEPETU APIGWA BAO NA FLORA MVUNGI NA MUMEWE H.BABA!
BAADA YA MAMBO KUMFIKA SHINGONI: MISS TZ 2014 AKIMBILIA KANISANI
OMMY DIMPOZ: ASANTE VANESSA MDEE KWA KUNIPOKEA FUKO LANGU
ALICHOFANYIWA DIAMOND FIESTA…NIMEAMINI MAISHA BILA UNAFKI HAYAENDI
Nakumbuka miaka mitano iliyopita aliyekuwa nguli wa filamu Nchini Tanzania marehemu “”Steven Kanumba”” alienda kwenye jumba la Big Brother….
amini usiamini bila sababu yyte ya maana watanzania ndo walikuwa wa kwanza kuanza kumsema kuwa hajui kuvaa, nani alimchagua , hajui kiingereza mpaka kufikia kumuigiza!!! Walisahau hata watu maruufu kama Messi na wengine wengi hawajui kuongea kabisa lugha hiyo..
Baada ya kifo chake watanzania hawahawa wakaanza kusema alikuwa nguli aliyetuwakilisha vizuri nje ya nchi na kulia sana!!!kumbe wakati akiwa hai tulikuwa tunamshusha chini..
Miaka mitano baadae Tanzania imempata mtu anayeiwakilisha vizuri nje ya mipaka na kuitangaza vizuri nchi yake..
Pasipokuwa na sababu za msingi (chuki binafsi tu)anapangiwa njama za kuzomewa na kuabishwa katika ardhi ya nchi yake ambayo kwa namna moja au nyingine kuna watu wameifahamu sababu yake!! Ukiuliza sababu za wengi wao kumchukia ni mafanikio yake lakini hata kama humpendi mtu hivi ndo hadi umzomee kwa kiasi kile !!!
leo na kesho naye huyu akitoka utaskia hawahawa waliokuwa wanamzomea wanaanza kusema jamaa alikuwa anatuwakilisha vizuri sana , ametutangaza sana kimataifa!! lakini Watanzania wenzake ndio vinara wa kumuangusha..
Si lazima kila mtu ampende Diamond ila kutumia nguvu kubwa sana kumuangusha mtu ni ishara ya uwoga na Roho ya kimaskini…
Nimeamini “”maisha bila unafki hayaendi”
UONGOZI MZIMA WA MDADISIBLOG UNAMTAKIA HAPPY BIRTHDAY MR BOB MAU
MASTAA WOTE WABONGO KWANINI MSIIGE MFANO WA HUYU
BAADA YA VIPIGO MFULULIZO NDANDA FC YAAMUA KUFANYA FUKUZA FUKUZA
HII NI KWA MASHABIKI WA CHELSEA! HIKI NDO KITU KINACHOENDELEA KUHUSU DIEGO COSTA
BAADA YA SARE YAO, HIKI NDICHO KILICHO MBELE YAO SIMBA NA YANGA, MWAKA HUU KAZI IPO!
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
MIAMBA ya soka Tanzania, Simba na Yanga iligawana pointi Jumamosi baada ya sare ya bila kufungana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Sare hiyo inaifanya Simba SC itimize pointi nne baada ya awali kutoa sare tatu pia, wakati Yanga SC inafikisha pointi saba baada ya mechi nne, ikiwa nyuma ya Azam FC na Mtibwa Sugar zenye pointi 10 kila moja kileleni mwa Ligi.
Pamoja na kushinda 2-1 mara mbili dhidi ya Prisons na JKT Ruvu, lakini Yanga SC ilikutana na upinzani mkali na matokeo yangeweza kuwa kinyume kama si bahati yao.
RATIBA RAUNDI MBILI ZIJAZO LIGI KJUU BARA
Oktoba 25, 2014
Stand United Vs Yanga SC
Ndanda FC Vs Mgambo JKT
Kagera Sugar Vs Coastal Union
Azam Fc Vs JKT Ruvu
Prisons Vs Simba SC
Ruvu Shoot Vs Polisi Moro
Oktoba 26, 2014
Mbeya City Vs Mtibwa Sugar
Novemba 1, 2014
Kagera Sugar Vs Yanga SC
Coastal Union Vs Ruvu Shooting
JKT Ruvu Vs Polisi Morogoro
Ndanda FC Vs Azam FC
Stand United Vs Prisons
Mtibwa Sugar Vs Simba SC
Novemba 2, 2014
Mgambo JKT Vs Mbeya City
Yanga SC sasa watasafiri hadi Shinyanga kuwafuata Stand United waliopanda Ligi Kuu msimu huu, mchezo utakaofanyika Jumamosi Uwanja wa Kambarage.
Stand imeonyesha ni timu imara ikifanikiwa kuvuna pointi tano katika mechi za ugenini, kutokana na sare mbili dhidi ya Simba SC na Kagera Sugar na ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Mgambo.
Stand ilipoteza mchezo wa kwanza nyumbani kwa kufungwa 4-1 na Ndanda FC ya Mtwara iliyopanda pia Ligi Kuu msimu huu, lakini baada ya hapo imecheza mechi tatu ugenini bila kufungwa.
Pata picha Yanga SC wanakwenda kukutana na upinzani wa aina gani katika mchezo huo Jumamosi.
Simba SC sasa. Watacheza na Prisons ya Mbeya Jumamosi Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Prisons ilionyesha upinzani ikifungwa na Yanga SC 2-1 na pia ilishinda ugenini 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting kabla ya kutoa sare ya 0-0 na Azam FC Mbeya.
Jana, Prisons wamefungwa 2-1 na JKT Ruvu Mbeya na baada ya mchezo huo, kocha Juma Mwambusi akasema amekubali matokeo na anaelekeza nguvu zake katika mchezo ujao.
Simba SC ambayo haijashinda mechi msimu huu kwa kutoa sare nne, unafikiri inakabiliwa na mechi ya aina gani mwishoni mwa wiki?
Sunday, October 19, 2014
DIVA WA CLOUDS AFUNGUKA MAZITO KUHUSU MAHUSIANO YAKE YA KIMAPENZI!







