Sunday, October 19, 2014

MATOKEO YA LIVERPOOL vs QPR HAYA HAPA

LIVERPOOL imeshinda 3-2 dhidi ya Queens Park Rangers jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa ugenini. Mabao ya Liverpool yamefungwa na Richard Dunne aliyejifunga dakika ya 67, Philip Coutinho dakika ya 90 na Steven Caulker aliyejifunga pia dakika hiyo hiyo ya 90. Richard Dunne leo ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kujifunga mabao 10 katika historia ya Ligi Kuu ya England. Raheem Sterling alianza leo kwenye kikosi cha Liverpool na kocha wa England, Roy Hodgson akamshuhudia kutokea jukwaani. Mario Balotelli alikosa bao akiwa amebaki yeye na nyavu, baada ya kupiga juu akiwa umbali wa mita tatu wakati huo matokeo bado yapo sare.

WATOTO WA SHILOLE WAMPA MTIHANI NUH MZIWANDA!

Watoto wawili wa kike wa muimbaji wa Tanzania, Shilole, hawamuiti mpenzi wa staa huyo Nuh Mziwanda ‘baba’ bali ‘uncle’ Akiongea na Power Jams ya East Africa Radio, Nuh amesema watoto hao wanampenda. “Watoto wananiita uncle,” amesema Nuh. “Nafurahi nikiamka asubuhi ‘uncle good morning’, yaani fresh, ‘uncle maji ya kuoga’. Ni watoto lakini wananipenda, wana love kwangu. Kuna

 BOFYA HAPA KUSOMA ZAID> 

TAZAMA PICHA ZAIDI YA 2O KILICHOJIRI JANA KWENYE SERENGETI FIESTA 2014 VIWANJA VYA LEADERS

Msanii kutoka Nchini Marekani T.I akitoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Dar Katika Show ya FIesta iliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya Leaders.
Msanii Davido kutoka nchini Nigeria Akiwajibika
Diamond Platnumz akitoa burudani

 BONYEZA HAPA KUANGALIA PICHA ZINGINE 

WATANGAZAJI MAMBURULAAZ WA TELEVISHENI WAAMUA KUTANGAZA KIPINDI WAKIWA HIVI

Watangazaji wawili wa kipindi cha
televishen "The View" wamewapa
watazamaji wao mshangao pale walipovua nguo zao na kubaki uchi wakati show hiyoikiendelea Sherri Shepard na Jenny McCarthy wliamua kubadilisha mambo na kutangaza kipindi chao wakiwa uchi wa mnyama. Watazamajihawakuonekana kujali
kutokana na tukio hilo na kuwapigia
makofi na kelele nying

Saturday, October 18, 2014

LIVE KUTOKA TAIFA; YANGA VS SIMBA

Dk 4 Okwi anaingia na
kujaribu lakini shuti lake
linakuwa nyanya.
Dk 6, Jaja anapiga kichwa
lakini kinatoka nje kidogo ya
lango la Simba.

Picha na salehally

KALI DUNIA NZIMA HAIJAWAHI KUTOKEA, REFA NICOLAS AMLIMA KADI NYEKUNDU CAVANI KISA KUSHANGILIA KWA STAILI YA MTUTU WA BUNDUKI

MSHAMBULIAJI Edinson Cavani jana alikuwa miongoni mwa wachezaji watatu walioonyeshwa kadi nyekundu wakati Paris St Germain ikiitandika RC Lens mabao 3-1 katika mchezo wa Ligue 1 Uwanja wa Stade de France. Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ufaransa alipewa kadi hiyo na refa Nicolas Rainville, baada ya kushangilia bao la mwisho la timu yake kwa ishara ya kupiga bunduki, staili maarufu kwa klabu ya Arsenal ya England. Rais wa PSG, Nasser Al-Khelaifi ameponda maamuzi hayo ya utata akisema kwamba kama adhabu zitatolewa kwa ushangiliaji wa aina hiyo, ni mbaya kwa soka ya Ufaransa. Mabao ya PSG yalifungwa na Cabaye dakika ya 28, Maxwell dakika ya 33 na Cavani dakika ya 55, wakati Lens pia ilipoteza wachezaji wawili waliotelewa kwa kadi nyekundu, Gbamin na Le Moigne, huku bao lao la kufutia machozi likifungwa ma Coulibaly dakika ya 10.
Mshambuliaji wa Paris Saint Germain, Edinson Cavani akiwa hamming macho yake wakati analimwa kadi nyekundu
Hiruhusiwi Ufaransa; Edinson Cavani akishangi kwa staili ya mtutu wa bunduki kabla ya kutol kwa kadi nyekundu

