Thursday, August 21, 2014

WACHEZAJI WA MAN CITY WAZIDI KUJITUNDIKA VITANZI,HUYU NAYE AJITUNDIKA KITANZI CHA MIAKA MINNE

MSHAMBULIAJI Edin Dzeko amesaini Mkataba wa miaka minne na mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester City. Mwanasioka huyo wa kimataifa wa Bosnia ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter juu ya kusaini kwake mkataba mpya akisema: "Furaha na kujivuniaa kusaini mkataba wangu mpya na Manchester City. Nipo hapa ambako ni kwangu. Nimerefusha hadi 2018,". Mpachika mabao huyo amefunga mara 65 katika mechi 156 alizoichezea klabu hiyo tangu ajiunge nayo kutoka Wolfsburg mwaka 2011. Na mdadisiblog/,festosaimon

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZA HAPA 

SIMBA NA YANGA OKTOBA 12 NA FEBAURI 8, MECHI ZAO NA AZAM FC…RATIBA KAMILI LIGI NZIMA HII HAPA

WATANI wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba SC na Yanga watakutana Oktoba 12, mwaka huu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mzunguko wa kwanza, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ladha ya Ligi Kuu ni mechi baina ya miamba hiyo miwili nchini- na kidogo mechi zinazozihusisha timu hizo na mabingwa watetezi, Azam FC, nazo pia huwa za kukata na shoka. Msimu uliopita, mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya 3-3, Simba wakitoka nyuma kwa 3-0 hadi mapumziko na marudiano, Yanga walisawazisha dakika za lala salama kupata sare ya 1-1. Lakini Simba SC ilijichukulia ubabe wa jumla wa msimu dhidi ya watani wao, baada ya kuwafunga Yanga SC 3-1 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe Desemba mwaka jana Uwanja wa Taifa. Mzunguko wa pili, timu hizo zitakutana Februari 8, mwakani, mchezo wa kwanza Yanga mwenyeji, wa pili Simba mwenyeji. Azam FC na Simba zitakutana Januari 1, mwaka 2015 wakati marudiano yatakuwa ni Aprili 12, mwaka huo. Yanga itamenyana na Azam FC Novemba 9, mwaka huu wakati mchezo wa marudiano utapangiwa siku. Ikumbukwe Septemba 13, Yanga na Azam FC zitafungua pazia la Ligi Kuu kwa mchezo wa Ngao ya Jamii Uwanja wa Taifa.

Wednesday, August 20, 2014

RATIBA LIGI KUU YATOKA; YANGA SC KUANZA NA MTIBWA SUGAR MOROGORO, AZAM NA POLISI MORO, SIMBA NA COASTAL DAR

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC wataanza na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu, wakati Yanga SC waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro siku hiyo. Washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine, Mbeya Septemba 20 na washindi wa nne, Simba SC wataanza na Coastal Union ya Tanga Septemba 21, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani. ITAENDELEA:

FIFA YAIPIGA NYUNDO NZITO TIMU YA BARCELONA

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limepiga nyundo kwenye kidonda baada ya kuizua Barcelona kusajili hadi Januari 2016. Awali Barcelona ilikata rufaa kwa Fifa ikipinga adhabu hiyo, badala yake Fifa imetia msisitizo kuhusiana na adhabu hiyo. Sasa Barcelona itaendelea kusubiri kufanya usajili hadi mwaka keshokutwa!. Na mdadisiblog/festosaimon

CHID BENZ AMWAGA MACHOZI CLOUDS ALIVYOKUWA ANAELEZEA STORY YA DIAMOND KABLA HAJAKUWA STAR

Chidi Benz alitabiri mbele ya Diamond Platnumz (wakati bado underground) kuwa angekuja kuwa msanii mkubwa. Hata hivyo maneno muhimu ambayo rapper huyo alimwambia Diamond ni kuwa asije kunywa pombe wala kuvuta (unga/bangi) maishani mwake. Chidi ambaye Jumanne hii ameachia single yake mpya 'Mpaka Kuche' aliyowashirikisha Diamond na AY, alikuwa akihojiwa kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM. Katika kuashiria kuwa hiyo ilikuwa ni interview iliyogusa sehemu ya katikati kabisa ya moyo wake, Chidi alijikuta akibubujikwa na machozi. Chidi alikumbushia siku Diamond alipompigia simu kujitambulisha kwake kuwa ni msanii mchanga anayetaka kumshirikisha kwenye wimbo wake. Hata hivyo siku Diamond amefanikiwa kumpata Chidi hewani ilikuwa ni baada ya kujaribu kumtafuta kwa siku nyingi bila mafanikio na aliwahi kumweleza mama yake namna alivyo na hamu ya kumshirikisha rapper huyo aliyekuwa akimkubali. Baada ya kumpigia simu, Chidi anadai alimuambia Diamond aende kwao maghorofani Ilala wakazungumze vizuri. "Sasa nikamuona (Diamond) nikajua huyo dogo ndio yule niliwaambiaga watu kuwa ‘huyu dogo ana sura moja hivi imekaa.. sura yake lazima utaiongelea tu, lazima utasema kitu, namuona atakuja kuwa staa tu, simjui lakini the way alivyo, atakuja kuwa staa,” alikumbushia Chidi.

