Kocha wa Simba SC,
Mzambia, Patrick
Phiri, amewapa
masharti mapya
wachezaji wake
ikiwemo kuwapiga
marufuku kukaa chini
muda wa mazoezi, hata
kama wakiambiwa
wapumzike.
Hilo limejiri hivi
karibuni wakati Simba
ilipokuwa ikiendelea
na mazoezi kisiwani
Zanzibar kwenye
Uwanja wa Chuo Kikuu
cha Kiislamu,
Chukwani ambapo Phiri
alikataza wachezaji
waliokuwa pembeni
wakipumzika
wakisubiri ratiba
nyingine, kukaa chini
wakiwa kwenye
mchakato wa mazoezi.
Katika mazoezi hayo,
wachezaji wa Simba
waligawiwa katika
vikosi vitatu ambapo
viwili vilikuwa
uwanjani, kile
kingine ndipo
wachezaji wake
wakaamua kukaa chini
kuwasubiri wenzao.
Bila kuchelewa, Phiri
alipoliona tukio
hilo, alilazimika
kuwafuata wachezaji
hao na kuwaambia kuwa
hawatakiwi kukaa
chini wakati wakiwa
kwenye programu ya
mazoezi, badala yake
wanatakiwa kusimama
hata kama wakiwa
wanapumzika au
wanakunywa maji.
“Hamtakiwi kukaa
chini kama hivyo,
kama ukiwa kwenye
programu ya mazoezi
ya kitimu kama hivi
unatakiwa kupumzika
kwa kusimama na hata
ukinywa maji hupaswi
pia kukaa chini,
hili lisijirudie
tena,” alisikika
Phiri akiwaonya
wachezaji wake hao. Na mdadisiblog/festosaumon |
0 comments:
Post a Comment