HILI NI PIGO LINGINE KUBWA WALILOLIPATA TIMU YA LIVERPOOL

KLABU ya Liverpool imepata pigo kubwa jana wakati Daniel Sturridge alipotakiwa kuwa nje kwa angalau wiki tatu zaidi baada ya kuumia tena mazoezini.
Kocha Brendan Rodgers amekuwa na matumaini kupona kwa mshambuliaji huyo kungeimarisha kikosi chake.
Sasa Sturridge, ambaye aliumia ndama wakati wa kupasha misuli moto Melwood Alhamisi, atakosa mechi kadhaa ngumu zikiwemo za nyumbani na ugenini za Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid.

Mshambuliaji wa Liverpool, Daniel Sturridge anatarajiwa kuendelea kuwa nje kwa wiki tatu zaidi

MECHI ZA LIVERPOOL AMBAZO SASA STURRIDGE ATAZIKOSA
1. QPR v Liverpool
2. Liverpool v Real Madrid
3. Liverpool v Hull
4. Liverpool v Swansea
5. Newcastle v Liverpool
6. Real Madrid v Liverpool
7. Liverpool v Chelsea
Liverpool itakuwa na mechi saba katika wiki tatu zijazo ikiwemo ya hatua ya 16 Bora ya Kombe la Ligi, au Capital One dhidi ya Swansea Oktoba 28 na ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Chelsea Uwanja wa Anfield Novemba 8.
Sturridge alipona maumivu ya mguu aliyopata akiichezea timu ya taifa ya England Septemba mwaka huu, maumivu ambayo yalizua mtafaruku baina ya Rodgers na kocha wa Three Lions, Roy Hodgson juu ya muda wa kupona kwa mpachika mabao huyo.

TUKIO ZIMA LA MAMA MCHAWI ALIYEDONDOKA WAKATI AKIJIANDAA KWENDA KUMUUA MJUKUU WAKE

hivi karibuni tuliweka hewani tukio zima la mama mchawi wa kinigeria aliyekuwa amedondoka chini huku akiwa uchi na mwili ukiwa na vidonda sehemu zote... Mama huyo alidondoka dakika chache baada ya kujigeuza ndege na kupaa hewani akienda kuua mtoto mchanga wa binti yake wa kumzaa. Inadaiwa kuwa. binti huyo amekuwa akizaa watoto na kufariki dakika chache baada ya kuzaliwa. Kumbe mbaya wake alikuwa ni mama yake mzazi ambaye alikuwa akivifuata vitoto hivyo na kisha kuviua.Imearifiwa kuwa dada wa watu kazunguka kwa waganga mbalimbali kutafuta tiba bila mafanikio, na ndipo alipoamua kumrudia mwenyezi mungu kwa kumpigia magoti, kumlilia na kumweleza shida zake kwa njia ya maombi, kitu ambacho Mungu baba wa mbinguni amekijibu na kumdondosha mama huyo baada ya nguvu ya maombi kumzidi.Hapo chini nimekuwekea video nzima toka Nigeria ikionesha tukio zima la mama huyo na jinsi polisi walivyokuwa wakihangaika kumnusuru asichomwe moto.

