Friday, August 29, 2014

YANGA KUVUNJA UKIMYA KUHUSU OKWI LEO HII

Siku moja baada ya kujiunga na Simba huku akiwa bado na mkataba na Yanga, uongozi wa Yanga utatoa ufafanuzi kuhusiana na Emmanuel Okwi. Yanga itatoa ufafanuzi kuhusiana na Okwi kuamua kwenda Simba. Habari kutoka ndani ya Yanga zinaeleza uongozi wa klabu hiyo kongwe utatoa ufafanuzi kuhusiana na uamuzi wa kumsajili Okwi. Okwi ametua Simba ikiwa ni siku chache tu baada ya Yanga kuwasilisha barua TFF ikitaka afungiwe kutokana na kukiuka kanuni. Yanga pia iliomba ilipwe fidia ya dola 200,000 (Sh milioni 330). Kabla ya TFF haijajibu lolote kuhusiana na suala hilo, Okwi ametua Simba



Posted via Blogaway

TETESI ZA SOKA ZILIZOSHAMILI KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA ULAYA LEO IJUMAA ZIPO HAPA

Boss wa Manchester United Louis van Gaal anajaribu kumnunua kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, na beki wa Ajax Daley Blind, 24, kabla ya dirisha la usajili kufungwa Septemba mosi (Daily Mirror), United watalazimika kulipa pauni milioni 20 kumsajili Blind (Sun), Liverpool bado wanajaribu kumfuatilia kiungo wa zamani wa Arsenal Alex Song, 26, ambaye yuko Barcelona (Metro), meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hatotaka kuwasajili Danny Welbeck, 23, kutoka Man U, Radamel Falcao kutoka Monaco, 28, na Nikola Zigic, 33, kutoka Birmingham (London24.com), Manchester United watapanda dau la pauni milioni 24 kwa kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 22, wakati Louis van Gaal akitaka kuwaondoa Welbeck, Tom Cleverly, 25, na Shinji Kagawa, 25 (Daily Telegraph), Cleverly yuko tayari kusalia hadi mwaka ujao mkataba wake utakapokwisha (Independent), Sunderland wametoa dau la pauni milioni 6 kumsajili beki Virgil van Dijk, 23, kutoka Celtic baada ya Toby Alderweireld, 25 wa Atletico Madrid kukataa kwenda kuichezea Black Cats (Times), mchezaji wa zamani wa Juventus Allesandro Del Piero amekubali kujiunga na Delhi Dynamos ya India baada ya mkataba wake na Sudney FC kumalizika (Football Italia), Crystal Palace wanajiandaa kumsajili tena Wilfried Zaha kutoka Manchester United baada ya Neil Warnock kurejea kama meneja (Daily Star), kiungo wa Real Madrid Xabi Alonso, 32 anakaribia kujiunga na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich kwa pauni milioni 8 (Guardian), Real Madrid wanataka kumsajili Marco Reus lakini wapo tayari kusubiri hadi msimu ujao (AS), Chelsea wamekubali euro milioni 12.5 kutoka AC Milan kumsajili Fernando Torres (The Sun), Borussia Dortmund wameonesha nia ya kumrejesha Shinji Kagawa katika Bundesliga, baada ya kushindwa kuwika akiwa Old Trafford (Kicker), maafisa wa Juventus wamekutana na maafisa wa Monaco kujadili suala la Radamel Falcao kwa mkopo (Gazetta dello Sport), Inter Milan wanataka kumchukua Xherdan Shaqiri kutoka Bayern Munich, iwapo Ricky Alvarez ataondoka wiki hii kwenda Sunderland (Corriere dello Sport) Diego Costa huenda akakosa kucheza kwa wiki sita baada ya kuumia msuli wa paja (Daily Telegraph). Zimesalia siku nne kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.

Posted via Blogaway

Shahidi Aelezea jinsi Alivyofanyishwa Mapenzi na Mganga wa Jadi, Isome hii kama ajabu vile.

