Sunday, August 17, 2014

Angalia picha Wasanii walivo wawasili Dodoma katika Kili Music Tour

DJ Choka ingawa hatujui mkoba aliobeba ni wa nani kati ya Mwasiti, Khadija Kopa au Shilole
Shilole akieleza alivyojipanga. Pembeni yake ni DJ Choka
Ben Pol ambaye ni mwenyeji wa wasanii wote akiongea
Joh Makini baada ya kuwasili jijini Dodoma
Joh Makini akisikiliza moja ya maswali toka kwa tangazaji wa Dodoma FM
Izzo Bizness katika interview
Wasanii wakisubiri kuingia studio za ABM FM
Rich Mavoko akifanyiwa mahojiano ndani ya Dodoma FM
Malkia wa mipasho Khadija Kopa akiimba moja ya vibwagizo vya wimbo wake

Hatimaye wakali watakaopanda jukwaani Agosti 16 wamewasili mkoani Dodoma salama salmini.

Wasanii hao waliwasili kwa basi maalum linalotumika katika ziara hiyo mchana na kwenda moja kwa moja katika mahojiano ya moja kwa moja katika vituo vya redio vya mkoani Dodoma. Wakihojiwa kwa nyakati tofauti wasanii hao wamewahakikishia mashabiki kuwa wamejipanga vizuri kulishambulia jukwaa.

Wasanii wanaotarajiwa kupanda jukwaani ni Mwasiti, Khadija Kopa, Shilole, Izzo Bizness, Rich Mavoko, Christian Bella, Madee, MwanaFA na Weusi.

 BONYEZA HAPA KAMA BADO UJAUNGANA NA BLOG HII 

Saturday, August 16, 2014

ARSENAL YAANZA VYEMA LIGI KUU ENGLAND, SPURS NAYO YAUA MTU

Alexis Sanchez akiwatoka mabeki wa Crystal Palace
Wachezaji wa Arsenal wakimpongeza Aaron Ramsey baada ya kufunga bao la ushindi

BAO la dakika ya 90 na ushei la Aaron Ramsey limeipa mwanzo mzuri Arsenal katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuichapa 2-1 Crystal Palace kwenye Uwanja wa Emirates, London.

Ilibaki kidogo tu Gunners kuanza kwa sare baada ya Crystal kutangulia kupata bao kupitia kwa Brede Hangeland dakika ya 35 kabla ya Laurent Koscielny kuisawazishia Arsenal dakika ya 45 na ushei.

Refa Jon Moss alimtoa nje kwa kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu Jason Puncheon wa Crystal Palace dakika ya 88 baada ya kumchezea rafu Monreal.

Kikois cha Arsenal kilikuwa; Szczesny, Debuchy, Chambers, Koscielny, Gibbs/Monreal dk53, Wilshere/Oxlade-Chamberlain dk69, Arteta, Sanchez, Ramsey, Cazorla, Sanogo/ Giroud dk62. Crystal Palace: Speroni, Kelly, Dann/Delaney dk75, Hangeland, Ward, Puncheon, Jedinak, Ledley, Bolasie/O'Keefe dk90, Chamakh na Campbell/Gayle dk85.

Katika mechi nyingine za ufunguzi leo Ligi Kuu England, Stoke City imelala nyumbani 1-0 mbele ya Aston Villa, bao pekee la Andreas Weimann dakika ya 50 Uwanja wa Britannia, Leicester City imetoka sare ya 2- 2 na Everton, Queens Park Rangers imefungwa 1-0 nyumbani na Hull City, bao pekee la James Chester dakika ya 52 Uwanja wa Loftus Road, West Bromwich Albion imetoka 2-2 na Sunderland Uwanja wa The Hawthorns, West Ham United imefungwa 1-0 nyumbani na Tottenham Hotspur bao pekee la Eric Dier dakika ya 90 na ushei Uwanja wa Boleyn Ground, wakati Manchester United imefungwa 2-1 nyumbani na Swansea City.

