Monday, October 06, 2014
HIVI NDO JINSI MADADA WAREMBO WANAVOFANYA LAANA KWENYE CLUB ZA USIKU
NI SHEEEDAH.....MTUMISHI AVAMIA ENEO LA MAKABURI NA KUJENGA BAA
News Alert: Siri yafichuka: Sababu ya wabunge kucheza "kitorondo" bungeni hii hapa
Baada ya "Rasimu ya Sitta" kupitishwa na Bunge maalumu baadhi ya wabunge walilipuka kwa furaha na wengine wakakata mauno hadharani, huku mbunge wa Njombe kaskazini Deo Sanga akicheza "Kitorondo" na kukata mauno mbele ya halaiki.
Pia kuna wabunge wengine walikua wakicheza kwa kufuatisha milio ya miziki iliyokua ikirindima kupitia simu zao za mkononi.Watu wengi walihamaki kitendo cha wabunge kufurahia Rasimu hiyo hadi kufikia hatua ya kujitoa akili.
Hii hapa siri ya furaha ya Wabunge hao..
RASIMU YA WARIOBA ILIPENDEKEZA:
1. Mbunge akigombea vipindi vitatu basi, awaachie wengine.
2. Mbunge akivurunda ktk utendaji wake, wananchi wana uwezo wa kumuondoa na kuchangua mwingine.
3. Hakuna mbunge kuwa Waziri, Mkuu wa mkoa, m/kiti wa bodi ya shirika etc. (kwanini vyeo vyote mjilundikie nyie?).
4. Elimu ya mbunge iwe angalau stashahada (diploma) na kuendelea.
RASIMU YA SITTA (ILIYOPITISHWA) IMEPENDEKEZA HIVI:1. Ukomo wa Ubunge usiwe vipindi vitatu.. Hata wazee waliokaa bungeni miaka 50 kama Kingunge, waendelee tukugombea. Vijana wanaotaka kuwa viongozi labda wakajaribu kwny SACCOSS sio UBUNGE.
2. Mbunge akivurunda wananchi hawawezi kumfanya kitu chochote hadi miaka mitano iishe na mbunge apewe pensheni yake (Mil.160).
3. Ruksa Mbunge kuwa waziri, Mkuu wamkoa, DC, Mwenyekiti wa shirika, na vyeo vingine kadri anavyoweza kujilundikia. Wanaosema mbunge asiwena vyeo viwili au zaidi, wana "wivu wa kike" (according to Pius Msekwa).
4. Elimu ya Mbunge iwe kama ya Deo Sanga (mbunge Njombe Kask), yaani kujua kusoma na kuandika tu inatosha. Rasimu ya Sitta inasema si lazima mbunge awe na degree, diploma, au cheti.Si lazima mbunge awe na elimu ya sekondari. Si lazima Mbunge awe amemaliza elimu ya msingi. Hata kama alisoma akaishia darasa la 3 lakini anajua kusoma na kuandika RUKSA KUGOMBEA UBUNGE.
Sasa je katika mazingira haya wabunge wataacha kukata mauno na kucheza"kitorondo" kwa Rasimu hii kupita??JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA UKWELI.
Malisa GJ || Your Partner In Critical Thinking.!
HUYU NI MCHEZAJI ALIYEINGIA KWENYE ORODHA YA WACHEZAJI WA MANCHESTER UNITED MUHIMU OLD TRAFORD
HIVI NDO JINSI ARSENAL WENGER ALIVOTAKA KUMCHEZESHEA KICHAPO MOURINHO STARMFORD BRIDGE
HIVI NDO JINSI KICHWA CHA SANCHEZ KILIVOMPELEKA KIPA WA CHELSEA HOSPITALI APO JANA
EPL: MATOKEO YA MACHESTER UNITED vs EVERTON HAYA HAPA
Sunday, October 05, 2014
MAJANGAZ HARUSI YA KWANZA KUFUNGWA NA WASHIRIKI WOTE WAKIWA WATUPU WA MNAYAMA
MHITIMU WA CHUO AVUA NGUO ZOTE JUKWAANI ALIPOITWA KUPEWA CHETI ZA KUMALIZA CHUO
SALOON ILIYOKO SINZA..INAYOFANYA MASAJI HUKU IKIJIHUSISHA NA UTOAJI WA HUDUMA YA NGONO CHAFU HII HAPA
CREDIT GPL
BONGO MOVIE YAZIDI PUKUTIKA HUYU MWINGINE AJITOA NA KUSEMA MANENO HAYA MAZITO
Rekodi mpya waliyoweka FC Barcelona kwenye La Liga hii hapa
Kama ulikosa mchezo wa FC Barcelona vs Rayo Vallecano, matokeo haya hapa
Angalia trailer ya filamu mpya aliyoigiza mchezaji huyu wa Man United
Kocha huyu alalamika kunyimwa mualiko wa mvinyo na Van Gaal
Simba bado hali tete, haya hapa matokeo yao dhidi ya Stand United na mechi zingine za VPL
KAMA ULIKOSA Matokeo ya Manchester City dhidi ya Aston Villa haya hapa
Saturday, October 04, 2014
TAMBWE FITI KABISA KUWAVAA STAND UNITED TAIFA LE
MSHAMBULIAJI Amisi Tambwe yuko fiti
kucheza mechi ya leo, timu yake Simba SC
ikimenyana na Stand United Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam- lakini beki Issa
Rashid ‘Baba Ubaya’ na winga Haroun
Chanongo wataendelea kupumzika.
Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe
ameiambia BIN ZUBEIRY jana usiku
kwamba, Tambwe alifanya mazoezi vizuri
jana na ameonyesha yuko fiti kabisa.
Tambwe aliumia goti juzi jioni mazoezini
Uwanja wa Boko Veterani na kuzua hofu
kwamba anaweza kuongeza idadi ya
majeruhi wa timu hiyo ambayo tayari
inawakosa Ivo Mapunda, Paul Kiongera,
Nassor Masoud ‘Chollo’, Baba Ubaya na
Chanongo.
“Tambwe amefanya mazoezi vizuri tu, kama
nilivyosema, hayakuwa maumivu makubwa
na tunashukuru imekuwa hivyo. Ni matarajio
yetu ataanza mechi na Stand,”amesema.
Daktari huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar
amesema kwamba Issa na Chanongo
wameendelea na mazoezi mepesi na
kwamba hawatakuwa tayari kwa mchezo wa
leo.
Baada ya sare mbili mfululizo 2-2 na
Coastal Union ikitoka kuongoza 2-0 hadi
mapumziko na 1-1 na Polisi Moro pia
ikiongoza hadi baada ya kipindi cha kwanza,
Simba SC itajaribu kusaka ushindi wa
kwanza leo dhidi ya timu iliyopanda msimu
huu, Stand.
Tayari Stand wamekwishaonja ladha ya
ushindi katika Ligi Kuu kufuatia kushinda 1-0
katika mchezo wao uliopita dhidi ya wenyeji
Mgambo JKT mjini Tanga.
Lakini ikumbukwe Stand ilianza na kipigo
cha nyumbani cha mabao 4-1 kutoka kwa
Ndanda waliopanda nao Ligi Kuu msimu
huu.







