Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu
aliopotangazwa mshindi.
Ziba masikio, fanya yako! Wakati watu
wakichonga juu ya sakata la madai ya
kuwa na mtoto na utata juu ya umri wake,
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu
anadaiwa kukimbilia kanisani. Habari za
uhakika zilidai kwamba, baada ya kutwaa
taji hilo hivi karibuni na kuibua
sintofahamu, mrembo huyo alikimbilia
kwenye Kanisa la Ufunuo kwa Nabii Yaspi
Bendera lilipo Yombo-Buza jijini Dar kwa
ajili ya kumshukuru Mungu kwa
kufanikisha ndoto yake ya kuwa Miss
Tanzania.
Ilidaiwa kwamba, Sitti ambaye ni mtoto wa
Mbunge wa Temeke kwa leseni ya CCM,
Abbas Zuberi Mtemvu, akiongozana na
mama yake, walikwenda kwenye kanisa
hilo kwa ajili ya kutoa shukrani kwa wema
aliomtendea Mungu.
“Watu wanaendelea kumsema mtoto wa
mwenzao huku yeye anamshukuru Mungu
kwa sababu hata kabla hajatwaa taji hilo
alikuwa akisali hapa hivyo Mungu
amepokea maombi yake na si vinginevyo
kama watu wanavyomsimanga,” alisema
muumini mmoja wa kanisa hilo. |
0 comments:
Post a Comment