Na mdadisiblog/festosaimon
 UNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI ZA KIMICHEZO ZAID BONYEZA HAPA  

AZAM FC YAUA 4-1 NA KWENDA ROBO FAINALI ILE KIBABE HASWA

AZAM FC imemaliza kwa ushindi mnono mechi za makundi, Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame baada ya kuifumua mabao 4-1 Adama City ya Ethiopia Uwanja wa Nyamirambo mjini hapa.

Kwa matokeo hayo Azam FC ya Tanzania Bara, imepanda kileleni mwa Kundi A kwa kufikisha pointi nane baada ya mechi nne, ikishinda mbili na sare mbili- hivyo kutinga Robo Fainali kibabe.

Rayon Sport ambayo hivi sasa inacheza na Atlabara ya Sudan Kusini, inaweza kupanda kileleni mwa kundi hilo iwapo itashinda. Dakika 45 za kwanza zilimalizika timu hizo zikiwa zimefungana bao 1-1, Azam wakitangulia kupitia kwa Nahodha John Bocco ‘Adebayor’ akiunganisha krosi ya Khamis Mcha ‘Vialli’ kabla ya Desaleny Debesh kuisawazishia Adama dakika ya 39.

Refa Mohamed Hassan kutoka Somalia alikataa bao la Kipre Herman Tchetche dakika ya 42, akidai kipa alibughudhiwa na kipindi cha pili Azam iliingia na moto mkali na kufanikiwa kuongeza mabao matatu.

Alianza Didier Kavumbangu dakika ya 55, akimalizia krosi ya Erasto Nyoni akafuatia Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya 60 baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa na Kipre Tchetche akamalizia dakika ya 74, krosi ya Nyoni.

Kocha Mcameroon Joseph Marous Omog alifurahia matokeo hayo na akasema sasa anajipanga kwa Robo Fainali. “Ushindi huu ni mzuri, nafurahi tunaingia Robo Fainali kwa kujiamini, sasa tunaelekeza nguvu zetu huko,”alisema.

Kikosi cha Azam FC; Mwadini Ali, Erasto Nyoni, Gardiel Michael/Said Mourad dk51, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’/Farid Mussa dk61, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Mudathir Yahya dk72, John Bocco ‘Adebayor’, Didier Kavumbangu na Kipre Tchetche. Adama City; Yakoub Fiseha/Yeraswork Terefe dk38, Suleiman Mohamed, Henok Gemtesa, Demetros Wisilase, Mintesinot Kebede, Wonooson Milkesa, Abreham Yisak, Ameha Belete, Abdulkerim Abafogi, Desaleny Debesh/ Abiy Beyene dk68 na Benyam Ayele.

Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUJIUNGA NASI UPATE HABARI KIRAHISI 

KOCHA MPYA, GUNDU PALE PALE MAN UNITED, YAFUMULIWA 2-1 NA SWANSEA OLD TRAFFORD UFUNGUZI LIGI KUU ENGLAND

Matatizo pale pale; Kocha Van Gaal kulia na Msaidizi wake, Ryan Giggs kushoto wakiwa hawaamini macho yao

KOCHA mpya matatizo yale yale Manchester United- hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mashetani hao Wekundu kuanza vibaya Ligi Kuu ya England kwa kuchapwa mabao 2-0 na Swansea City Uwanja wa Old Trafford. Mabao yaliyomfanya kocha Mholanzi, Louis Van Gaal aanze vibaya Ligi Kuu yamefungwa na Ki dakika ya 28 na Sigurdsson dakika ya 72, wakati Nahodha Wayne Rooney aliifungia United dakika ya 53. Kikosi cha Man Utd kilikuwa; De Gea; Jones, Smalling, Blackett, Lingard/Januzaj dk24, Fletcher, Herrera/Fellaini dk67, Young, Mata, Hernandez/Nani dk46 na Rooney. Swansea; Fabianski; Rangel, Amat, Williams, Taylor/Tiendalli, Ki, Shelvey, Routledge, Sigurdsson, Dyer/Montero dk67 na Bony/ Gomis dk77.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII 

HUU NI USHAURI WA BURE KUTOKA KWA H-BABA KWENDA KWA DIAMOND NA WEMA

Msanii wa muziki na filamu H.Baba ambaye yupo ndani ya ndoa na msanii mwenzake Flora Mvungi ametoa maoni yake kwa kile kinachooendelea kati ya pande mbili za kishabiki za Diamond na mpenzi wake Wema.

Kupitia ukurasa Instagram, H.Baba amesema: Tanzaniteone uyo anawaambia sina chakusema kuhusu baba yangu na mama yangu ila baba analolakuwaambia Wema na Naseeb.

Wema kapewa lawama nyingi ila asilaumiwe kwasababu kuu nyingi tu anaeweza kumuongoza Wema ni Naseeb au mama Wema na Martin, upande mwingine Wema na Daimond wanamakosa kwani wanasubiri nini kuowana kama Kweli wanapendana wangefunga ndoa yaya yote yasingetokea kusaidiana kazini ipo ata mie huwanapanda na Mama Tanzaniteone kwenye show zangu pia filamu ya wife nashiriki. ushauri wangu Diamond unaweza kumuongoza Wema vyema tuu kama mimi ninavyomuongoza Mama Tanzaniteone ninaimani unaweza kumuongoza vyema zaidi yetu sisi.

Wawili wakipendana kuingilia penzi ni inshu ila wanapendezana sana chamsingi wangesaidiana kwenye kazi zaidi kama wema anavyoonekana akitoa #saport kubwa kwa #NASEEB na naseeb aonyeshe ushirikiano kwenye mov za wema awepo pia watauza sana kama tunavyouza filamu zetu Mie namamatanzaniteone Ikitoka leo inaisha fasta.

Pia amuongoze kwenye kipindi cha WEMA SHOW mnasaidiana kwelii ata maadui wataogopa #diamond anaweza kumpandisha wema na wema anaweza kumpandisha #daimond wote mnanguvu sana mnamashabiki sana #owaneni mtulie tuuu kwani nn mnakosa mbona sisi tupo tunaishi vyema kwa uwezo wa mungu kazi tunapata mtoto tunamlea vyema hatujalala Njaa kwasababu mwanaume kazini mwanamke kazini #NDOA raha sana asikudanganye mtu unaheshimika popote palee kama #Mume wa mtu na #mke wa mtu #Muda ndo huu umriii uwoo unakwenda fanyeni yenu fasta #leo juu kesho chini #tunawapenda sana tunawatakia maisha mema yenye Furaha kama sisi apa tunafuraha Muda wote? Karibuni kwenye ndoa muone rahaaa..

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI KIRAHISI 

Ndege ya India iliyokuwa na abiria 280 yashuka futi 5000 angani baada ya rubani kusinzia

Mamlaka ya anga nchini India inachunguza tukio la hatari lililotokea Agosti 8, baada ya ndege ya Jet Airways Boeing 777-300 iliposhuka angani kwa zaidi ya futi 5000 (mita 1500) kutoka kwenye urefu waliopangiwa kuruka baada ya rubani wake kusinzia.

Tukio hilo lilitokea wakati ndege hiyo ikifanya safari kutoka Mumbai, India kwenda Brussels, Ubelgiji. Times of India imeripoti kuwa rubani aliyekuwa akiongoza ndege hiyo alipumzika kidogo, mapumziko ambayo kwa viwango vya kimataifa huitwa ‘controlled rest’ kwa zile ndege za masafa marefu.

Safari ya ndege kutoka Mumbai hadi Brussels ni masaa 9. Rubani msaidizi alitakiwa kuchukua majukumu yote ya kuongoza ndege kwa wakati huo, lakini inadaiwa rubani huyo wa kike alisema naye alikuwa busy na tablet ya ndege hivyo hakugundua ndege ilipoanza kushuka kutoka kwenye urefu wa futi 34,000 iliyotakiwa kuruka wakati wanapita Uturuki.

