Wednesday, August 20, 2014

HAYA NDO MTOKEO YA MECHI KATI YA REALMADRID VS ATLETICO SUPER CUP YA KWANZA BERNABEU

REAL Madrid imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Atletico Madrid katika mchezo wa kwanza wa Super Cup ya Hispania usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu. Msambuliaji Crisitiano Ronaldo alitolewa kipindi cha pili kumpisha mchezaji mpya, James Rodriguez, kabla ya Mcolombia huyo kuifungia bao la kuongoza Real dakika ya 81. Atletico Madrid ilikomboa bao hilo zikiwa zimesalia dakika tatu kupitia kwa Raul Garcia na sasa Real Madrid itakabiliwa na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano Uwanja wa Vicente Calderon. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Kroos, Alonso, Bale, Ronaldo/Rodriguez dk45 na Benzema. Atletico Madrid: Moya, Juanfran, Miranda, Godin, Siqueira, Mario, Gabi, Koke, Saul/ Griezmann dk56, Raul Garcia, Mandzukic

0 comments:

Post a Comment