YANGA walikuwa kambini mjini
Pemba lakini juzi Jumamosi
wakatua Unguja na jana Jumapili
wakakipiga na Shanghani mchana
kwenye mechi ya kirafiki katika
Uwanja wa Amani.
Ujio wa Yanga Unguja kiufundi ni
faida pia kwa Simba ambayo
imeweka kambi yake eneo la
Mbweni ikifanya mazoezi Uwanja
wa Chuoni.
Yanga itapata nafasi ya kuisoma
Simba kwenye mechi zake za
kirafiki mpaka mazoezini na Simba
nao hivyohivyo.
Lakini Kocha Marcio Maximo
ameshitukia hali hiyo na kutamka
kwamba anafanya mambo yake
kwa akili sana na hakuna timu
yoyote itaweza kusoma mbinu
zake kwani hatazitumia hadharani
kwa muda wote atakaokuwa
Unguja.
Kocha huyo ambaye timu yake ina
wachezaji wawili raia wa Brazil,
alisema kwamba anafanya mambo
kwa umakini sana na hata mbinu
zake za maangamizi atawapa
wachezaji katika mazingira ya siri.
Anamaanisha kwamba hata Simba
au Azam wakiangalia mechi yake
yoyote ya kirafiki kwa sasa
haitawasaidia.
“Unajua tunakwenda kwenye
ushindani kucheza ligi, kila mtu
anataka kujua una mbinu gani
hivyo suala hilo niko makini nalo
sana, sitaki watu wagundue mbinu
zangu, ”alisema Maximo ambaye
bado hajatangaza kumuacha
mchezaji wake ghali wa kigeni,
Mganda Emmanuel Okwi licha ya
kuchelewa.
Keshokutwa Jumatano, Yanga
itacheza mechi nyingine ya kirafiki
dhidi ya Shangani na baada ya
hapo, watarudi Dar es Salaam
kucheza mechi mbili ngumu.
Yanga awali ilicheza na Chipukizi
na Shanghani.
Katika hatua nyingine, Mbrazili
Andrey Coutinho amewavutia zaidi
mashabiki wa Pemba.
Kocha Mkuu wa Chipukizi ya
Pemba iliyofungwa na Yanga bao
1-0, amesema yeye ni Coutinho tu
kwenye kikosi hicho na
kilichomvutia zaidi ni namna
anavyotumia akili kupenya sehemu
ngumu.
Coutinho anachezesha timu vizuri,
pasi zake zenye macho zilimfanya
Mbrazili mwenzake, Genilson
Santos Santana ‘Jaja’ ang’ae
kwenye mechi yao na Chipukizi ya
Pemba.
Mchezaji huyo mwenye mwili
mdogo, ana kasi na alishirikiana
vizuri na Mrisho Ngassa,
Mnyarwanda Haruna Niyonzima
katika kuchezesha timu.
Kwenye Uwanja wa Gombani, kila
alipokuwa akiunasa mpira zilisikika
kelele za mashabiki zikimshangilia. Credit mwanaspoti |
0 comments:
Post a Comment