 |
Kipindi cha michezo cha Radio One ‘Spoti Leo’
kimepata pigo kali baada ya watangazaji wake
mahiri, Maulid Kitenge na Omary Katanga
kuhamia EFM 93.7 ya Dar es Salaam.
Maulid Kitenge na Omary Katanga enzi
wakiwa Radio One
Kuondoka ghafla kwa watangazaji hao
waliokifanya kipindi cha ‘Spoti Leo’ kuwa
kipindi bora zaidi cha michezo nchini kutokana
na umahiri wao katika kuhoji na kutangaza
vipindi vya michezo, ni pigo kubwa kuwahi
kutokea Radio One katika kipindi cha miaka ya
hivi karibuni.
Kuziba pengo hilo, watangazaji wa michezo wa
Capital FM (kituo cha radio ndugu) ndio
wanaofanya kipindi cha michezo cha Radio One
kwakuwa Isaac Gamba ambaye naye hufanya
kipindi hicho yupo likizo.
Maulid Kitenge na Omary Katanga wanaanza
kutangaza kipindi cha michezo cha EFM cha
nusu saa, leo Alhamis kuanza saa 1 jioni.
Wasikilize Kitenge na Katanga kwenye promo ya
kipindi chao EFM. |
BONYEZA HAPA KUWASIKILIZA
0 comments:
Post a Comment