Friday, October 31, 2014

TORRES AFUNGUKA RASMI KUHUSU MOURINHO JUU YA KUONDOKA KWAKE CHELSEA

Mshambuliaji nyota wa Chelsea anayekipiga AC Milan kwa mkopo amesema hakuondoka katika klabu hiyo ya London kwa kulazimishwa na Kocha Jose Mourinho. Torres raia wa Hispania amesema ulikuwa ni uamuzi wake kufanya na maneno yake yameondoa taarifa za utata kwamba Mourinho ndiye alimtaka kwenda Milan kwa mkopo wa miaka miwili.

RASMI ANGA FIFA YAACHIA NEMBO YA KOMBE LA DUNIA 2018, WANA ANGA WA WAITANGAZA

NEMBO ITAKAYOTUMIKA KWENYE KOMBE LA DUNIA MWAKA 2018 NCHII RUSSIA IMEANIKWA HADHARANI KUPITIA WANA ANGA WA NCHI HIYO. WALE JAMAA AMBAO HUENDA MWEZINI. SASA IKO WAZI NA INAJULIKANA IKIWA NI BAADA YA ILE YA ZAKUMI YA AFRIKA KUSINI MWAKA 2010 NA ILE YA BRAZIL 2014.

Wednesday, October 29, 2014

RONALDO APIGA HAT TRICK YA TUZO LA LIGA, MESSI AAMBULIA PATUPU

Cristiano Ronaldo amekomba zawadi tatu 'hat trick' za tuzo ya wachezaji bora Ligi ya Hispania maarufu kama La Liga. Huku mpinzani wake Lionel Messi akiambulia patupu, tuzo tatu alizobeba Ronaldo ni pamoja na Mchezaji Bora, Mfungaji Bora na Mshambuliaji Bora wa La Liga. Ilikuwa furaha kubwa kwa Ronaldo ambaye aliongozana na mpenzi wake Iryna Shayk, mwanamitindo kutoka Urusi. Pamoja na Ronaldo kubeba tuzo hizo, timu yake ya Real Madrid imetawala zaidi kuliko klabu nyingine ya Hispania. Zawadi ya kiungo bora imekwenda kwa Luka Modric huku Sergio Ramos akichukua tuzo ya beki bora. Kipa mpya wa Real Madrid, Keylor Navas amechukua tuzo ya mlinda mlango bora. Kabla ya kutua Madrid, Navas alikuwa akikipiga Levante. Barcelona pia imefanikiwa kupata tuzo tatu, Andrés Iniesta alitangazwa kuwa kiungo bora mshambuliaji, huku Ivan Rakitic na Rafinha wakitwaa tuzo mbili za Fair Play and Breakthrough. Kutokana na mafanikio makubwa msimu uliopita, Kocha wa Atlético, Diego Simeone alibeba tuzo ya Kocha Bora. Mshambuliaji nyota wa Sevilla, Carlos Bacca akachukua tuzo mchezaji Bora kutoka Amerika Kusini na Yacine Brahimi wa Granada akawa Mchezaji Bora kutoka Afrika.

RAY C AHAMUA KUMFUTIA KESI CHID BENZ KESI!

