Wednesday, August 27, 2014

CAPITAL ONE: MAN U YAPIGWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI NA KITIMU CHA MCHANGANI,GIGGS AMWAGA CHOZI

Wachezaji wa MK Dons wakishangilia bao lao la kwanza
Analia: Kocha Msaidizi Ryan Giggs akiwa ameshika kichwa akilia kwa uchungu mwishoni mwa mchezo huo, huku kocha Louis van Gaal akiwa haamini macho yake
Wachezaji wa United wakiwa hoi baada ya kipigo

KOCHA Louis van Gaal ameendelea kuogelea katika bwawa la maji moto Manchester United, baada ya usiku huu kfungwa na Mk Dons ya Daraja la Kwanza mabao 4-0 katika michuano ya Kombe la Ligi, maarufu Capital One. Mabao yaliyomtia machungu Van Gaal leo yamefungwa na Will Grigg dakika ya 25 na 63 na Benik Afobe anayecheza kwa mkopo kutoka Arsenal dakika ya 70 na 83. Kocha Msaidizi Ryan Giggs alionekana kufuta machozi baada ya bao la tatu, akiwa kwenye benchi na bosi wake, van Gaal. Kikosi cha MK Dons: Martin, Baldock, Kay, McFadzean, Lewington, Carruthers, Potter, Reeves, Alli, Bowditch, Grigg. Subs: Green, Spence, Randall, McLoughlin, Powell, Hitchcock, Afobe. Man Utd: De Gea, Vermijl, Evans, Michael Keane, James, Janko, Anderson, Kagawa, Powell, Welbeck, Hernandez.

Tuesday, August 26, 2014

UNAWEZA KUZIELEZEAJE PICHA PICHA HIZI!!! UKIWA KAMA MTU MWENYE AKILI ZAKO TIMAMAMU!!

VAN GAAL MENO THELATHINI NA NJE, YOTE MBILI AKIWA NA WAKALA WA DI MARIA LEO

DILI la Angel di Maria kutua Manchester United linakaribia kabisa kutimia baada ya wakala wake, Jorge Mendes kupigwa picha akiwa na kocha wa Mashetani hao Wekundu, Louis van Gaal. Van Gaal alikuwa akitabasamu na Mendes wakati wawili hao wakiwa kwenye gari kuelekea viwanja vya mazoezi vya United leo wakitazamiwa kukamilisha dili la Di Maria na klabu hiyo.

DUH POZI GANI HILI?!! NANI AMETISHA ZAIDI…..UNAWEZA HATA KUOA?HUMU HUMU

LA LIGA:MATOKEO NA WAFUNGAJI WA MECHI KATI YA REALMADRID vs CORDOBA UWANJA WA BERNABEU

REAL Madrid jana imeuanza vyema msimu mpya wa La Liga kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Cordoba iliyopanda daraja Uwanja wa Bernabeu. Shukurani kwao, wafungaji wa mabao hayo, Mfaransa Karim Benzema dakika ya 30 na Mwanasoka Bora wa Dunia, Mreno Cristiano Ronaldo dakika ya 90. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa; Casillas, Arbeloa/Carvajal dk73, Ramos, Pepe, Marcelo, Kroos, Modric, Bale, James/Isco dk72, Ronaldo na Benzema/Khedira dk76. Cordoba: Carlos, Gunino, Inigo, Pantic, Crespo, Rossi, Garai, Pinillos/Cartabia dk46, Ryder/Fidel dk62, Lopez Silva na Havenaar/ Xisco dk67.

TAZAMA PICHA ZA KILICHOJIRI KATIKA PARTY ILIYOANDALIWA NA DIVA WA CLOUDS FM PALE MAISHA CLUB

Juzi ndani ya Club Maisha dar es salaam,kulikua na Party kubwa iliyoandaliwa na Mtangazaji wa Kituo cha Clouds Fm Ala za
Roho, Party hii ilihudhuriwa na wajanja wengi wa Town na burudani ilitolewa na Rapper Chidi Benz ambaye kwa muda
mrefu hajaonekana kwenye Majukwaa na sasa hivi anai promote Ngoma yake mpya
Mpaka Kuchwee aliyo washirikisha
Diamond na Ambwene Yesaya (A.Y) Chidi alipokelewa na vizuri na mashabiki waliohudhuria usiku huo, wengine walioperform ni Bob Junior Sharobaro mwenye nyota ya chips Mayai, Kassim Mganga kutoka Manza Bay Tanga, Shilolole
Kiuno pamoja na Mpenzi wake Nuh
Mziwanda wao ndio walifunga kazi kabisa kwa kula denda on stage, Godzilla pia aliperform pamoja na Wadananda, Party hii
iliisha mida ya saa kumi na moja alfajiri.

Download new audio Abdu Kiba - Kabibi

 BOFYA HAPA  kudownload

Muziki unalipa: Davido anunua private Jet (ndege)yake icheki hapa

Mwimbaji wa ‘Ayee’ Davido wa Nigeria amethibitisha kuwa mbali na kuwa mtoto wa bilionea lakini muziki unamlipa kwa kiasi cha kumuwezesha kumiliki private Jet yake. Kama wewe unamfollow Davido kwenye Instagram yake bila shaka utakuwa shahidi kuwa ‘Skelewu’ hit maker anapiga show nyingi sana sababu post zake nyingi huwa ni kuhusu safari za show. Weekend iliyopita alipost picha akiwa kwenye private Jet hiyo kabla ya safari ya kuelekea Togo kwenye show nyingine.

