Wednesday, August 20, 2014

DIVA WA CLOUDS FM ATUBU KUMKOSEA MSANII CHID BENZ BAADA YA KUMCHAFUA HUKO INSTAGRAM!!!

Mwanadada mtangazaji wa Clouds FM, Loveness maarufu kama DIVA..jana kupitia ukurasa wake wa Instagram alikili kumkosea msanii wa Bongo flava, Chid Benz....kutokana na comment yake ya siku za hivi karibuni kuhusiana na issue ya Chid kumpiga Ray C... Soma hapa alichokiandika!!!

DUNGA AWATOSA ALVES, MARCELO, AITA KIKOSI CHAKE KUWAVAA COLOMBIA

Kocha wa Brazil, Dunga ametangaza kikosi chake kwa ajili ya ya mechi za kirafiki dhidi ya Colombia, mechi itakayopigwa Septemba 5 jijini Miami, na dhidi ya Ecuador Septemba 9 jijini New Jersey, Marekani. Kati ya wachezaji aliowaita ni Miranda wa Atlético de Madrid na Filipe Luís. Lakini Dunga akaamua kuwaacha mabeki Dani Alves wa Barcelona na Marcelo wa Real Madrid. Nahodha Thiago Silva anayekipiga PSG pia ni mgonjwa, hivyo pia amemuacha katika kikosi chake. Wachezaji waliocheza Kombe la Dunia 2014 ambao Dunga amewaita ni Jefferson, David Luiz, Maicon, Luiz Gustavo, Fernandinho, Ramires, Oscar, Hulk, Willian and Neymar.

HAYA NDO MTOKEO YA MECHI KATI YA REALMADRID VS ATLETICO SUPER CUP YA KWANZA BERNABEU

REAL Madrid imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Atletico Madrid katika mchezo wa kwanza wa Super Cup ya Hispania usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu. Msambuliaji Crisitiano Ronaldo alitolewa kipindi cha pili kumpisha mchezaji mpya, James Rodriguez, kabla ya Mcolombia huyo kuifungia bao la kuongoza Real dakika ya 81. Atletico Madrid ilikomboa bao hilo zikiwa zimesalia dakika tatu kupitia kwa Raul Garcia na sasa Real Madrid itakabiliwa na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano Uwanja wa Vicente Calderon. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo, Modric, Kroos, Alonso, Bale, Ronaldo/Rodriguez dk45 na Benzema. Atletico Madrid: Moya, Juanfran, Miranda, Godin, Siqueira, Mario, Gabi, Koke, Saul/ Griezmann dk56, Raul Garcia, Mandzukic

ORIJINO KOMEDI WAPATA PIGO JINGINE, MENEJA WAO AWAKIMBIA. SOMA HAPA

Kundi maarufu la vichekesho ambalo kwa sasa ni kama halipo, limepata pigo kubwa baada ya aliyekuwa meneja wao, mtangazaji nyota wa zamani wa televisheni, Christina Mosha maarufu kama Seven, kuwamwaga na hivyo kuachana nao. Akizungumza na gazeti hili juzikati, Seven alisema ameachana nao baada ya mkataba wake wa sasa kumzuia kufanya kazi na watu wengine zaidi ya walio chini ya mwajiri wake mpya. “Hivi sasa niko na Sony, wao wananizuia kufanya kazi na wasanii ambao hawako nao, hivyo baada ya mkataba wangu na wao kumalizika, nimeamua kuachana nao. Mimi ni mwakilishi wa Sony barani Afrika, ninashughulika na wasanii toka nchi tofauti za Afrika, kama Senegal, Kenya na kwingineko kasoro Afrika Kusini,” alisema.

COUTINHO AITWA BRAZIL MPYA BAADA YA KOCHA DUNGA KUBOMOA KIKOSI KILICHOVURUNDA KOMBE LA DUNIA

KOCHA mpya wa Brazil, Carlos Dunga amekibomoa kikosi cha timu hiyo kilichovurunda Kombe la Dunia kwa kuwatema wachezaji 13 na kuita wengine wapya. Philippe Coutinho ni miongoni mwa ingizo jipya la wachezaji baada ya Kombe la Dunia baada ya Dunga kuvutiwa na kazi yake akiichezea Liverpool, wakati Neymar aliyepona majeruhi yake yaliyomfanya akose mechi mbili za mwisho za Kombe la Dunia ameitwa pia. Kikois cha wachezaji 22 kimetajwa jana kwa ajili ya mechi mbili za kiradiki dhidi ya Colombia na Ecuador. Na mdadisiblog,/festosaimon

