Thursday, August 21, 2014

KIAFRIKA ZAIDI: KWAHILI HAKUNA MZUNGU ANAYEWEZA…..!!!!!

Picha: Mfahamu ‘baby mama’ wa Professor J, ‘Mama Lisa’

Black Rhyno amewahi kuoa kumzidi kaka yake Professor J lakini hiyo haimaanishi kuwa Mchawi huyo wa Rhymes hana mke mtarajiwa. Kupitia Instagram, Professor J amemweka wazi mwanamke anayeweza kushika wadhifa wa Mrs Joseph Haule. “OF COURSE ni Baba LISA na Mama LISA. …. What more can I SAY?? #MWANALIZOMBE,” ameandika Professor kwenye picha hiyo juu.

CHEKI GAZETI LA MICHEZO LA AS LA HISPANIA LILIVYOANDIKA KUHUSU UJIO WA REAL MADRID

Gazeti maarufu la michezo la AS la nchini Hispania, limetumia ukurasa mzima kuelezea ziara ya kikosi cha wakongwe cha Real Madrid. Gazeti hilo limeelezea namna kikosi hicho kinavyofanya ziara kwa mara ya kwanza barani Afrika. Madrid watacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Tanzania Eleven ambao wameanza kujifua chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa. Mechi hiyo itapigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Madrid wanatarajia kuanza kuwasili kesho. Kati ya wadhamini wa ziara hiyo na mechi ya kirafiki ni TSN ambao pia ni waratibu wa ziara hiyo, Hoteli ya Sapphire, Bin Slum, Gazeti la Championi na kampuni ya ndege ya Fast Jet. Na salehe ally

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBONYA HAPA 

Picha: Hii ndo hotel ambayo wachezaji waliochaguliwa kukipiga na wakongwe wa Realmadrid Agosti 23 wameweka kambi

Kikosi cha Tanzania Eleven chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa, kitaweka kambi kwenye hoteli maarufu ya kisasa ya Sapphire Court ya jijini Dar es Salaam. Kambi hiyo inatarajia kuanza leo na wachezaji wataingia kambini hapo kujiandaa kwa ajili ya mechi dhidi ya wakongwe wa Real Madrid itakayopigwa jijini Dar es Salaam, Jumamosi. Madrid itaongozwa na Luis Figo aliyewahi kuwa nota wa Barcelona, baadaye Real Madrid na Inter Milan. Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu na tayari tiketi zimeanza kuuzwa katika sehemu mbalimbali.Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI ILI UPATE HABARI KIRAHISI 

WACHEZAJI WA MAN CITY WAZIDI KUJITUNDIKA VITANZI,HUYU NAYE AJITUNDIKA KITANZI CHA MIAKA MINNE

MSHAMBULIAJI Edin Dzeko amesaini Mkataba wa miaka minne na mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester City. Mwanasioka huyo wa kimataifa wa Bosnia ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter juu ya kusaini kwake mkataba mpya akisema: "Furaha na kujivuniaa kusaini mkataba wangu mpya na Manchester City. Nipo hapa ambako ni kwangu. Nimerefusha hadi 2018,". Mpachika mabao huyo amefunga mara 65 katika mechi 156 alizoichezea klabu hiyo tangu ajiunge nayo kutoka Wolfsburg mwaka 2011. Na mdadisiblog/,festosaimon

