Tuesday, August 26, 2014

SOMA KISA CHA BALOTELLI KUENDELEA KUITUMIA JEZI NAMBA 45 HATA BAADA YA KUTUA LIVERPOOL

mshambuliaji Mario Balotelli ameamua kuchukua jezi kipenzi chake namba 45 ambayo ataitumia akiwa na Liverpool. Balotelli amekuwa akiitumia namba 45 tokea akiwa Inter Milan, baadaye akajiunga na Man City na hata alipokwenda AC Milan. Jezi hiyo anaamini ndiyo yenye bahati kwa kuwa wakati akiwa kinda anaichezea Inter Milan, alifunga mabao manne katika mechi nne. Katika kikosi cha AC Milan, vijana waliochaguliwa kuchezea timu ya wakubwa huvaa jezi kuanzia namba 36 hadi 45. Kingine Balotelli ambaye leo alishuhudia mechi kati ya Man City dhidi ya timu yake mpya ya Liverpool akiwa jukwaani Ambapo man city ilishinda 3-1, a amekuwa akitania 4+5=9 akiwa ana maana anavaa jezi namba 9, kijanja.

ANGEL DI MARIA AWASILI MAN UNITED KUKAMILISHA USAJILI WA REKODI ENGLAND NA MSHAHARA MNONO

KIUNGO Angel di Maria amewasili viwanja vya mazoezi vya Manchester United, Carrington kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wa Pauni 60 kutoka Real Madrid ya Hispania. Nyota huyo wa Argentina aliyeng'ara kwenye Kombe a Dunia amewasili England huku viongozi wa Old Trafford wakiendelea na mazungumzo na Real Madrid juu ya kukamilisha uhamisho wa dau la rekodi Uingereza. Di Maria, mwenye umri wa miaka 26, anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake usiku huu ambao utamfanya alipwe Pauni 200,000 kwa wiki kwa zaidi ya miaka mitano, mshahara ambao pia utamfanya awe mchezaji wa pili kulipwa zaidi katika klabu hiyo baada ya Nahodha, Wayne Rooney. Amenaswa: Di Maria akiwa kiri nyuma kushoto kwenye gari kuelekea viwanja vya mazoezi vya United Di Maria anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake usiku huu Uhamisho wote utaigharimu United zaidi ya Pauni Milioni 90 na mchezaji huyo ataingia moja kwa moja katika kikosi kilichojeruhiwa cha Louis van Gaal kwa ajili ya mchezo dhidi ya timu iliyopanda Ligi Kuu, Burnley.

Epl: Matokeo na wafungaji wa mechi ya Liverpool vs Man City haya hapa

MABINGWA wa Ligi Kuu ya England, Manchester City wamewachapa mabao 3-1 wapinzani wao katika mbio za taji hilo msimu uliopita, Liverpool usiku huu Uwanja wa Etihad mjini Manchester. Stevan Jovetic alifunga mabao mawili moja kila kipindi la kwanza dakika ya 41 na pili dakika ya 55 kabla ya Edin Dzeko kuingia na kufunga la tatu katika mpira wa kwanza aliogusa dakika ya 68. Dzeko alifunga bao hilo kabla hata Sergio Aguero aliuemposha hajafika kwenye benchi na Liverpool wakapata bao la kufutia machozi dakika ya 83 kupitia kwa Lambert. Mshambuliaji mpya wa Liverpool, Mario Balotelli alikuwa jukwaani akiishuhudia timu yake ya zamani ikishinda. Kikosi cha Man City kilikuwa: Hart, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Nasri, Toure, Fernando, Silva/Jesus Navas DK65, Jovetic/ Fernandinho DK80 na Dzeko/Aguero dk69. Liverpool: Mignolet, Johnson, Skrtel, Lovren, Moreno, Henderson, Gerrard, Allen/Can dk75, Sterling/Lambert dk79, Sturridge na Coutinho/ Markovic dk60.

Monday, August 25, 2014

BALOTELLI ASAINI MIAKA MITATU LIVERPOOL, MSHAHARA MNONO NA JEZI NAMBA 45, AANZA KAZI LEO DHIDI YA MAN CITY

MSHAMBULIAJI Mario Balotelli amekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 16 kutoka AC Milan kutua Liverpool kwa Mkataba wa miaka mitatau. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 aliwasili Melwood leo mchana kukamilisha uhamisho wake kabla ya kwenda kufanya mazoezi maalum na mkuu wa idara ya kuwaweka fiti wachezaji, Ryland Morgans. Nyota huyo wa zamani wa Manchester City atakuwa akilipwa mshahara wa Pauni 125,000 kwa wiki Anfield na atakuwepo kwenye mchezo dhidi ya timu yake hiyo ya zamani usiku wa leo. Pamoja na kusaini mkataba wa miaka mitatu, Balotelli anaweza kuongezewa mwaka mmoja kwa mujibu wa kandarasi hiyo.