Rehema Chalamila ‘Ray C’. WAKATI nyota wa muziki wa Hip Hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’ akikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa na madawa ya kulevya akiwa njiani kuelekea Mbeya, Rehema Chalamila ‘Ray C’ aliyekuwa amemfungulia kesi ya kumpiga katika kituo cha Polisi cha Oysterbay, amefuta shauri hilo na kumsamehe. Akipiga stori na gazeti hili, Ray C alisema ameamua kumsamehe kwa sababu yeye ni mtu wa Mungu na anaamini yanayomtokea ni ishara ya kumtambulisha kuwa matumizi ya dawa za kulevya hayafai. “Mimi ni mtu wa Mungu, nimemsamehe na wala sitaki kesi naye, lakini kumsamehe mimi peke yangu hakusaidii, Watanzania wote kwa pamoja tumuombee ili jambo hili limalizike na likiisha, ninamuomba aje tushiriki pamoja katika tiba ya Methadone,” alisema. Ray C maarufu kama kiuno bila mfupa, alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuandika waraka katika akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram, akimsihi Chid Benz kuachana na matumizi hayo ya madawa ya kulevya.
Nyota wa muziki wa Hip Hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’. “Pole kaka yangu Chid Benz, naumia kuona tatizo ulilokuwa nalo bado haujalitafutia jibu, mimi ni dada yako na tumeshafanya kazi pamoja. Tatizo ulilonalo na mimi nilishakuwa nalo na niliweza kulitatua sababu nilijitambua na kutafuta suluhu, nimejaribu kila njia kukushauri badala yake ukaja na rungu la kimasai na kunitandika nalo nyumbani kwangu,” yalisomeka baadhi ya maandishi yake mtandaoni. Ray C aliendelea kuandika kuwa kitendo cha kukamatwa kwake na madawa hayo kitakuwa ni jibu zuri kwake kuwa anakoenda si salama na kumtaka abadili njia na kuungana naye kwenye tiba ya Methadone kwani ndiyo kiboko ya madawa ya kulevya.
Kamanda Nzowa. Chid Benz alikamatwa akiwa na kete 14 za madawa ya kulevya pamoja na misokoto miwili ya bangi hadi gazeti hili linakwenda mtamboni, alikuwa bado hajafikishwa mahakamani kukabiliana na tuhuma hizo.

HIKI NDO KITU KIKUBWA ALICHOKIFANYA BALOTEL AKITOKEA BENCHI USIKU HUU DHIDI YA SWANSEA

KLABU ya Liverpool imeichapa Swansea mabao 2-1 katika mchezo wa Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Capital One Cup usiku huu Uwanja wa Anfield. Jordan Henderson alipewa beji ya Unahodha, kocha Brendan Rodgers akifanya mabadiliko ya wachezaji tisa katika kikosi chake cha kwanza. Winga wa Swans, Marvin Emnes aliifungia timu yake bao la kwanza dakika ya 65, kabla ya Mario Balotelli aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Rickie Lambert kusawazisha zikiwa zimesalia dakika tano. Federico Fernandez alitolewa kwa kadi nyekundu dakika za mwisho kwa kumchezea rafu Philippe Coutinho kabla ya Dejan Lovren kuifungia Liverpool bao la ushindi dakika za majeruhi na kuwapeleka Wekundu hao Robo Fainali.

CPL:MATOKEO YA CHELSEA vs SHREWBURY HAYA HAPA

KLABU ya Chelsea imetinga Robo Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup baada ya kuichapa mabao 2-1 Shrewsbury usiku huu. Chelsea ilipata bao la kwanza mapema tu kipindi wakati mkongwe, Didier Drogba alipomalizia pasi maridadi ya mwanasoka wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah. Lakini Shrewsbury ikapata bao la kusawazisha kupitia kwa Andrew Mangan aliyetokea benchi dakika ya 77, kabla ya Jermaine Grandison kujifunga dakika nne baadaye kuipa ushindi timu ya Jose Mourinho.

Tuesday, October 28, 2014

Kingine alichozungumza Jackie Chan kuhusiana na mtoto wake kukamatwa na dawa za kulevya.

Mkali wa movie kutoka Hong Kong China, Jackie Chan ameomba vyombo vya habari ‘vijichunge’ na namna vinavyoandika taarifa kuhusiana na kitendo cha mtoto wake kukamatwa na dawa za kulevya kwa kuwa kufanya hivyo si kumuumiza yeye (Jackie Chan) bali ni kumuumiza mama wa mtoto huyo. Jackie Chan amesema kupitia tukio hilo amejifunza kuwa baba bora kitu ambacho hakukijua siku za nyuma. Mtoto wa staa huyo, Jaycee Chan alikamatwa kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi zaidi ya gramu 100 ndani ya nyumba yake, na baadaye kushitakiwa kwa kuuza dawa hizo. Jackie Chan ambaye amekuwa balozi wa kupinga dawa za kulevya tangu mwaka 2009, amesononeshwa na pia ameomba radhi kwa kosa alilotenda mwanae ambapo hii imekuwa mara yake ya kwanza kujibu swali linalohusiana na kesi ya mtoto wake, akisema kupitia hilo amejifunza kuwa baba bora.

