Friday, August 22, 2014

TB JOSHUA ATUMA MSAADA WA CHUPA 4000 ZA MAJI YA UPAKO KUPONYA EBOLA

Nabii maarufu ndani na nje ya bara la Afrika TB Joshua wa kanisa la All nations (Scoan) la nchini Nigeria ametuma chupa 4000 za maji ya upako pamoja na dola za kimarekani 50,000 nchini Sierra Leon ili kusaidia kutibu ugonjwa wa ebola ambao umeikamata nchi hiyo. Nabii Joshua amesema kupitia tovuti ya kanisa lake kwamba maji hayo yamesafirishwa kwa ndege maalumu ya kukodi ambayo gharama yake pia ni dola 50,000 na kufanya gharama kamili dola 100,000 (laki moja) kwa msaada alioutoa akishirikiana na wadau wa Emanuel TV ya kanisa lake. Katika taarifa yake kupitia tovuti hiyo nabii TB Joshua amesema Mungu mwenye nguvu atajidhihirisha uweza wake kupitia maji hayo ya upako ambayo yametolewa kwa watu waliokumbwa na ebola. "Sio maji ndiyo ya ponyayo wagonjwa ila ni Yesu mwenyewe, lazima mtu anayemuombea mwingine na yule anayeombewa wawe na imani. lazima imani iwe hai ili kupata uponyaji kwasababu ndiyo husababisha uponyaji na sio maji ya upako" amekaririwa nabii Joshua. Watu waliotumia maji hayo ya upako wamekiri kuwa na imani nayo kutokana na wengi kufunguliwa na miujiza mingi kutendeka kutoka hali ya kutokuwa na uwezo wa kuzaa na hatimaye kupata mtoto lakini pia maji hayo yamekuwa kinga ya risasi kupenya kwenye gari kama mtu mmoja kutoka nchini Ghana alivyopona mikononi mwa majambazi waliokuwa wakishambulia kwa risasi gari lake yeye akiwemo ndani bila mafanikio. Na mdadisiblog/festosaimon

DJ FETTY WA CLOUDS NOMA SANA ATWAGANA NGUMI LIVE LIVE CLUB

Stori: Musa Mateja MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga. Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa kumuona akizichapa na mrembo huyo ikidaiwa walizinguana, hata hivyo waliamuliwa kabla mambo hayajawa mabayaw. Ziara ya Tamasha la Fiesta kesho itahamia Tanga ambapo wasanii kibao wataangusha burudani ndani ya Uwanja wa Mkwakwani

SASA CAF YAICHARUKIA YANGA MCHANA KWEUPE

Shirikisho la Soka Afrika (Caf) limewataka Yanga ambao ni wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho kuwa na kiwanja chao cha mazoezi. Yanga ambayo ipo kisiwani Pemba kwa ajili ya kambi yake ya kujiandaa na mikikimikiki ya msimu mpya, inatarajiwa kuwakilisha taifa katika Kombe la Shirikisho Afrika, lakini imekuwa haina uwanja wa kudumu wa kufanyia mazoezi. Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema agizo hilo la Caf limezitaka timu zote za hapa nchini ambazo zitashiriki mashindano ya kimataifa kuwa na viwanja rasmi vya mazoezi ambavyo vitaweza kutumika muda wowote. “Tumepewa agizo na Caf juu ya kuziambia timu za Azam na Yanga ambazo zitaiwakilisha nchi yetu kwenye mashindano ya kimataifa kuwa na viwanja vyake rasmi vya mazoezi na kama timu haitakamilisha agizo hilo, inaweza ikaondolewa kushiriki mashindano hayo,” alisema Wambura. Ulipotafutwa uongozi wa Yanga kulizungumzia hilo, haukupatikana.

UNASEMA PHIRI MPOLE, SOMA HAPA UONE ANAPOKUWA KAZINI

Kocha wa Simba SC, Mzambia, Patrick Phiri, amewapa masharti mapya wachezaji wake ikiwemo kuwapiga marufuku kukaa chini muda wa mazoezi, hata kama wakiambiwa wapumzike. Hilo limejiri hivi karibuni wakati Simba ilipokuwa ikiendelea na mazoezi kisiwani Zanzibar kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Kiislamu, Chukwani ambapo Phiri alikataza wachezaji waliokuwa pembeni wakipumzika wakisubiri ratiba nyingine, kukaa chini wakiwa kwenye mchakato wa mazoezi. Katika mazoezi hayo, wachezaji wa Simba waligawiwa katika vikosi vitatu ambapo viwili vilikuwa uwanjani, kile kingine ndipo wachezaji wake wakaamua kukaa chini kuwasubiri wenzao. Bila kuchelewa, Phiri alipoliona tukio hilo, alilazimika kuwafuata wachezaji hao na kuwaambia kuwa hawatakiwi kukaa chini wakati wakiwa kwenye programu ya mazoezi, badala yake wanatakiwa kusimama hata kama wakiwa wanapumzika au wanakunywa maji. “Hamtakiwi kukaa chini kama hivyo, kama ukiwa kwenye programu ya mazoezi ya kitimu kama hivi unatakiwa kupumzika kwa kusimama na hata ukinywa maji hupaswi pia kukaa chini, hili lisijirudie tena,” alisikika Phiri akiwaonya wachezaji wake hao. Na mdadisiblog/festosaumon

Shakira atuhumiwa ku- copy na ku-paste wimbo

Sehemu kidogo ya wimbo wa Loca (Spanish version) kutoka kwa mwimbaji Shakira ilikuwa ni kazi ya mtungaji mwingine wa nyimbo anaitwa Ramon Arias Vazquez.

Jaji Alvin Hellerstein alisema toleo la wimbo “Loca” la lugha ya kihispania 2010 lilikiuka haki za umiliki za wimbo wa mwimbaji Ramon Arias Vazquez.

Wimbo huo ulikuwemo kwenye albam yake ya mwaka 2010 ‘Sale el Sol’ na uamuzi unatarajiwa kuelekeza fidia atakayolipwa kwa mlalamikaji

IMEJULIKANA KUMBE KAVUMBAGU ANATUMIA VIDONGE

Straika wa Azam FC, Mrundi, Didier Kavumbagu ameweka wazi kuwa, anatumia vidonge maalum kuongeza virutubisho vya mwili ambavyo vinamsaidia kuwa mwepesi na kumudu programu za kocha wake. Kavumbagu ambaye alikipiga Yanga misimu miwili kwa mafanikio aliyasema hayo hivi karibuni ambapo alikiri kuwa vidonge hivyo vinaongeza virutubisho muhimu mwilini, pia kuulainisha mwili kuwa tayari kwa ajili ya mazoezi magumu ya kimichezo na si vinginevyo. “Nimefanya vizuri katika mazoezi kwa kuwa ninapata muda mwingi wa kupumzika na kula chakula katika muda mwafaka, pia kuna rafiki yangu yupo Ulaya amenitumia vidonge f’lani vya vitamin ambavyo nikimeza vinaufanya mwili uwe huru na kuwa tayari kwa ajili ya mazoezi. “Ni vidonge vya kawaida ambavyo mwanamichezo yeyote anaweza kutumia bila ya kupata madhara, hata Didier Drogba wa Chelsea anavitumia sana,” alisema Kavumbagu. Alipotafutwa Daktari wa Azam, Mwanandi Mwankenwa juu ya ufafanuzi wa vidonge hivyo, alisema: “Navifahamu vidonge hivyo, vinatumiwa na wachezaji wengi wa Azam, siyo yeye tu, hata (John) Bocco na wengine pia wanatumia, havina madhara kiafya.” SOURCE: CHAMPIONI

KOCHA JULIO ATOA KALI YA MWAKA BAADA YA KUMNASA KIBAO MWANDISHI WA HABARI

Kocha msaidizi wa timu ya wachezaji wa zamani wa Tanzania Eleven, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, juzi alitoa kituko kwa kumchapa kofi mwandishi ambaye (siyo wa Championi) alikuwa akimrekodi bila idhini yake baada ya kumaliza mazoezi yanayofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar. Julio alifanya kitendo hicho baada ya kugundua anarekodiwa pasipo mwenyewe kujua, jambo ambalo lilimkera, hivyo kuchukua uamuzi huo kama alivyofanya staa wa Argentina, Diego Maradona hivi karibuni. Julio alizungukwa na kundi kubwa la mashabiki ambapo alikuwa akipiga nao soga mbalimbali. Wakati mazungumzo yamekolea, kocha huyo alimpokonya simu kijana aliyekuwa karibu yake na kuitupa mbali na kisha kumpiga kibao na kumsindikizia na maneno yake yalee ya mbwembwe. “Haiwezekani we ufike unirekodi tu mimi wakati nipo kwenye mazungumzo binafsi,” alisema Julio na kuungwa mkono na wale aliokuwa akizungumza nao. SOURCE: CHAMPIONI

HII TABIA SASA NI BALAA...WADADA WANAZIDI KUJINANILIUUU..WAKATI WANAUME KIBAO HAWANA WAPENZI!!!!

Swali tuwafanyeje!!!

WANAWAKE WENGI NAMNA HII.....KAMA WEWE NDIO HAKIMU HUYU JAMAA UNGEMPA ADHABU GANI?

Jamaa aliebambwa anamla uroda
Mbuzi!!!!

BAADA YA LIVERPOOL KUMSAJILI BALOTEL JANA JIONI HUU NDO USAJILI MWINGINE MKUBWA UNAOFUATA

Kama ulikuwa unadhani Liverpool wamemaliza kazi baada ya kuwa hatua chache za kumnasa mtukutu Mario Barwuah Barotelli nakupa pole tena sana. Mchapo uko hivi Liverpool iko tayari kumpa mshambuliaji Mcameroun Samweli Eto'o mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengere cha kuongeza mmoja zaidi. Tayari kifuta jasho cha £75,000 kwa wiki kiko mezani Anfield,bonuses + michuano ya ligi ya mabingwa atake nini zaidi huyu swahiba wa Mourinho na Guardiola? Mara kadhaa Eto'o amenukuliwa akisema bado anataka kubaki England bado ana muda zaidi wa kucheza ligi kubwa na yenye ushindani... Marekani bado mapema sana kwake....... Bado ana deni na nafsi yake anataka amfunge Pellegrini ampe pole,amfunge Mourinho amcheke.