 BOFYA HAPA KUIANGALIA VIDEO 

ANGALIA HII VIDEO ALICHOFANYIWA BAADA YA KUMSHIKA MCHEZAJI

Muamuzi Manuel Zeleya ameingia katika lindi la lawama kutoka kwa wachezaji pamoja na viongozi wa klabu ya Marathon inayoshiriki ligi kuu ya nchini Honduras, kufuatia adhabu ya kadi nyekundu aliyompa mlinda mlango wa klabu hiyo. Viongozi pamoja na wachezaji wamekuwa wakimlalamikia muamuzi huyo kufuatia maamuzi mazito aliyoyachukua, na kupelekea kikosi chao kicheza pungufu. Muamuzi Zeleya alichukua jukumu la kumuadhibu mlinda mlango wa klabu ya Marathon, Junior Morales wakati wa mchezo wa ligi uliowakutanisha na Real Sociedad, kutokana na utovu wa nidhamu aliouonyesha wa kumshika makalio kwa makusudi mchezaji wa timu pinzani. Hata hivyo muamuzi huyo hakuona kosa hilo, mpaka pale aliposhtuliwa na msaidia wake namba mbili, na katika hali ya mshangao alichukua maamuzi ya kumuonyesha kadi nyekundu Junior Morales na mwisho wa mambo aliamuru mkwaju wa penati kupigwa kwenye lango la Marathon. Wakati maamuzi hayo yanachukuliwa tayari timu hizo zilikuwa zimefungana bao moja kwa moja. Katika picha za televisheni Junior Morales ameonekana akimshika makalio mshambuliaji wa Real Sociedad, Morales kwa makusudi baada ya kuumiliki mpira uliokuwa unaambaa ambaa kwenye lango lake. Hata hivyo Henry Martinez aliechukua jukumu la kupiga mkwaju wa penati kufuatia maamuzi yaliyochukuliwa na Manuel Zeleya, alikosa na hivyo kuufanya mchezo huo kumalizika kwa matokeo ya sare ya bao moja kwa moja.

 BOFYA HAPA KUIONA VIDEO HIYOO 

MREMBO ANAYEONGOZA BONGO KWA KUWAZUZUA WANAUME HUYU HAPA

UNAJUA KUWA KUNA UWEZEKANO DAVIDO ASISHIRIKI TAMASHA LA FIESTA KWA AMRI YA MAHAKAMA! SHUKA NAYO HAPA

Friday, October 17, 2014

KILICHOMPATA ADMIN WA BLOG MOJA HIVI KUHUSIANA NA KUMTETEA MISS TANZANIA 2014 WEE...SOMA HAPO CHINI

Sekeseke hilo limeendelea kutokea katika blog moja ambayo inahusika na umbea wa hapa Mjini ambapo admin wake aliweka mada kuhusiana na Ushindi na Umri wa Miss Tanzania 2014 aka Miss France, Miss 23 mara baada ya kuweka mada hiyo Basi Wachangiaji wakachangia na ndipo Baadae Admin wa Blog hiyo akaweka post Yenye kumtete Unajua Alichokipata Fuatilia threat hizo chini hapo........................ Na Haya ndio Maneno ya Admi wa Blog hiyo Ya Udaku aka Umbea.... Duuh ..Nimekoma! Leo nilipost Post Moja Nikimtetea Miss Tanzania kwa Kile Kinachoendelea Mitandaoni Kuhusu Ushindi wake na Umri ..Yenye Kichwa cha habari : Tumechokaaa na Story za Miss Tanzania ooh Hana Vigezo ooh Sijui Mkubwa Mara Nini na Nini "Watz bwana hata angepewa nani hilo taji la miss Tanzania msingerizika mngemchamba tu ! Muacheni Mtoto wa watu apumue kama kushinda ndio kashashinda umri wake unaingiliana vipi na umiss?" Nilichoambulia nia Kupewa za uso live Bila chenga ....Hii inaonesha Issue hii ya Miss Tanzania Bado Inaendelea kuwagusa Watu Sana Kiasi kikubwa. Soma Hapo chini Nilichoambia na Wadau wa Udaku ...Mekoma mie...Wapi Lundenga?

WEMA SEPETU USO KWA USO NA MUME WA LADY JAY DEE, GADNER!

Muigizaji maarufu nchini Wema Sepetu na Mchekeshaji MC Pilipili wanatarajiwa kuwa wa kwanza kukizindua kipindi cha Kili Chat Shows kinachotarajiwa kuanza leo. Kipindi hicho kitakachokuwa kikiendeshwa na Gadner G Habash kitakuwa ni cha nusu saa na kitakuwa kikiwakutanisha mastaa wawili wanaoshabikia timu za Yanga na Simba ambapo watapata nafasi ya kushindana namna wanavyozielewa klabu hizo. Pia mashabiki watapata nafasi ya kuwahoji maswali kuhusu shughuli zao.Kipindi hicho kitakachokuwa kikirushwa Alhamisi saa tatu usiku katika kituo cha East Africa TV ni wa kampeni ya Nani Mtani Jembe ambayo ilianza mwanzoni mwa mwezi huu kwa mashabiki wa Yanga na Simba kushiriki kampeni hiyo ambayo jumla ya Sh 100 zinashindaniwa kwa mashabiki kupiga kura kwa SMS kwa kutuma namba za ndani ya kizibo kila wanapokunywa bia ya Kilimanjaro.

MAKAVU LIVE: JOHARI, CHUCHU HUU KAMA SIYO USHAMBA NI NINI?

