Thursday, August 21, 2014

KAMA UNGEKUWA MWALIMU WA NIDHAMU UNGEWPA ADHABU GANI WANAFUNZI HAWA?

HIVI NDO VITUO VITAKAVYO UZA TIKETI ZA MECHI KATI YA WAKONGWE WA REALMADRID VS TANZANIA ELEVEN

Waratibu wa ziara ya kikosi cha Real Madrid, Kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), wametangaza sehemu ambazo tiketi za mechi inayosubiriwa kwa hamu ya wakongwe wa Tanzania Al maarufu kama Tanzania Eleven dhidi ya Real Madrid wakongwe zinapouzwa.
Wamesema vituo vinaweza kuongezeka kutokana na mahtaji ya juu ya watu lakini vituo zaidi ya 10 tayari zimeanza kuuza tiketi hizo.

TICKET   ZA REAL MADRID  ZINAPATIKANA  KATKA  VITUO VIFUATAVYO.
TSN   BAMAGA SUPERMARKET .
TSN  OIL  BAMAGA PETROL STATION.
TSN   SUPERMARKET  UPANGA .
TSN  SUPERMARKET  TEGETA.
BIG BON    MSIMBAZI.
BIG BON   SINZA.
BIG BON  TEMEKE.
BIG BON MBAGALA.
BIG BON TEGETA.
TSN SUPERMARKET TANCORT  HOUSE .
MARRY   BROWN MASAKI.
TSN   SUPERMARKET  MIKOCHENI.
TSN  OIL TABATA  KIMANGA.
ENGEN   MIKOCHENI
MARRY  BROWN MLIMANI CITY

KIBOKO YA MAN U YASAJILI BEKI WA ARGENTINA

KLABU ya Swansea City imekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 8 wa Federico Fernandez kutoka Napoli. Beki huyo wa kati alikwenda kufanyiwa vipimo vya afya wiki hii Wales na kusaini Mkataba wa miaka minne, akiweka rekodi ya kuwa mchezaji ghali zaidi wa nafasi za ulinzi kusajiliwa na klabu za Wales. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye aliichezea Argentina katika Kombe la Dunia, ataziba pengo la beki wa kati Chico Flores aliyeondoka, kwa kucheza na Ashley Williams. Na mdadisiblog/festosaimon

#Exclusive: Tumesoma sana ya Magazeti, sasa tuisikilize sauti ya Okwi mwenyewe kuhusu kuondoka Yanga.

Mganda Emmanuel Okwi harudi tena Yanga na sasa ameweka wazi kwamba anashughulikia mipango yake kwenda kucheza soka la Ulaya >>> Okwi aachana na Yanga mchana kweupe!!!!! >>> Okwi achukizwa na ishu ya DVD ya Maximo <<<< hizo ni baadhi tu ya sentensi kwenye Magazeti mbalimbali ya Tanzania kwa wiki kadhaa ila ukweli kutoka kwa Okwi mwenyewe ni huu hapa chini.

Akiwa Kampala ameongea kwenye Exclusive interview na Bill the African ambae ni ripota wa millardayo.com na AyoTV Kampala Uganda na kusema haya >>> ‘Mimi na Yanga tulikua na makubaliano ya mkataba na hakuna ukweli kwamba Mshahara niliokua nalipwa Yanga ni mdogo, mshahara usingekua unatosha nisingekubali kusaini mkataba ‘ ‘Ni kweli kuna mambo mengi hayapo sawa kati yangu na club yangu ya Yanga ila ni mambo ya ndani ambayo nisingependa kuyazungumzia, ni mambo madogo ambayo nadhani yanaweza kuisha‘ ‘Hakuna ukweli kwamba mimi nakwenda Ulaya, sijui hata imetoka wapi na nani kaanzisha hii ya Ulaya, mimi bado ni mchezaji halali wa Yanga na huwa naongea nao karibu kila siku, hata jana nimetoka kuongea na katibu mkuu na mambo yote yanaelekea vizuri hamna shida yoyote mpaka sasa hivi‘

Kama unahitaji zaidi kupata ushahidi wa sauti yake Okwi akiongelea hi iishu bonyeza play hapa chini.  PLAY HAPA
USIKILIZE 

Credit millardayo

LIVERPOOL SASA YAGEUKIA KWA MARIO BALOTELLI

Liverpool imeanza mipango ya kumnasa Mario Balotelli kutoka AC Milan. Kocha wa Liverpool, Brendan Rogders anataka kumnsa mshambuliaji huyo kwa mkopo kuyoka Milan. Awali kocha huyo alisema hawana mpango wa kumsajili Balotelli. Hata hivyo imeelezwa AC Milan wangependa suala hilo liwe biashara ya ‘cash’ na si mkopo. Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA USOME HABARI ZINGINE 

TIMU YA ARSENAL YAPATA PIGO LINGINE KUBWA

NAHODHA wa Arsenal, Mikel Arteta atakosa mechi mbili zijazo za klabu yake baada ya kuumia kifundo cha mguu katika mchezo wa kwanza wa mchujo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Besiktas. Nyota huyo wa Arsenal alitolewa nje dakika ya 50 kwenye Uwanja wa Olympic Ataturk baada ya kuumizwa na mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Demba Ba. Arsenal pia itamkosa nyota wake mwingine, Aaron Ramsey katika mchezo wa marudiano na timu hiyo ya Uturuki, baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya nano kipindi cha kwanza dhidi ya Beskitas. Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI  

EFM yavunja ngome ya kipindi cha michezo cha Radio One, yawachukua Maulid Kitenge na Omary Katanga