DIVA WA CLOUDS FM ATUBU KUMKOSEA MSANII CHID BENZ BAADA YA KUMCHAFUA HUKO INSTAGRAM!!!

Mwanadada mtangazaji wa Clouds FM, Loveness maarufu kama DIVA..jana kupitia ukurasa wake wa Instagram alikili kumkosea msanii wa Bongo flava, Chid Benz....kutokana na comment yake ya siku za hivi karibuni kuhusiana na issue ya Chid kumpiga Ray C... Soma hapa alichokiandika!!!

DUNGA AWATOSA ALVES, MARCELO, AITA KIKOSI CHAKE KUWAVAA COLOMBIA

Kocha wa Brazil, Dunga ametangaza kikosi chake kwa ajili ya ya mechi za kirafiki dhidi ya Colombia, mechi itakayopigwa Septemba 5 jijini Miami, na dhidi ya Ecuador Septemba 9 jijini New Jersey, Marekani. Kati ya wachezaji aliowaita ni Miranda wa Atlético de Madrid na Filipe Luís. Lakini Dunga akaamua kuwaacha mabeki Dani Alves wa Barcelona na Marcelo wa Real Madrid. Nahodha Thiago Silva anayekipiga PSG pia ni mgonjwa, hivyo pia amemuacha katika kikosi chake. Wachezaji waliocheza Kombe la Dunia 2014 ambao Dunga amewaita ni Jefferson, David Luiz, Maicon, Luiz Gustavo, Fernandinho, Ramires, Oscar, Hulk, Willian and Neymar.

HAYA NDO MTOKEO YA MECHI KATI YA REALMADRID VS ATLETICO SUPER CUP YA KWANZA BERNABEU

REAL Madrid imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Atletico Madrid katika mchezo wa kwanza wa Super Cup ya Hispania usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu. Msambuliaji Crisitiano Ronaldo alitolewa kipindi cha pili kumpisha mchezaji mpya, James Rodriguez, kabla ya Mcolombia huyo kuifungia bao la kuongoza Real dakika ya 81. Atletico Madrid ilikomboa bao hilo zikiwa zimesalia dakika tatu kupitia kwa Raul Garcia na sasa Real Madrid itakabiliwa na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano Uwanja wa Vicente Calderon. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Kroos, Alonso, Bale, Ronaldo/Rodriguez dk45 na Benzema. Atletico Madrid: Moya, Juanfran, Miranda, Godin, Siqueira, Mario, Gabi, Koke, Saul/ Griezmann dk56, Raul Garcia, Mandzukic

ORIJINO KOMEDI WAPATA PIGO JINGINE, MENEJA WAO AWAKIMBIA. SOMA HAPA

Kundi maarufu la vichekesho ambalo kwa sasa ni kama halipo, limepata pigo kubwa baada ya aliyekuwa meneja wao, mtangazaji nyota wa zamani wa televisheni, Christina Mosha maarufu kama Seven, kuwamwaga na hivyo kuachana nao. Akizungumza na gazeti hili juzikati, Seven alisema ameachana nao baada ya mkataba wake wa sasa kumzuia kufanya kazi na watu wengine zaidi ya walio chini ya mwajiri wake mpya. “Hivi sasa niko na Sony, wao wananizuia kufanya kazi na wasanii ambao hawako nao, hivyo baada ya mkataba wangu na wao kumalizika, nimeamua kuachana nao. Mimi ni mwakilishi wa Sony barani Afrika, ninashughulika na wasanii toka nchi tofauti za Afrika, kama Senegal, Kenya na kwingineko kasoro Afrika Kusini,” alisema.

COUTINHO AITWA BRAZIL MPYA BAADA YA KOCHA DUNGA KUBOMOA KIKOSI KILICHOVURUNDA KOMBE LA DUNIA

KOCHA mpya wa Brazil, Carlos Dunga amekibomoa kikosi cha timu hiyo kilichovurunda Kombe la Dunia kwa kuwatema wachezaji 13 na kuita wengine wapya. Philippe Coutinho ni miongoni mwa ingizo jipya la wachezaji baada ya Kombe la Dunia baada ya Dunga kuvutiwa na kazi yake akiichezea Liverpool, wakati Neymar aliyepona majeruhi yake yaliyomfanya akose mechi mbili za mwisho za Kombe la Dunia ameitwa pia. Kikois cha wachezaji 22 kimetajwa jana kwa ajili ya mechi mbili za kiradiki dhidi ya Colombia na Ecuador. Na mdadisiblog,/festosaimon