Shahidi wa pili katika kesi ya kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu inayomkabili mganga wa kienyeji, Yahaya Michael (34) ameieleza Mahakama ya Wilaya ya Ilala jinsi alivyoingiliwa kimwili na mganga huyo kwa madai kwamba atampatia dawa ya kupata mtoto. Mwanahamisi Omary (26) alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Hassan Juma kuwa alimfahamu mganga huyo baada ya kusumbuliwa na tumbo la uzazi kwa muda mrefu. Akiongozwa na Wakili wa Serikali Felista Mosha, Mwanahamisi alidai alikuwa akitibiwa ugonjwa huo bila ya kutoa taarifa kwa mumewe Edrick Elinezer. Alidai alitibiwa kwa miezi sita bila ya mafanikio. Shahidi huyo alidai Aprili, mwaka huu, Michael alimwambia kuwa ana majini hivyo hawezi kupata mtoto na kumpatia dawa kwa ajili ya kunywa na kuoga. Alidai mganga huyo alikuwa akimtibu nyumbani kwake lakini baadaye alihamishia ofisi yake katika nyumba ya kulala wageni iliyopo Kigogo Luhanga na kudai kuwa mganga huyo alikuwa akipaka dawa katika uume wake na kumuingilia kimwili huku akiwa hajitambui kwa madai kwamba atamsaidia kupata mtoto. Aliendelea kudai kwamba baada ya kutokuwa na mawasiliano kwa muda mrefu na mumewe, alipata taarifa kuwa mume wake alipigiwa simu na mganga huyo na kumtaka apeleke gari lake Toyota Rav4 lenye namba za usajili T 139 BSG maeneo ya Jangwani kwa kuwa majini ya mkewe yanataka mtoto. Awali, Hakimu Juma alisema wadhamini wa mshitakiwa wanatakiwa kumtafuta mshitakiwa huyo na kumfikisha Mahakamani hapo, aliwatahadharisha wasipofanya hivyo kwa wakati watalipa faini ya Sh milioni sita kwa kila mmoja. Michael alidaiwa Aprili 29, mwaka jana, maeneo ya Jangwani Wilaya ya Ilala, alijipatia gari aina ya Toyota Rav4 T 139 BSG lenye thamani ya Sh milioni 12 mali ya Eliezer kwa njia ya udanganyifu. Kesi hiyo itasikilizwa tena Septemba 18, mwaka huu.

