 |
| Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Simba, Zacharia
Hans Poppe amesema
walichokifanya Yanga,
ndicho kinachowarudia.
Hans Poppe amerusha dongo
nilo Jangwani ikiwa ni
kuonyesha kwamba Yanga
walimsajili Okwi wakati
Simba ikiwa inaidai Etoile
du Sahel dola 300,000.
“Lazima wajue unapomtendea
mwenzako, kesho yake
kinarudi kwako,” alisema
Hans Poppe ambaye ndiye
injini ya usajili ya Simba.
Awali Hans Poppe alieleza
kuwa Okwi ameomba kurudi
Simba na wao wamempokea kwa
mikono miwili.
“Tumempokea baada kuipokea
barua yake na kuijadili,
kwa kuwa Yanga wamemuacha
na hata FIfa inasisitiza
wachezaji kupata nafasi ya
kucheza ili kuepusha kuua
vipaji vyao, tumeamua kuwa
naye,” alisema Hans Poppe. |
ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBOFYA HAPA
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment