 |
KAMA Emmanuel Okwi alizoea kudekezwa na
viongozi wa Yanga, sasa amekutana na kiboko
yake jambo ambalo huenda likamshtua yeye
sambamba na wachezaji wengine wa kigeni.
Kocha pekee mkuu Mbrazil kwenye Ligi ya
Tanzania, Marcio Maximo ametamka kuwa
anawajua wachezaji watano tu wa kigeni Yanga
na ndio atakaowatumia.
Miongoni mwao jina la Okwi ambaye yupo Dar
es Salaam halimo.
Maximo amesema atafanya kazi na Hamis Kiiza
raia wa Uganda, Wanyarwanda Haruna
Niyonzima na Mbuyu Twite pamoja Wabrazili
Andrey Coutinho na Genilson Santos ‘Jaja’ ndiyo
anaowatambua.
Pamoja na wachezaji hao watano wanaofanya
mazoezi ya pamoja, Yanga ina mkataba na Okwi
anayefanya timu kuwa na wachezaji sita wa
kigeni idadi ambayo hadi kesho Jumatano siku
ya kufunga dirisha la usajili lazima ipunguzwe
kwa mmoja kukatwa.
Akizungumza na Mwanaspoti, Maximo alisema:
“Ninao wachezaji watano tayari wa kutoka nje
ya nchi kwenye timu yangu, hao ndiyo
nitakaofanya nao kazi msimu huu.
“Huyo Okwi sijamwona na hajaripoti kwenye
timu yangu nifanyaje? Nitafanya kazi na hao
tu.”
Awali Kiiza ndiyo alikuwa aachwe, lakini sasa
hali imeanza kuwa shwari kwake kutokana na
nidhamu yake na jinsi anavyojituma mazoezini.
Okwi ambaye alikuwa anapewa kipaumbele
lakini alichelewa kujiunga na timu kwa sababu
zisizojulikana, inadaiwa kuwa uongozi
umemwambia ajieleze kwa barua na baada ya
hapo atapewa adhabu ambayo ni siri.
Kocha Msaidizi wa Yanga, Leonardo Neiva
ambaye pia ni Mbrazili, alisema
wamefurahishwa na uwezo wa straika Kiiza na
kukiri kuwa ana sababu zote za kubaki Yanga.
Aliliambia Mwanaspoti kuwa wamependa vigezo
vitatu alivyonavyo straika huyo ambavyo ni
nguvu, mipango mizuri ya uwanjani na uwezo
wake wa kucheza kwenye nafasi tatu tofauti
kwa ufasaha.
“Anaweza kucheza kiungo vizuri tu kwani ana
nguvu, kasi na vilevile mbinu , ana uwezo
mkubwa wa kucheza winga na anatoa krosi
nzuri na zenye malengo huku akikimbia kwa
kasi, anacheza nafasi ya straika wa mwisho
pia,” alisema Neiva.Source mwanaspoti |
>>>>>>>>> BOFYA HAPA <<<<>>>uhungane nasi
0 comments:
Post a Comment