Posted via Blogaway

soma hapa Alichosema wema baada ya Diamond kutangaza ndoa

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz ametangaza ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Wema Sepetu anayosema itafungwa hivi karibuni. Msanii huyo ghali zaidi nchini kwa sasa, ametamka hayo alipozungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam juzi Jumatano. Alisema kuna mambo mengi yaliyomchelewesha kufikia hatua hiyo, ikiwamo maandalizi kwani amepanga mashabiki wake wahudhurie harusi hiyo. “Ndoa ni kitu cha heri na baraka, lakini kitu kinachofanya kidogo mambo yachelewe ni kwamba sisi au mimi ni mtu ninayefahamika, kwa hiyo hata ndoa yangu watu wengi wanatamani waihudhurie,” alisema Diamond. Pia amesisitiza kwamba ndoa si jambo la masihara kwani ni tendo la kiimani na ndio maana amekuwa makini katika mipango yake. “Nataka kila kitu kishuhudiwe na mashabiki, ninaweza hata kuifanyia Uwanja wa Taifa,” aliongeza. “Unajua nilishindwa kufanya mambo haya haraka kwa sababu wengi nadhani wangeamini kwamba ninafanya hivyo ili kutafuta umaarufu zaidi, tunataka tufanye kiusahihi yasije tokea mambo kama ya Instagram tunataka tuje kuwa mfano wa kuigwa.” Alipoulizwa tarehe ya ndoa hiyo Diamond alisema: “Nilishasema ni hivi karibuni, unajua siku zote vitu vya kheri waswahili wanasema lazima uvifiche, hata Mwenyezi Mungu naye anasema anampenda mtu aliye na siri, lazima vitu vingine uvifiche ili vipate kufanikiwa. Wakati mwingine kunakuwa na husda, hasidi kwa hiyo ukiviweka wazi sana vinaweza kutofanikiwa.” Taarifa kwamba Diamond hataoa zilisambaa na kudaiwa kumchefua mchumba wake Wema Sepetu ambapo katika mahojiano mkali huyo wa wimbo ‘Mdogo Mdogo’ alisema: “Kwanza sikuwahi kusema siwezi kuoa, nilishtushwa na gazeti hilo, nilisikitika kwa kweli na iliniuma sana, lakini nikaona nikijibu nitaonekana kwamba sina adabu, kwa sababu siku zote anayeanza huwa haonekani lakini anayemaliza. Pia siwezi kubishana na vyombo vya habari, mwisho wa siku ni watu haohao nitawategemea wanifanyie kazi zangu,” alisema. Hata hivyo Diamond alisema mchumba wake anaumizwa na vichwa vya habari ambavyo vimekuwa mwiba kwake. “Hata hivyo magazeti yetu tumeshayazoea jinsi yanavyoandika, wakati mwingine inakuwa kama chachandu au kufurahisha baraza,” aliongeza. Kuhusu taarifa kwamba ameachana na mchumba wake huyo, alisema: “Hatuna tatizo watu wengi wanasema tumeachana, lakini hatujaachana na hatuwezi kujibishana. “Sijui nikujibu nini kwa sababu kila nitakachokujibu utaona namsifia kwa sababu yule ni mchumba wangu. “Lakini ninachoweza kukwambia ni kuwa sisi ndio tunaoujua ukweli wa uhusiano wetu. “Sidhani kama ni sahihi mapenzi yetu yakawa na wasemaji wengine zaidi yetu wenyewe. Sasa ni ajabu watu wanaposema yao.”

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

DIAMOND PLATNUMZ AMTEMBEZEA KICHAPO ‘HEAVY’ BABY AKE WEMA SEPETU CHANZO KIPO HAPA

Rais wa serikali ya watu wasafi Tanzania, Naseeb Abdul Ei Kei Ei Diamond Platnumz au Sukari ya warembo amemshushia kichapo cha mbwa mwizi, nyonga mkalia ini wake, Wema Abraham Sepetu huku chanzo kikidaiwa kuwa wivu wa mapenzi baini yake na mwanamitindo mrembo Victoria Kimani kutoka Area Code 254, Kenya. Hii ndio Picha(Selfie) iliyozua utata inayomuonyesha Ommy Dimpoz, Victoria Kimani na Diamond Platnumz wakiwa studio kabla ya Timbwili kutokea… Kwa mujibu wa gossip Cop ni kwamba ugomvi ulianzishwa kufuatia kitendo cha mmanyema anayefanya poa katika gemu ya muziki wa Bongo Fleva, Omari Nyembo ‘Ommy Dimpoz kuposti picha akiwa pamoja na Diamond na Victoria Kimani katika studio za T.H.T Kinondoni wakirekodi nyimbo yao na punde habari zilipomfikia madam Wema ndipo alipoamua kutimba eneo la tukio na hatimaye kuchezea kichapo kilichomfanya atoke nduki eneo la tukio. Pichani ni Madam Wema Sepetu baada ya kuchezea kichapo, ukitazama picha hiyo utaona jinsi Miss Tanzania huyo alivyovimba eneo la usoni baada ya kuchezea vitasa vkutoka kwa Rais wa Wasafi.

Posted via Blogaway

Good news!! hivi ndivyo makundi ya Champions League yalivyopangwa

Hatimaye ligi ya mabingwa wa Ulaya imeanza kwa kupangwa kwa makundi ya michuano hiyo ambapo tukio la upangwaji wa makundi haya umefanyika kwenye jiji la Monaco, Ufaransa na mpango wote ndio umekua hivi.

Kundi A

Atletico Madrid
Juventus
Olympiakos
Malmo

Kundi B

Real Madrid
Basel
LIVERPOOL
Ludogorets

Kundi C

Benfica
Zenit St Petersburg
Bayer Leverkusen
Monaco

Kundi D

ARSENAL
Borussia Dortmund
Galatasaray
Anderlecht

Kundi E

Bayern Munich
MANCHESTER CITY
CSKA Moscow
Roma

Kundi F

Barcelona
Paris St-Germain
Ajax
Apoel Nicosia

Kundi G

CHELSEA
Schalke
Sporting Lisbon
Maribor

Kundi H

Porto
Shakhtar Donetsk
Athletic Bilbao
Bate Borisov

 BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

Nani kati ya Ronaldo, Neur au Ribery kachukua tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya? jibu liko hapa

Katika upangaji wa makundi na ratiba ya ligi ya mabingwa ulaya pia amechaguliwa mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa ulaya ambapo Cristiano Ronaldo, Manuel Neur na Arjen Robben walikuwa wakiwania tuzo hiyo ambayo mwaka jana ilichukuliwa na Frank Ribery wa Bayern Munich. Taarifa ikufikie kwamba mshindi wa mwaka huu ni Cristiano Ronaldo ambaye pia ni mwanasoka bora wa dunia ambapo kwenye hii amewashinda Robben na Neur kwa kura zilizopigwa na waandishi wa habari na tayari baada ya kutangazwa, amekabidhiwa tuzo yake muda mfupi uliopita jijini Monaco.

Kujiunga nasi  BOFYA HAPA  


Posted via Blogaway

PICHA ZA NJEMBA ILIYOBAMBWA IKIMGEGEDA MWANAFUNZI WA SEKONDARI....NAKUTOA PESA ILI MAMBO YAISHE

Picha zingine Bofya hapa

KUHUSU OKWI, HANS POPPE AIBUKA AWAPIGA DONGO ZITO YANGA

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema walichokifanya Yanga, ndicho kinachowarudia. Hans Poppe amerusha dongo nilo Jangwani ikiwa ni kuonyesha kwamba Yanga walimsajili Okwi wakati Simba ikiwa inaidai Etoile du Sahel dola 300,000. “Lazima wajue unapomtendea mwenzako, kesho yake kinarudi kwako,” alisema Hans Poppe ambaye ndiye injini ya usajili ya Simba. Awali Hans Poppe alieleza kuwa Okwi ameomba kurudi Simba na wao wamempokea kwa mikono miwili. “Tumempokea baada kuipokea barua yake na kuijadili, kwa kuwa Yanga wamemuacha na hata FIfa inasisitiza wachezaji kupata nafasi ya kucheza ili kuepusha kuua vipaji vyao, tumeamua kuwa naye,” alisema Hans Poppe.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

Thursday, August 28, 2014

RONALDO AMPIGA BAO ROBBEN, AWA MCHEZAJI BORA WA ULAYA

Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mchezaji bora wa Ulaya. Ronaldo aliyeisaidia Real Madrid ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wachezaji wawili wa Real Madrid, Arjen Robben na Manuel Neur.

Posted via Blogaway

SIMBA YAMRUDISHIA OKWI JEZI NAMBA 25, KESHO ANAPAA KWENDA ZANZIBAR

Baada ya kumpokea kwa mikono miwili, Simba imeamua kumrudishia Emmanuel Okwi jezi yake namba 25. Kabla ya kuondoka kwenda Etoile du Sahel alipouzwa 'bure' na Simba chini ya Ismail Aden Rage, Okwi alikuwa akitumia jezi hiyo. Yanga pia walimpa jezi hiyo, lakini leo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha kuwa Simba imempa Okwi namna 25. Baada ya kupokea namba hiyo, Okwi kesho anapaa Zanzibar kuungana na wenzake ambao wako kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara.

Habari zingine BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

SIMBA YAMRUDISHIA OKWI JEZI NAMBA 25, KESHO ANAPAA KWENDA ZANZIBAR

Baada ya kumpokea kwa mikono miwili, Simba imeamua kumrudishia Emmanuel Okwi jezi yake namba 25. Kabla ya kuondoka kwenda Etoile du Sahel alipouzwa 'bure' na Simba chini ya Ismail Aden Rage, Okwi alikuwa akitumia jezi hiyo. Yanga pia walimpa jezi hiyo, lakini leo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha kuwa Simba imempa Okwi namna 25. Baada ya kupokea namba hiyo, Okwi kesho anapaa Zanzibar kuungana na wenzake ambao wako kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara.

Habari zingine BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

SIMBA YAMRUDISHIA OKWI JEZI NAMBA 25, KESHO ANAPAA KWENDA ZANZIBAR

Baada ya kumpokea kwa mikono miwili, Simba imeamua kumrudishia Emmanuel Okwi jezi yake namba 25. Kabla ya kuondoka kwenda Etoile du Sahel alipouzwa 'bure' na Simba chini ya Ismail Aden Rage, Okwi alikuwa akitumia jezi hiyo. Yanga pia walimpa jezi hiyo, lakini leo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha kuwa Simba imempa Okwi namna 25. Baada ya kupokea namba hiyo, Okwi kesho anapaa Zanzibar kuungana na wenzake ambao wako kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara.

Habari zingine BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

SIMBA YAMRUDISHIA OKWI JEZI NAMBA 25, KESHO ANAPAA KWENDA ZANZIBAR

Baada ya kumpokea kwa mikono miwili, Simba imeamua kumrudishia Emmanuel Okwi jezi yake namba 25. Kabla ya kuondoka kwenda Etoile du Sahel alipouzwa 'bure' na Simba chini ya Ismail Aden Rage, Okwi alikuwa akitumia jezi hiyo. Yanga pia walimpa jezi hiyo, lakini leo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha kuwa Simba imempa Okwi namna 25. Baada ya kupokea namba hiyo, Okwi kesho anapaa Zanzibar kuungana na wenzake ambao wako kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara.

Habari zingine BOFYA HAPA 


Posted via Blogaway

TFF YAIBEBA YANGA KWA ‘ JAJA’