SASA SIMBA WAIKEJELI VIBAYA SANA YANGA

VIONGOZI wa Simba wameiangalia Yanga katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Shangani na wakatamka kauli ambazo ni kama wameipuuza kwa kusema: “Yanga wenyewe ndiyo hawa? Watatukoma.” Lakini kejeli hiyo ya Simba imekuja siku moja baada ya Kocha Marcio Maximo kutamka kwamba yupo makini na kila anachofanya na hawezi kuonyesha makucha yake hapa Unguja kwa vile anajua anafuatiliwa. Hivyo licha ya kwamba wanashinda lakini kocha huyo alisisitiza kwamba kinachoonekana sasa ni utangulizi ‘trela’ tu picha lenyewe bado. Vigogo wa Simba walioishuhudia Yanga yenye mastraika wawili Wabrazili ni Makamu wa Rais, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Kassim Dewji, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Collins Frisch, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano Mohamed Nassoro na Makamu wake, Idd Kajuna, wajumbe wengine ni Adam Mgoyi, Mohamed Omary na Hussein Simba. Mbali na hao, kocha wa Simba, Patrick Phiri ambaye pia aliwaona wachezaji wote wa Yanga kwenye mchezo huo akasema Maximo ana kazi ya ziada kurekebisha kikosi chake kwani kina upungufu. “Nimeona mechi lakini bado kuna mapungufu, Maximo anatakiwa kufanya kazi ili kuimarisha kikosi chake,” alisema Phiri huku akiishudia Yanga ikishinda mabao 2-0. “Kazi wanayo, kwa soka lile Maximo anatakiwa kufanya jitihada za makusudi ili kuhakikisha kikosi hakimsumbui msimu ujao, wamecheza chini ya kiwango tofauti na tulivyofikiria,” alisema. Kwa upande wa Dewji yeye alisema: “Kikosi chetu kimecheza vizuri sana (dhidi ya Kilimani City) japokuwa kina udhaifu mdogo ambao kocha atarekebisha, lakini nimeangalia mechi ya Yanga haijanifurahisha, wana kazi. “Kilimani City ni wazuri na wamecheza soka safi ambalo kila mmoja aliyefika kuangalia amefurahia, hata sisi wenyewe tumekubali kuwa timu hiyo ni nzuri ingawa sisi ni wazuri zaidi.” Katika mechi ya Simba ambayo ilikuwa ya kirafiki kama ile ya Yanga na Shangani, Simba ilishinda bao 2-1. Mabao ya Simba yalifungwa na Shaban Kisiga kwa njia ya penalti na jingine lilifungwa na Haruna Chanongo.credit mwanaspoti

 BONYEZA HAPA KUSOMA HABARI NYINGINE 

Emmanuel Okwi sasa akutana na kiboko yake

KAMA Emmanuel Okwi alizoea kudekezwa na viongozi wa Yanga, sasa amekutana na kiboko yake jambo ambalo huenda likamshtua yeye sambamba na wachezaji wengine wa kigeni. Kocha pekee mkuu Mbrazil kwenye Ligi ya Tanzania, Marcio Maximo ametamka kuwa anawajua wachezaji watano tu wa kigeni Yanga na ndio atakaowatumia. Miongoni mwao jina la Okwi ambaye yupo Dar es Salaam halimo. Maximo amesema atafanya kazi na Hamis Kiiza raia wa Uganda, Wanyarwanda Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite pamoja Wabrazili Andrey Coutinho na Genilson Santos ‘Jaja’ ndiyo anaowatambua. Pamoja na wachezaji hao watano wanaofanya mazoezi ya pamoja, Yanga ina mkataba na Okwi anayefanya timu kuwa na wachezaji sita wa kigeni idadi ambayo hadi kesho Jumatano siku ya kufunga dirisha la usajili lazima ipunguzwe kwa mmoja kukatwa. Akizungumza na Mwanaspoti, Maximo alisema: “Ninao wachezaji watano tayari wa kutoka nje ya nchi kwenye timu yangu, hao ndiyo nitakaofanya nao kazi msimu huu. “Huyo Okwi sijamwona na hajaripoti kwenye timu yangu nifanyaje? Nitafanya kazi na hao tu.” Awali Kiiza ndiyo alikuwa aachwe, lakini sasa hali imeanza kuwa shwari kwake kutokana na nidhamu yake na jinsi anavyojituma mazoezini. Okwi ambaye alikuwa anapewa kipaumbele lakini alichelewa kujiunga na timu kwa sababu zisizojulikana, inadaiwa kuwa uongozi umemwambia ajieleze kwa barua na baada ya hapo atapewa adhabu ambayo ni siri. Kocha Msaidizi wa Yanga, Leonardo Neiva ambaye pia ni Mbrazili, alisema wamefurahishwa na uwezo wa straika Kiiza na kukiri kuwa ana sababu zote za kubaki Yanga. Aliliambia Mwanaspoti kuwa wamependa vigezo vitatu alivyonavyo straika huyo ambavyo ni nguvu, mipango mizuri ya uwanjani na uwezo wake wa kucheza kwenye nafasi tatu tofauti kwa ufasaha. “Anaweza kucheza kiungo vizuri tu kwani ana nguvu, kasi na vilevile mbinu , ana uwezo mkubwa wa kucheza winga na anatoa krosi nzuri na zenye malengo huku akikimbia kwa kasi, anacheza nafasi ya straika wa mwisho pia,” alisema Neiva.Source mwanaspoti

 >>>>>>>>> BOFYA HAPA <<<<>>>uhungane nasi