MASANJA MKANDAMIZAJI NAYE AVUNJA UKIMYA JUU YA SAKATA LA MISS TANZANIA 2014

MISS TANZANIAAAAAA!!! ...HIVI LUNGENGA UKOJE? ...NILIKUWA NAKUAMINIA SANA.. ...SASA MBONA UNANIANGUSHA BRO! ...HIVI HAYO MANENO WANAYOSEMA HUYASIKIIIII?? ...HIVI UNATAKA MUNGU AKUPE NINI LAKINIII? ...HIVI UNATAKA MPAKA UISIKIE SAUTI YA MUNGU NDO USHTUKE... ...AMKA BRO WAKE UPPPPPPPPPP!!

ANGALIA HII PICHA INASEMA MENGI SANA AMUA MWENYEWE INASEMA NINI TENA LIVE!!

KAMATI YA MISS TANZANIA WALIKOROGA ZAIDI ONA WALICHOSEMA NA USHAHIDI UPO WAZI LIVE!!

East Africa Television (EATV) MISS TANZANIA 2014 SITTI MTEMVU ANA MIAKA 23 NA SIO 18 Katibu wa kamati ya Miss Tanzania Bosco Majaliwa amesema kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu amezaliwa mei 31 mwaka 1991 na umri wake sahihi ni miaka 23 na sio miaka 18 kama ilivyozagaa sehemu mbalimbali. Katibu huyo aliongeza kuwa Sitti ana shahada ya ya uhusiano wa kimataifa na alimaliza masomo yake Desemba mwaka jana katika chuo kikuu cha North Texas kilichoko kwenye jiji la Dallas nchini Marekani. Sitti Mtemvu bado hajasoma ngazi ya shahada ya uzamili (Masters) kwa sasa ila anatarajiwa kwenda kusoma ngazi hiyo huko nchini Marekani.

PICHA ZA GARI JIPYA LA KIFAHARI LINALODAIWA KUWA LA DIAMOND PLATNUMZ

Gari aina ya Mercedes 350 Cdi inyosemekana inamilikiwa na msanii Diamond. Hiyo ni Mercedes Ml 350 Cdi ya mwaka 2014 Radio Mbao moja ya mjini imevumisha kwamba ni kitu kipya cha Diamond Platnumz bado hata namba hakijabatizwa nazo na ni kipya kabisa kama Waswahili wasemavyo zero kilomita. Hivi wote mwajua hakuna siri dunia hii , na kama halipo lajongea , ukweli utajulikana tu …

TAARIFA YA JWTZ KUHUSU TUHUMA ZA ASKARI WAKE KUWAPORA WAVUVI HUKO MARA

MPIGA DEBE HUYU AUSHANGAZA UMMA MKOANI MBEYA KWA KITENDO HIKI ALICHOFANYA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida , mpigadebe maarufu katika kituo cha mabasi cha mbalizi wilayani mbeya amenunua mbuzi wawili na bidhaa nyingine za aina mbalimbali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja na kuzipeleka kwenye vituo vya watoto yatima kama zawadi huku akiwaasa watoto hao kutoshawishika kwenda kupiga debe kwenye vituo vya mabasi. Mpigadebe maarufu katika kituo cha mabasi cha mbalizi, Anganile Mwamuluma Andrea ambaye amefanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 20 ameushangaza umma wa wakazi wa mbeya baada ya kuamua kununua mbuzi wawili, mchele , maharagwe, sabuni, mafuta ya kupikia na mahindi na kupeleka bidhaa hizo katika vituo viwili vya watoto yatima ambako amezitoa kama zawadi kwa watoto hao , huku akiwaasa kutoshawishika kujihusisha na kazi ya kupiga Debe kwenye vituo vya mabasi .
Walimu wa watoto hao wameeleza kushtushwa na kitendo cha mpigadebe huyo, lakini wakasema kuwa ni mfano Bora wa kuigwa kwa vijana wanaofanikiwa kukumbuka mazingira walikotoka, huku wakiwahimiza wazazi kuongeza upendo kwa watoto wao ili kupunguza wimbi la watoto wanaoishi katika mazingira magumu nchini . Baadhi ya watoto ambao wamepokea msaada huo , wamemshukuru mpigadebe huyo na kuwataka watu wengine kupata funzo la kuthamini na kuwapenda watoto ikiwa ni pamoja na kuwaandalia mazingira mazuri ya kujitegemea. ITV