Monday, October 27, 2014

NUH MZIWANDA AHAMUA TENA KUWANYAMAZISHA WANAFKI KWA KUCHORA TATOO NYINGINE YENYE PICHA YA MPENZI WAKE SHILOLE

Wakati Nick Cannon ametoka kufunika Tattoo yenye jina la mke wake Mariah Carey ambaye wametengana kwa kuongeza mchoro mwingine juu yake hivi karibuni, msanii wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda ameongeza Tattoo ya pili ya mpenzi wake Shilole kwenye mkono wake. Nuh amesema mchoro huo wa pili kwenye mwili wake una sura ya Shishi baada ya ile ya kwanza ambayo ni jina la ‘Shishi Bybee’. “Tattoo ya pili ni sura aisee sura ya mpenzi wangu Shishi,” ameiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm. “nimetaka kuweka maana ya jina pamoja na sura yake unajua jina tu lilikuwepo kukamilisha upendo ule na thamani na shkurani kwake so nilichora ile Shishi Bybee ya maneno halafu baadae nimechora sura yake, nimechora mkono ule ule, so hii shishi Bybee iko nyuma ya mkono wangu halafu hii sura yake iko mbele.”
Mziwanda ameongeza kuwa mchoro huo umegharimu shilingi laki nne na nusu. “Tattoo nimechora juzi, tumetumia kama laki nne hivi nne na nusu ukijumlisha na usafiri sababu jamaa alikua katoka Arusha. Ile ya mwanzo iligharimu kama laki mbili mbili na nusu”.

Sunday, October 26, 2014

HII NDO TIMU ANAYOTARAJIA KUTUA DAVID MOYES

KOCHA David Moyes yumo kwenye orodha fupi ya mwisho ya makocha wanaotakiwa na Inter Milan ya Italia inayotaka kumtimua kocha wake wa sasa, Walter Mazzarri. Kocha huyo wa zamani wa Manchester United na Everton anapewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya Mazzarri, ambaye timu yake inacheza na Cesena leo akiwa katika shinikizo baada ya mwanzo mbaya unaoifanya Inter iwe katika nafasi ya tisa kwenye msiamo wa ligi hivi sasa. Moyes mwenyewe amekua akiamini akipata nafasi ya kufundisha klabu nje ya Uingereza itakuwa ni fursa nzuri kwake kurejesha heshima yake- hivyo akifanikiwa mpango huo atakuwa ametimiza ndoto zake kwa sasa.

Saturday, October 25, 2014

JE UNAFAMAMU NI WASANII GANI WA BONGO WALIMSHTUA SANA DAVIDO KWENYE FIESTA 2014 DAR

Unaambiwa weekend iliyopita kwenye Fiesta ya Dar es salaam mwimbaji Davido wa Nigeria alitumia dakika zake zote kutazama screen zilizokua zimewekwa nyuma ya stage ya Fiesta baada ya kusikia shangwe zilizokua zinapigwa baada ya Wakali wengine kupewa time ya kumiliki stage. Alilazimika kutazama TV hizo kwa umakini baada ya kuona shangwe walilopata WEUSIambapo mashabiki walikua wanaimba nyimbo zao kwa muda mrefu ambapo Davido kabla ya kuuliza alitumia muda mrefu kuwatazama kwa makini baada ya kushangazwa na shangwe walilokua wanapata WEUSI hawa.
Baada ya Wakali hawa kumaliza show Davido alianza kuuliza ni kina nani na wana umaarufu kiasi gani ambapo mmoja wa marafiki zake amesema stori hazikuishia uwanjani kwenye Fiesta bali mpaka Hotelini Davido alionyesha kushangazwa na shangwe la WEUSI na kuwaongelea tena. Hii itafanya idadi ya Wasanii wa bongo wanaofahamika na Davido iongezeke manake alipokuja juzi Tanzania alihojiwa muda mfupi tu baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege na kusema msanii pekee wa Tanzania anaemfahamu ni Diamond Platnumz. Mengine aliyoyasema ni kwamba kwenye album yake mpya inayotoka mwanzoni mwa 2015 wameshirikishwa wasanii wachache kutoka Afrika ambao ni pamoja na Diamond na Mafikizolo na kwamba kuna wasanii wawili wakubwa wa kimataifa aliowashirikisha ambao hatowataja kwa sasa