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZA HAPA 

SIMBA NA YANGA OKTOBA 12 NA FEBAURI 8, MECHI ZAO NA AZAM FC…RATIBA KAMILI LIGI NZIMA HII HAPA

WATANI wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba SC na Yanga watakutana Oktoba 12, mwaka huu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mzunguko wa kwanza, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ladha ya Ligi Kuu ni mechi baina ya miamba hiyo miwili nchini- na kidogo mechi zinazozihusisha timu hizo na mabingwa watetezi, Azam FC, nazo pia huwa za kukata na shoka. Msimu uliopita, mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya 3-3, Simba wakitoka nyuma kwa 3-0 hadi mapumziko na marudiano, Yanga walisawazisha dakika za lala salama kupata sare ya 1-1. Lakini Simba SC ilijichukulia ubabe wa jumla wa msimu dhidi ya watani wao, baada ya kuwafunga Yanga SC 3-1 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe Desemba mwaka jana Uwanja wa Taifa. Mzunguko wa pili, timu hizo zitakutana Februari 8, mwakani, mchezo wa kwanza Yanga mwenyeji, wa pili Simba mwenyeji. Azam FC na Simba zitakutana Januari 1, mwaka 2015 wakati marudiano yatakuwa ni Aprili 12, mwaka huo. Yanga itamenyana na Azam FC Novemba 9, mwaka huu wakati mchezo wa marudiano utapangiwa siku. Ikumbukwe Septemba 13, Yanga na Azam FC zitafungua pazia la Ligi Kuu kwa mchezo wa Ngao ya Jamii Uwanja wa Taifa.

Wednesday, August 20, 2014

RATIBA LIGI KUU YATOKA; YANGA SC KUANZA NA MTIBWA SUGAR MOROGORO, AZAM NA POLISI MORO, SIMBA NA COASTAL DAR

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC wataanza na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu, wakati Yanga SC waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro siku hiyo. Washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine, Mbeya Septemba 20 na washindi wa nne, Simba SC wataanza na Coastal Union ya Tanga Septemba 21, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani. ITAENDELEA:

FIFA YAIPIGA NYUNDO NZITO TIMU YA BARCELONA

Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limepiga nyundo kwenye kidonda baada ya kuizua Barcelona kusajili hadi Januari 2016. Awali Barcelona ilikata rufaa kwa Fifa ikipinga adhabu hiyo, badala yake Fifa imetia msisitizo kuhusiana na adhabu hiyo. Sasa Barcelona itaendelea kusubiri kufanya usajili hadi mwaka keshokutwa!. Na mdadisiblog/festosaimon

CHID BENZ AMWAGA MACHOZI CLOUDS ALIVYOKUWA ANAELEZEA STORY YA DIAMOND KABLA HAJAKUWA STAR

Chidi Benz alitabiri mbele ya Diamond Platnumz (wakati bado underground) kuwa angekuja kuwa msanii mkubwa. Hata hivyo maneno muhimu ambayo rapper huyo alimwambia Diamond ni kuwa asije kunywa pombe wala kuvuta (unga/bangi) maishani mwake. Chidi ambaye Jumanne hii ameachia single yake mpya 'Mpaka Kuche' aliyowashirikisha Diamond na AY, alikuwa akihojiwa kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM. Katika kuashiria kuwa hiyo ilikuwa ni interview iliyogusa sehemu ya katikati kabisa ya moyo wake, Chidi alijikuta akibubujikwa na machozi. Chidi alikumbushia siku Diamond alipompigia simu kujitambulisha kwake kuwa ni msanii mchanga anayetaka kumshirikisha kwenye wimbo wake. Hata hivyo siku Diamond amefanikiwa kumpata Chidi hewani ilikuwa ni baada ya kujaribu kumtafuta kwa siku nyingi bila mafanikio na aliwahi kumweleza mama yake namna alivyo na hamu ya kumshirikisha rapper huyo aliyekuwa akimkubali. Baada ya kumpigia simu, Chidi anadai alimuambia Diamond aende kwao maghorofani Ilala wakazungumze vizuri. "Sasa nikamuona (Diamond) nikajua huyo dogo ndio yule niliwaambiaga watu kuwa ‘huyu dogo ana sura moja hivi imekaa.. sura yake lazima utaiongelea tu, lazima utasema kitu, namuona atakuja kuwa staa tu, simjui lakini the way alivyo, atakuja kuwa staa,” alikumbushia Chidi.