Friday, August 29, 2014

Nani kati ya Ronaldo, Neur au Ribery kachukua tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya? jibu liko hapa

Katika upangaji wa makundi na ratiba ya ligi ya mabingwa ulaya pia amechaguliwa mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa ulaya ambapo Cristiano Ronaldo, Manuel Neur na Arjen Robben walikuwa wakiwania tuzo hiyo ambayo mwaka jana ilichukuliwa na Frank Ribery wa Bayern Munich. Taarifa ikufikie kwamba mshindi wa mwaka huu ni Cristiano Ronaldo ambaye pia ni mwanasoka bora wa dunia ambapo kwenye hii amewashinda Robben na Neur kwa kura zilizopigwa na waandishi wa habari na tayari baada ya kutangazwa, amekabidhiwa tuzo yake muda mfupi uliopita jijini Monaco.

Kujiunga nasi  BOFYA HAPA  


Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment