Monday, August 25, 2014

Wachezaji bora wa Dunia wanne wacheza Tanzania wajue hapa

TANZANIA haijawahi kushiriki fainali za Kombe la Dunia hata kwa mwaliko maalumu katika historia ya miaka 34 ya michuano hiyo, lakini imeweka historia ya kuwaleta nchini wachezaji wanne waliowahi kutwaa tuzo za Mchezaji Bora wa Dunia wa Fifa. Juzi Jumamosi kikosi cha wakongwe wa Real Madrid kilicheza na wakongwe wa Tanzania na kuwafunga mabao 3-1, lakini ujio huo uliandika historia kwa Tanzania kwa kuwaweka uwanjani wachezaji Luis Figo na Fabio Cannavaro waliowahi kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia. Wachezaji wengine waliowahi kuja Tanzania wenye rekodi hiyo kubwa duniani ni Ricardo Kaka wa Brazili na Geogre Weah wa Liberia. Figo ambaye licha ya kustaafu soka miaka mingi iliyopita, juzi alicheza kwa kiwango cha juu na kuwa kivutio kwa Watanzania waliiofurika uwanjani. Mreno huyo alinyakua tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia mwaka 2000. Cannavaro alinyakuwa tuzo hiyo mwaka 2006 wakati Kaka alinyakua mwaka 2007. Mliberia Weah ambaye ndiye Mwafrika wa kwanza kupata heshima hiyo, alinyakua tuzo hiyo maarufu kwa jina la Ballon d’Or mwaka 1995. Weah alikuja Tanzania mwaka 1994 akiwa na kikosi cha Liberia. Kaka alikwemo kwenye kikosi cha Brazili kilichoifunga Tanzania mabao 5-1 mwaka 2010. Kati ya wana tuzo hao, ni Weah na Kaka pekee ndiyo waliokuja nchini wakiwa bado wanacheza soka la kulipwa na la kimataifa. Ujio wa Figo na Cannavaro umekuja wakiwa tayari wametundika daluga (wamestaafu). Credit mwanaspoti

0 comments:

Post a Comment