Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale
amesema haoni kama wameathirika na kundi la
watu waliomzomea msanii huyo wakati
akitumbuiza Jumamosi hii kwenye show ya
Serengeti Fiesta, Leaders Club jijini Dar es
Salaam.
Tale amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM
kuwa walikuwa na taarifa kuhusu mpango huo
hata kabla ya show na hivyo walijiandaa.
“Tulikuwa tumemjenga kisaikolojia, kwahiyo hiyo
ni sehemu ya kazi na mashabiki ingekuwa
wanapiga kelele kama tumekosea show kweli,
lakini sio hivyo. Show ilikuwa sawa,” amesema
Tale.
“Tunachojua sisi msanii wetu anafanya vizuri na
sasa hivi nguvu zetu tumeelekeza katika tuzo.
Wananchi wakaze kumpigia kula katika tuzo
Channel O na MTV, sie sasa hivi tunasonga
mbele, tunachojua chema chajiuza, kibaya
chajitembeza.” |
0 comments:
Post a Comment