MAMBO YAIVA ZIARA YA REAL MADRID NCHINI… FIGO, OWEN NA KAREMEBU WATUA KESHO DAR

MWANASOKA bora wa zamani wa dunia, Mreno Luis Filipe Madeira Caeiro Figo anatarajiwa kutua kesho na msafara wa kwanza ya magwiji wa Real Madrid tayari kwa mchezo dhidi ya magwiji wa Tanzania Agosti 23 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Figo ataongozana na nyota wengine wawili waliowika Real Madrid muongo uliopita, mshambuliaji Michael Owen aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi Kombe la Dunia mwaka 1998 Ufaransa na mwanasoka bora wa Oceania mara mbili 1995 na 1998 Christian Karembeu. Figo aliyestaafu Mei 31 mwaka 2009, alipiga tuzo mbili mfululizo mwaka 2000, Mwanasoka Bora Ulaya na Dunia na anakuja Tanzania kuwakumbushia watu enzi zake anatamba Real Madrid. Mapokezi makubwa yameandaliwa kwa ajili ya magwiji hao Real Madrid ambao sasa wanakuja kwa awali na hadi Agosti 22 kikosi kizima kitakuwa kimekamilika Dar es Salaam. Mkurugenzi wa makampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), Farough Baghozah ameiambia BIN ZUBEIRY kwamba magwiji hao watapokewa kwa maandamano Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam na kupelekwa hoteli ya Ladger Plaza, Bahari Beach. Kikosi cha magwiji wa Tanzania, kitakachomenyana na Real Madrid kinaendelea mazoezi Uwanja wa Karume kwa wiki sasa kwa ajili ya mchezo huo wa kihistoria. Makipa maarufu waliowahi kuwika nchini, Mwameja Mohamed na Manyika Peter wamejumuishwa katika kikosi cha Tanzania All Stars kitakachomenyana na magwiji hao wa Real Madrid. Chini ya makocha Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ na Wasaidizi Freddy Felix Minziro na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, Daktari Mwanandi Mkwankemwa na viongozi Mtemi Ramadhani, Hassan Mnyenye, Omar Gumbo na Hamisi Kisiwa kikosi hicho kitaingia kambini Dar es Salaam kujiandaa kwa mchezo huo wa Agosti 23, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Wengine walioItwa ni mabeki Nsajigwa Shadrack, Mecky Mexime, Boniface Pawasa, John Mwansasu, Abubakar Kombo, George Masatu, Habib Kondo, Viungo Suleiman Matola, Shaaban Ramadhani, Salvatory Edward, Sabri Ramadhani ‘China’, Yussuf Macho, Abdul Mashine, Abdul Maneno, Mao Mkami, Steven Nyenge, Madaraka Suleiman, Akida Makunda na Mtwa Kihwelo. Washambuliaji ni Monja Liseki, Iddi Moshi, Dua Said, Emmanuel Gabriel, Said Maulid, Thomas Kipese, Nasor Mwinyi ‘Bwanga’, Edibilly Lunyamila, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Clement Kahbuka, Madaraka Suleiman na Akida Makunda. Wachezaji waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Real Madrid watakuja nchini. Katika ziara hiyo, pamoja na kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi maalum cha wachezaji nyota wa Tanzania Agosti 23, pia watafanya utalii katika vivutio mbalimbali, ikiwemo kupanda mlima Kilimanjaro. Miongoni mwa nyota wanaotarajiwa kuja na Real nchini ni pamoja na Wanasoka Bora wa zamani wa Dunia, Mfaransa Zinadine Zidane, Mreno Luis Figo na Mbrazil, Ronaldo Lima. Na mdadisiblog,/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII 

Barcelona wameitaja hii ndio bei ya Suarez lakini kuna mambo yanachanganya.

Tunafahamu kwamba Luis Suarez alijiunga na Barcelona mwaka huu wa 2014 akitokea Liverpool aliyoichezea toka mwaka 2011-2014 na kuifungia magoli 69 kwenye mechi 110 alizocheza. Sasa ishu imekuja kwenye ada ya uhamisho kwenda Barca ambapo club hiyo imeweka wazi jana kwamba ilimchukua kwa pounds milioni 65 kutoka Liverpool. Kuna mchanganyiko umetokea baada ya hiyo bei kutajwa kwa sababu Liverpool walisema bei waliyomuuza mng’ataji huyu ni Pound milioni 75.

HII NDIO SABABU YA MIMI KUAMUA KUTAFUTA MKWANJA KWA NGUVU ZOTE ILI SIKUMOJA NIJE KUWAPATA WATOTO KAMA HAWA

BAYERN WALIVUNJA 'PROMISI', WALIMUAMBIA GUARDIOLA KWAMBA, KROOS HATOUZWA

Bayern Munich walivunja ahadi waliyompa Kocha Pep Guardiola kwamba kiungo Toni Kroos hatouzwa. Uongozi wa Bayern ulimuahidi Guardiola ambaye alisisitiza kiungo huyo ni muhimu sana. Lakini mwisho ilishindikana, akauzwa kwa wababe wa Hispania, Real Madrid. Pamoja na kuwa na Xabi Alonso ambaye ni mmoja wa viungo nyota, Madrid imemwaga mamilioni kumtwaa Kroos ambaye tayari ameanza kuonyesha cheche. Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI ILI UPATE HABARI PUNDE ZITUFIKIAPO