MATAJIRI wa Simba wamefurahishwa na
matokeo ya suluhu waliyopata dhidi ya
Yanga na kusema bila kambi yao ya
nchini Afrika Kusini wangeweza
kufungwa si chini ya mabao 3-0 na
Yanga.
Kabla ya matokeo hayo ya juzi
Jumamosi pale Uwanja wa Taifa, Simba
ilikuwa Afrika Kusini ambako iliweka
kambi ya siku nane kujiandaa na
mchezo huo wa Ligi Kuu Bara ambao
ulimalizika suluhu.
Akizungumza na Mwanaspoti, Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya
Simba, Kassim Dewji ‘KD’, alisema kikosi
chao kilikuwa katika hali mbaya ya
kuweza kupoteza vibaya mechi dhidi ya
Yanga na wasingefanya jitihada hizo
wangejikuta wanapata kipigo cha aibu.
Dewji ambaye ndiye aliyekuwa mmoja
wa waratibu wa kambi hiyo, alisema
Yanga kabla ya mchezo huo walikuwa
katika morali nzuri kuliko Simba.
Alisema kambi na gharama mbalimbali
walizoziingia zimewagharimu zaidi ya
Dola 350,000 ambazo ni sawa na Sh58
milioni.
“Hatukuwa katika hali nzuri,
tulilazimika kutumia akili hiyo ya
haraka kuinusuru klabu kupata kipigo
cha aibu maana tuliangalia timu yetu
kulinganisha na Yanga na kubaini
endapo tusingeandaa ile kambi
tungeweza kupata kipigo cha aibu cha si
chini ya bao 3-0,”alisema Dewji.
Matokeo hayo yamewakera mabosi wa
Yanga waliokuwa wanataka ushindi
kuziba kelele za Simba huku wachezaji
kilio chao ni kukosa Sh80 milioni
walizoahidiwa endapo wangeshinda
huku Simba nao wakikosa Sh100 milioni
ambazo wangepewa kama wangeishinda
Yanga.
“Tulipambana sana hasa sisi mabeki,
lakini tatizo lilikuwa mbele katika
umaliziaji tu, tulikuwa tunalala na fedha
uongozi ulituletea Sh80 milioni taslimu
na ukatuhoji nani akabidhiwe lakini
ndiyo hivyo tumechemsha,” alisema kwa
huzuni beki mmoja wa Yanga. |
0 comments:
Post a Comment