Friday, August 22, 2014

SASA CAF YAICHARUKIA YANGA MCHANA KWEUPE

Shirikisho la Soka Afrika (Caf) limewataka Yanga ambao ni wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho kuwa na kiwanja chao cha mazoezi. Yanga ambayo ipo kisiwani Pemba kwa ajili ya kambi yake ya kujiandaa na mikikimikiki ya msimu mpya, inatarajiwa kuwakilisha taifa katika Kombe la Shirikisho Afrika, lakini imekuwa haina uwanja wa kudumu wa kufanyia mazoezi. Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema agizo hilo la Caf limezitaka timu zote za hapa nchini ambazo zitashiriki mashindano ya kimataifa kuwa na viwanja rasmi vya mazoezi ambavyo vitaweza kutumika muda wowote. “Tumepewa agizo na Caf juu ya kuziambia timu za Azam na Yanga ambazo zitaiwakilisha nchi yetu kwenye mashindano ya kimataifa kuwa na viwanja vyake rasmi vya mazoezi na kama timu haitakamilisha agizo hilo, inaweza ikaondolewa kushiriki mashindano hayo,” alisema Wambura. Ulipotafutwa uongozi wa Yanga kulizungumzia hilo, haukupatikana.

0 comments:

Post a Comment