Wachezaji bora wa Dunia wanne wacheza Tanzania wajue hapa

TANZANIA haijawahi kushiriki fainali za Kombe la Dunia hata kwa mwaliko maalumu katika historia ya miaka 34 ya michuano hiyo, lakini imeweka historia ya kuwaleta nchini wachezaji wanne waliowahi kutwaa tuzo za Mchezaji Bora wa Dunia wa Fifa. Juzi Jumamosi kikosi cha wakongwe wa Real Madrid kilicheza na wakongwe wa Tanzania na kuwafunga mabao 3-1, lakini ujio huo uliandika historia kwa Tanzania kwa kuwaweka uwanjani wachezaji Luis Figo na Fabio Cannavaro waliowahi kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia. Wachezaji wengine waliowahi kuja Tanzania wenye rekodi hiyo kubwa duniani ni Ricardo Kaka wa Brazili na Geogre Weah wa Liberia. Figo ambaye licha ya kustaafu soka miaka mingi iliyopita, juzi alicheza kwa kiwango cha juu na kuwa kivutio kwa Watanzania waliiofurika uwanjani. Mreno huyo alinyakua tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia mwaka 2000. Cannavaro alinyakuwa tuzo hiyo mwaka 2006 wakati Kaka alinyakua mwaka 2007. Mliberia Weah ambaye ndiye Mwafrika wa kwanza kupata heshima hiyo, alinyakua tuzo hiyo maarufu kwa jina la Ballon d’Or mwaka 1995. Weah alikuja Tanzania mwaka 1994 akiwa na kikosi cha Liberia. Kaka alikwemo kwenye kikosi cha Brazili kilichoifunga Tanzania mabao 5-1 mwaka 2010. Kati ya wana tuzo hao, ni Weah na Kaka pekee ndiyo waliokuja nchini wakiwa bado wanacheza soka la kulipwa na la kimataifa. Ujio wa Figo na Cannavaro umekuja wakiwa tayari wametundika daluga (wamestaafu). Credit mwanaspoti

BAADA YA KIPIGO KIMOJA NA DROO MOJA KOCHA VAN GAAL AFUNGUKA MAZITO

KOCHA Mkuu wa Manchester United, Louis van Gaal amesema itakuwa ni muujiza mkubwa kwa timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu. Mdachi huyo ameilinganisha United ya sasa na Bayern Munich ya mwaka 2009 wakati alipokuwa akiinoa timu hiyo iliyokuwa na kikosi kilichokuwa na kasoro nyingi. Hata hivyo, Van Gaal akamaliza ligi msimu huo kwa kunyakua Ubingwa wa Bundesliga, kitu ambacho haoni kama kitaweza kujirudia kwa sasa akiwa na cha United. Wasiwasi wa Van Gaal umeibuka baada ya wiki iliyopita kuchapwa na Swansea City nyumbani Old Trafford katika mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu England na kikosi chake jana Jumapili kilitarajia kumenyana na Sunderland kwenye ligi hiyo. Alipoulizwa kama aanze kutazamwa kiwango chake kwenye msimu wa kwanza au wa pili klabuni hapo, Van Gaal alijibu: “Siku zote hiyo ndiyo inakuwa kesi kubwa. Kitu ambacho kimenipa uzoefu ni kwamba nilikuwa bingwa Barcelona na Bayern, hivyo inawekana ila ni ngumu sana. “Nilipokwenda Bayern Munich kikosi kilikuwa hovyo. Kitu ambacho tulikifanya hadi mwisho wa msimu kilikuwa ni muujiza. Hapa Man United pia kikosi hakijatengemaa. Kuna namba 9 watano na namba 10 sita. Hatuna mabeki.” Alipoulizwa kama itakuwa muujiza kwa United kutwaa taji la Ligi Kuu England msimu huu, Van Gaal alisema: “Ndiyo, nadhani ni hivyo. Sawa siku zote inawezekana, lakini itakuwa ngumu sana.” credit mwanaspoti

