KIUNGO Angel di Maria amewasili viwanja vya
mazoezi vya Manchester United, Carrington
kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wa Pauni 60
kutoka Real Madrid ya Hispania.
Nyota huyo wa Argentina aliyeng'ara kwenye
Kombe a Dunia amewasili England huku
viongozi wa Old Trafford wakiendelea na
mazungumzo na Real Madrid juu ya
kukamilisha uhamisho wa dau la rekodi
Uingereza.
Di Maria, mwenye umri wa miaka 26,
anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake usiku
huu ambao utamfanya alipwe Pauni 200,000
kwa wiki kwa zaidi ya miaka mitano, mshahara
ambao pia utamfanya awe mchezaji wa pili
kulipwa zaidi katika klabu hiyo baada ya
Nahodha, Wayne Rooney.
Amenaswa: Di Maria akiwa kiri nyuma kushoto
kwenye gari kuelekea viwanja vya mazoezi vya
United
Di Maria anatarajiwa kukamilisha uhamisho
wake usiku huu
Uhamisho wote utaigharimu United zaidi ya
Pauni Milioni 90 na mchezaji huyo ataingia
moja kwa moja katika kikosi kilichojeruhiwa
cha Louis van Gaal kwa ajili ya mchezo dhidi
ya timu iliyopanda Ligi Kuu, Burnley. |
0 comments:
Post a Comment