Kipindi cha michezo cha Radio One ‘Spoti Leo’ kimepata pigo kali baada ya watangazaji wake mahiri, Maulid Kitenge na Omary Katanga kuhamia EFM 93.7 ya Dar es Salaam. Maulid Kitenge na Omary Katanga enzi wakiwa Radio One Kuondoka ghafla kwa watangazaji hao waliokifanya kipindi cha ‘Spoti Leo’ kuwa kipindi bora zaidi cha michezo nchini kutokana na umahiri wao katika kuhoji na kutangaza vipindi vya michezo, ni pigo kubwa kuwahi kutokea Radio One katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni. Kuziba pengo hilo, watangazaji wa michezo wa Capital FM (kituo cha radio ndugu) ndio wanaofanya kipindi cha michezo cha Radio One kwakuwa Isaac Gamba ambaye naye hufanya kipindi hicho yupo likizo. Maulid Kitenge na Omary Katanga wanaanza kutangaza kipindi cha michezo cha EFM cha nusu saa, leo Alhamis kuanza saa 1 jioni. Wasikilize Kitenge na Katanga kwenye promo ya kipindi chao EFM.

           BONYEZA HAPA           KUWASIKILIZA 

HII MPYAAA..!! SIKIA HII YA INAYOMUHUSU DULLY SYKES KUIBA MKE WA MZUNGU NA KUTAKA KUMUOA, SIKILIZA NDUGU WALIVYOKUJA JUU..!!

Kama ilivyo ada makamanda wa @gossipcourt walipokua mzigoni walifanikiwa kunasa vinasaba vya sauti vikimzungumzia msanii wa mziki wa kizazi kipya u maarufu kama bongo flava alievunja ndoa ya mwanadada aliolewa na mzungu,huku wengi wakimshangaa bidada huyo kwa kuchezea bahati ati kumfanyia vituko mzungo na kuhamia kwa bongo flava huyo huku wakiponda starehe na raha kwa pesa zinazotoka kwa mzungu huyo....

 BONYEZA HAPA KUSIKILIZA 

SOMA ALICHOKISEMA ALIKIBA KUHUSU UWEZEKANO WA KUFANYA NYIMBO NA DIAMOND

Ulichokuwa ukisubiri kwa muda mrefu huenda kikatokea hivi karibuni. Collabo ya Alikiba na Diamond Platnumz mabibi na mabwana inanukia. Akizungumza na kipindi cha Jahazi cha Clouds FM leo (20/8), Alikiba amesema upo uwezekano wa kufanya kazi ya pamoja kama kukitokea mabadiliko. “Mawazo ya kolabo yapo, mawazo unapata mengi tu, hiyo nimeshaisikia vilevile, na wewe sio mtu wa kwanza kuniuliza hicho kitu kipo. "Lakini muziki vile vile kama unavyoona kuna mavazi na style, vazi hili linatakiwa liende disko hili ni vazi la beach, vazi hili la ofisini, vazi hili la mpirani, hili la mchangani, hili la kwenye ukumbi unajua vitu kama hivyo! alisema AliKiba. "Kwahiyo Diamond akipata vazi lake ambalo linahusiana na vazi ambalo natakiwa nivae, hakuna tatizo tunafanya kazi kama kawaida, kwa sababu yeye anafanya kazi vizuri,” Alipoulizwa kama kuna uwezekano wa kufanya show kubwa na Diamond alijibu kwa kicheko: “Wewe hujui kama watu wanasubiria (show) au unajisahaulisha.”

SOMA HAPA KIPYA ALICHOKISEMA DIVA KUHUSU PENZI LAKE KWA CRAZY GK

Ile hatua ya U boifriend na U girlfriend ikiwa imepita na kuingia katika hatua ya uchumba wa mahaba kedekede, dada yetu Diva alijikuta anamwaga chozi baada ya watu mbalimbali kumtupia maneno kwamba amempendea King Crazy Gk umaarufu wake ili abaki kupata KIKI Mjini. Diva alijikuta anatoa maneno makali ya hasira na kuangua kilio na kudai kuwa hajampendea Gk umaarufu wake sababu yeye ni Diva ni maarufu pia hapa Tanzania, hakuishia hapo alizidi kudai ya kuwa amechoshwa na watu wengi kusema ana mahusiano na Gk ambae hana Pesa na ameachana na mwanaume ambae anapesa na cheo kikubwa Tanzania. Diva:Nimechoshwa kuulizwa maswali ya Prezzo au mwanasiasa sababu huko siko tena na sina mahusiano nao zaidi ya urafiki wa kawaida wa kuongea nao kama watanzania wenzangu na pili amedai kuwa hana hisia zozote za kimapenzi na watu hao sababu yeye yuko na Mpenzi wake na anafurahia mapenzi hayo na mume wake ambae ni Mungu wa Muziki Tanzania. Diva Binti mwenye mvuto na umbo la kuvutia na mvuto wa sura ya babyface na macho ya duara alidai kuwa King Crazy Gk ni Mtu mwenye kipato kizuri tu ila sio mtu wa kujionyesha au kuishi maisha ya kujionyesha na ni mtu mtaratibu anaeishi maisha yake alioridhika nayo na anatumia pesa zake kulipia elimu na kufanya mambo yake na biashara zake binafsi tofauti na watu wanavyomfikiria. Diva la Diva alisema kuwa Hakumpendea Gk Pesa au Umaarufu wake amempenda yeye kama yeye na anachukia baadhi ya watu kumuingilia kimawazo maisha yake ya mapenzi ambayo mashabiki wengi wameonekana kuvutiwa nayo kupitia mtandao wa instagram. Na mdadisiblog/festosaimon