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam, Shirikisho la soka nchini, TFF limesogeza mbele muda wa usajili kwa klabu za ligi kuu na ligi daraja la kwanza kwa masaa 48 zaidi, Siku mbili kwa wachezaji wa ndani na wiki moja zaidi kwa usajili wa wachezaji wa kigeni kutoka nje ya nchini. Uamuzi huo umefikiwa baada ya klabu zote 14 za ligi kuu na 15 za ligi daraja la kwanza kushindwa kukamilisha taratibu za uhamisho wa Kieloktroniki. Ni timu moja tu iliyoweza kukamilisha usaajili wake siku ya jana ambayo ilikuwa ni ya mwisho baada ya mara mbili kuongezwa kwa muda. Yanga SC wameshindwa kupata hati ya uhamisho wa kimataifa ( ITC) ya mshambulizi, Geilson Santos ‘ Jaja’ na kuna uwezekano mkubwa wa mchezaji huyo kutoka Brazil akaondolewa kat ika timu hiyo. Katikati ya mwaka 2010 timu hiyo ilishindwa kukamilisha taratibu za kumuhamisha mshambulizi raia wa Ghana, Keneth Asamoah aliyekuwa akichezea klabu ya FK Jagodina ya Serbia. Jaja anaweza kutemwa na kuwapisha Waganda, Hamis Kizza na Emmanuel Okwi kuungana na wachezaji wengine wa kimataifa, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Andry Coutinho. Jina la mchezaji halipo katika orodha ya wachezaji wa Yanga na hakuna maombi yoyote ambayo uongozi wa Yanga umewasilisha kwa shirikisho la soka nchini, TFF hadi kufikia siku ya jana. Kama mshambulizi huyo atakwama kusajiliwa kama ilivyokuwa kwa Asamoah huku akiwa na mkataba wa miaka miwili uongozi hautakwepa lawama hivyo wanatakiwa kufanya kila wawezalo na si kujiaminisha kupata msaada wa muda mrefu kutoka kwa Okwi, na Kizza. Afadhali kwa Kizza yeye ni mchezaji wa Yanga hasa ila Okwi ataendelea kuwasumbua Yanga. Uongozi wa Yanga unasema kuwa kumekuwa na tatizo la mawasiliano kati yao na Shirikisho la soka la Brazil, CBF, ila hawajafanya jitihada za kupeleka maombi hayo rasmi kwa TFF ambao watafanya mawasiliano na wenzao wa Brazil ili kuhakikisha mchezaji huyo anasajiliwa na kukamilisha taratibu zote. Itakuwa ni sawa na kukosa umakini kwa viongozi wa Yanga kwa kuwa wamekuwa wakifahamu, Jaja ni mchezaji wao mpya tangu mwezi uliopita. Mfumo wa TMS umekuwa ukiwasumbua viongozi wa klabu za Tanzania lakini maombi ya uhamisho wa wachezaji yanayofanywa kutumia mfumo huo hufanyika haraka. ‘ SaSA Yanga wamepata muda zaidi wa kufikiria kwa umakini ni mchezaji gani wa kigeni anayetakiwa kuachwa kati ya washambuliaji hao watatu. Kulikuwa na uwezekano mkubwa wa Jaja kuachwa, lakini matumaini ya Mbrazil huyo kucheza Tanzania yamerejea baada ya muda zaidi wa usajili kuongezwa.

Posted via Blogaway

KWA MARA YA KWANZA RONALDO AFUNGUKA KUHUSIANA NA URAFIKI WAKE NA MESSI

Kwa mara ya kwanza mshambuliaji nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefunguka kuhusiana na uhusiano wake na Lionel Messi na kusema anamheshimu hasa juhudi zake za kutaka mafanikio kama mchezaji pamoja na klabu yake ya Barcelona.

SWALI. Baada ya miaka mitano sasa na Real Madrid, umechoka kulinganishwa na Messi au umejifunza jambo?
JIBU. Ni sehemu ya kazi tu kama vile ambavyo kwenye mashindano ya langalanga (Formula 1), watu wanafananisha kati ya Ferrari na Mercedes. Haya yamekuwa maisha yangu hapa Madrid, lakini najua mambo yanabadilika na hata nilipokwenda Manchester kulikuwa na mengine tofauti.
SWALI. Kumekuwa na taarifa kwamba uhusiano wako wewe na Messi nje ya mpira umekuwa si mzuri?
JIBU. Si kweli, sisi ni marafiki, ni marafiki kazini. Binafsi sina rafiki nje ya mpira, pia sina urafiki na Messi nje ya mpira. Anajitahidi kufanya makubwa katika klabu yake na timu ya taifa, sawa ninavyofanya mimi. Tunachezea timu zenye upinzani mkubwa na huenda ushindani huo unafanya watu wayakuze hayo mambo.
SWALI. Unafikiri wewe na Messi, siku moja mtakutana, mkae na kuanza kujadili haya yaliyotokea huku mkiangua vicheko kwa furaha?


JIBU. Nafikiri inawezekana, soka ni mchezo wa furaha, soka ni kitu kikubwa na unaweza kuufananisha na saa. Ndiyo maana nashauri kuwaangalia wapinzani kwa jicho la mafanikio na kukubali wanachofanya kwa vile ni kitu kizuri.