Maximo aizuga vibaya timu ya Simba

YANGA walikuwa kambini mjini Pemba lakini juzi Jumamosi wakatua Unguja na jana Jumapili wakakipiga na Shanghani mchana kwenye mechi ya kirafiki katika Uwanja wa Amani. Ujio wa Yanga Unguja kiufundi ni faida pia kwa Simba ambayo imeweka kambi yake eneo la Mbweni ikifanya mazoezi Uwanja wa Chuoni. Yanga itapata nafasi ya kuisoma Simba kwenye mechi zake za kirafiki mpaka mazoezini na Simba nao hivyohivyo. Lakini Kocha Marcio Maximo ameshitukia hali hiyo na kutamka kwamba anafanya mambo yake kwa akili sana na hakuna timu yoyote itaweza kusoma mbinu zake kwani hatazitumia hadharani kwa muda wote atakaokuwa Unguja. Kocha huyo ambaye timu yake ina wachezaji wawili raia wa Brazil, alisema kwamba anafanya mambo kwa umakini sana na hata mbinu zake za maangamizi atawapa wachezaji katika mazingira ya siri. Anamaanisha kwamba hata Simba au Azam wakiangalia mechi yake yoyote ya kirafiki kwa sasa haitawasaidia. “Unajua tunakwenda kwenye ushindani kucheza ligi, kila mtu anataka kujua una mbinu gani hivyo suala hilo niko makini nalo sana, sitaki watu wagundue mbinu zangu, ”alisema Maximo ambaye bado hajatangaza kumuacha mchezaji wake ghali wa kigeni, Mganda Emmanuel Okwi licha ya kuchelewa. Keshokutwa Jumatano, Yanga itacheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Shangani na baada ya hapo, watarudi Dar es Salaam kucheza mechi mbili ngumu. Yanga awali ilicheza na Chipukizi na Shanghani. Katika hatua nyingine, Mbrazili Andrey Coutinho amewavutia zaidi mashabiki wa Pemba. Kocha Mkuu wa Chipukizi ya Pemba iliyofungwa na Yanga bao 1-0, amesema yeye ni Coutinho tu kwenye kikosi hicho na kilichomvutia zaidi ni namna anavyotumia akili kupenya sehemu ngumu. Coutinho anachezesha timu vizuri, pasi zake zenye macho zilimfanya Mbrazili mwenzake, Genilson Santos Santana ‘Jaja’ ang’ae kwenye mechi yao na Chipukizi ya Pemba. Mchezaji huyo mwenye mwili mdogo, ana kasi na alishirikiana vizuri na Mrisho Ngassa, Mnyarwanda Haruna Niyonzima katika kuchezesha timu. Kwenye Uwanja wa Gombani, kila alipokuwa akiunasa mpira zilisikika kelele za mashabiki zikimshangilia. Credit mwanaspoti

HII NDO TOFAUTI NA BAADHI YA WATU WANAVYO MCHUKULIA ….LULU

"Pepo ipo miguuni mwa mama yako....usifanye mchezo na mama. Hata wakifika followers wengi kama wa BeyoncĂ©. Mama ni mama. Haina ubishi wala usupa star. Nimefurahi kumkuta @officiallulumichael akiwa anampaka mama yake mafuta na kumvalisha viatu. Mwenyezi mungu akuongezee dogo. Kesho massage" ….by @glammadam INSTAGRAM

New AUDIO | BenPol - Twapendana | Download hapA

<<<<<<<<< BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD >>>>>>>>>

PAKA JEUSI LAKATIZA UWANJANI CAMP NOU, BARCA YAUA 3-0 LA LIGA

BARCELONA imeanza vyema La Liga kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Elche Uwanja wa Camp Npu usiku wa kuamkia leo. Katika mchezo huo, kiungo wa Barca Javier Mascherano alitolewa nje kwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza, kocha mpya Luis Enrique akiiongoza timu kwa mara ya kwanza, alionyesha mwanzo mzuri. Lionel Messi aliifungia Barca bao la kwanza baada ya kuwazidi ujanja mabeki sita Elche, kabla ya kinda Munir El Hadaddi kufunga la pili, mabao yote kipindi cha kwanza. Nyota wa Argentina, Lionel Messi alifunga bao lake la pili na la tatu la kuhitimisha ushindi wa Barca baada ya jitihada binafsi kipindi cha pili. Paka mweusi alikatiza Uwanja wa Camp Nou mwanzoni tu mwa mchezo na kusababisha mechi isimame kwa muda ili aondoke.