 |
VIONGOZI wa Simba wameiangalia Yanga katika
mechi yao ya kirafiki dhidi ya Shangani na
wakatamka kauli ambazo ni kama wameipuuza
kwa kusema: “Yanga wenyewe ndiyo hawa?
Watatukoma.”
Lakini kejeli hiyo ya Simba imekuja siku moja
baada ya Kocha Marcio Maximo kutamka
kwamba yupo makini na kila anachofanya na
hawezi kuonyesha makucha yake hapa Unguja
kwa vile anajua anafuatiliwa.
Hivyo licha ya kwamba wanashinda lakini
kocha huyo alisisitiza kwamba kinachoonekana
sasa ni utangulizi ‘trela’ tu picha lenyewe bado.
Vigogo wa Simba walioishuhudia Yanga yenye
mastraika wawili Wabrazili ni Makamu wa Rais,
Geofrey Nyange ‘Kaburu’, Makamu Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili, Kassim Dewji, Mjumbe wa
Kamati ya Utendaji ambaye pia ni Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Collins
Frisch, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano
Mohamed Nassoro na Makamu wake, Idd
Kajuna, wajumbe wengine ni Adam Mgoyi,
Mohamed Omary na Hussein Simba.
Mbali na hao, kocha wa Simba, Patrick Phiri
ambaye pia aliwaona wachezaji wote wa Yanga
kwenye mchezo huo akasema Maximo ana kazi
ya ziada kurekebisha kikosi chake kwani kina
upungufu.
“Nimeona mechi lakini bado kuna mapungufu,
Maximo anatakiwa kufanya kazi ili kuimarisha
kikosi chake,” alisema Phiri huku akiishudia
Yanga ikishinda mabao 2-0.
“Kazi wanayo, kwa soka lile Maximo anatakiwa
kufanya jitihada za makusudi ili kuhakikisha
kikosi hakimsumbui msimu ujao, wamecheza
chini ya kiwango tofauti na tulivyofikiria,”
alisema.
Kwa upande wa Dewji yeye alisema: “Kikosi
chetu kimecheza vizuri sana (dhidi ya Kilimani
City) japokuwa kina udhaifu mdogo ambao
kocha atarekebisha, lakini nimeangalia mechi
ya Yanga haijanifurahisha, wana kazi.
“Kilimani City ni wazuri na wamecheza soka safi
ambalo kila mmoja aliyefika kuangalia
amefurahia, hata sisi wenyewe tumekubali
kuwa timu hiyo ni nzuri ingawa sisi ni wazuri
zaidi.”
Katika mechi ya Simba ambayo ilikuwa ya
kirafiki kama ile ya Yanga na Shangani, Simba
ilishinda bao 2-1. Mabao ya Simba yalifungwa
na Shaban Kisiga kwa njia ya penalti na jingine
lilifungwa na Haruna Chanongo.credit mwanaspoti |
BONYEZA HAPA KUSOMA HABARI NYINGINE
0 comments:
Post a Comment