Posted via Blogaway

USAJILI LIGI KUU BARA WASOGEZWA MBELE TENA, SABABU YENYEWE NI ‘KICHEKESHO KWELI KWELI’

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM DIRISHA la usajili la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa wachezaji wazalendo limesogezwa mbele kwa Saa 48 kuanzia jana, kutokana na timu kushindwa kukamilisha usajili katika muda husika jana. Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, sababu za kusogeza mbele ni klabu zote za Ligi Kuu kushindwa kukamilisha usajili jana. “Nadhani wameshindwa kuutumia huu mfumo wetu mpya wa elektroniki, sasa tumewapa Saa 48 zaidi warekebishe, zikiisha hizo, hapo hakuna nafasi tena, tunasonga mbele,”amesema Mwesigwa. Amesema kwamba hadi muda wa kufunga usajili jana Saa 6:00 usiku, ni timu moja tu, Kimondo FC ya Daraja la Kwanza ndiyo iliyokuwa imefanikiwa kukamilisha usajili wake katika mfumo huo. “Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Kimondo kwa kumudu kuutumia mfumo huu na kuwasilisha usajili wao ndani ya muda,”amesema. Aidha, Mwesigwa amesema kwamba dirisha la usajili kwa wachezaji wa kigeni litafungwa Septemba 6, mwaka huu. “Hili dirisha la wachezaji wa kigeni likifungwa, hakuna nyongeza ya muda tena, kwa kuwa hili lipo katika mfumo wa kimataifa chini ya FIFA, likifungwa, limefungwa dunia nzima, hivyo nawasihi viongozi wa klabu wahakikishe hawafanyi makoasa,”amesema.

Posted via Blogaway

Mtoto wa miaka 9 alivyomuua Mwalimu akimfundisha kutumia bunduki.

Pale ambapo kwanza unaweza kushtushwa na umri mdogo wa mtoto mwenyewe aliekua anafundishwa kufyetua risasi kwenye bunduki, hii imetokea Arizona nchini Marekani ambapo mtoto wa miaka 9 ndio kichwa cha habari kwenye mafunzo ya kutumia submachine gun iliyotengenezwa Israel. Mtoto huyu wa kike anaetokea New York alikua kwenye mapumziko na matembezi kama mtalii kwenye mji wa Arizona ambako pia ndio alichukua time yake ya ziada kujifunza kutumia bunduki lakini kwa bahati mbaya risasi ikafyetuka na kumjeruhi mwalimu wake aitwae Charles Vacca mwenye umri wa miaka 39 ambae alifariki baadae hospitalini. Wakati tukio linatokea mtoto huyu alikua na wazazi wake ambapo tovuti ya bullets and burgers imesema watoto kati ya miaka 8 na 17 wanaweza kufyetua risasi kama iwapo tu watakua chini ya uangalizi wa Mzazi au Mwalimu. Hii sio mara ya kwanza kwa tukio kama hili, ilishawahi kutokea mwaka 2008 ambapo mtoto wa miaka 8 alijiua kwa bahati mbaya kwa risasi kwenye onyesho la bunduki hukohuko Marekani.

Posted via Blogaway

Namna utapeli wa kutumia majina ya watu unavyotumika,msikilize Godzila feki akimtapeli mtu.

Mara chache zinapotoka stori za mtu kutaperiwa na mtu akidhani labda ni star fulani alikua akiwasiliana nae kiasi hadi cha kumuamini na kumtumia pesa lakini anapotuma pesa anashangaa kuona mtu huyo anavyobadilika. Watu wa namna hii wanapopata wanachokitaka huwa wanazima simu au hawapokei kabisa,sasa kwenye meza ya Soudy Brown kuna msanii mchanga kataperiwa na Godzilla ‘feki’ kwa kumtaka amtumie kiasi fulani cha pesa kisha wafanye colabo. Bonyeza play kusikiliza.

Source millardayo


Posted via Blogaway