Kwa bahati nzuri waongozaji wa anga wa Uturuki waligundua kuwa ndege hiyo iliyokuwa katika anga lao imeshuka kwenye urefu (altitude) ambao umepangwa kwaajili ya ndege nyingine, na kumtaarifu rubani msaidizi arudi kwenye urefu waliopangiwa.

Marubani wote wawili wa ndege hiyo wamesimamishwa kupisha uchunguzi .

 BONYEZA HAPA KUJIUNGANISHA NA BLOG HII 

LIGI KUU ENGLAND YAANZA LEO, MAN UNITED YA VAN GAAL, CHELSEA YA MOURINHO YENYE DIEGO COSTA, LIVERPOOL BILA SUAREZ, ARSENAL MPYA NA MABINGWA MAN CITY…PATAMU HAPOO!

Kazi inaanza; Kocha Louis Van Gaal tayari kuanzisha zama mpya Manchester United leo
Mabingwa; Manchester City wanaanza kutetea taji lao
Arsenal inaingia kwenye kampeni mpya na kikosi kilichoboreshwa
Kocha Jose Mourinho anaanza kujaribu tena kuipa ubingwa wa Chelsea

LIGI KUU ya England inaanza leo na Louis van Gaal anaanzisha rasmi zama mpya Manchester United atakapoiongoza dhidi ya Swansea City Uwanja wa Old Traffford.

Mwalimu huyo wa Kiholanzi mwenye umri wa miaka 63 amefanya vizuri katika wiki zake nne za kwanza United, akiiwezesha timu kushinda mechi tano na sare moja katika mech za kujiandaa na msimu na sasa watu wanataka kuangalia mafanikio yake katika ligi.

Swansea ni moja kati ya timu nane ambazo msimu uliopita zilishinda mechi Old Trafford Mashetani Wekundu wakiwa chini ya kocha David Moyes aliyetupiwa virago kwa matokeo mabaya mwishoni mwa msimu. Ikumbukwe, United pia ilikutana na Swansea katika mchezo wa ufunguzi wa ligi msimu huo 2013-2014 wakiwa mabingwa watetezi na kushinda mabao 4-1 Uwanja wa Liberty, siku za mwanzoni za Moyes kazini.

Matokeo hayo hayakuwa na maana, kwani mwishoni mwa msimu United ilimaliza katika nafasi ya saba.

Wayne Rooney ataiongoza United kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Nahodha Jumanne timu hiyo ikishinda mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Valencia.

United itamkosa beki wake kinda wa kushoto mwenye umri wa miaka 19 iliyemnunua kwa Pauni Milioni 27, Luke Shaw, ambaye anasumbuliwa na maumivu ya nyama.

Baada ya kuimarisha kikosi kwa kusajili nyota kadhaa wapya, kocha Arsene Wenger ataiongoza Arsenal katika mchezo wa ugenini dhidi ya Crystal Palace. Ikiwa imetoka kumaliza ukame wa miaka tisa wa mataji kwa kushinda Kombe la FA msimu uliopita, Arsenal ilifungua msimu vizuri kwa kutwaa Ngao ya Jamii baada ya kuifumua Manchester City 3-0 wiki iliyopita.

Mchezaji mpya, Alexis Sanchez, aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 30 kutoka Barcelona, anatarajiwa kuwamo kwenye kikosi cha leo katika mchezo wa kwanza wa ushindani sambamba na Nahodha mpya, Mikel Arteta.

Palace inaingia katika mchezo wa leo ikiwa katika mgogoro, kufuatia taarifa za kuondoka kwa kocha Tony Pulis juzi baada ya kutofautiana na wamiliki juu ya sera ya usajili.

Mabingwa wa Championship, Leicester City watacheza mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England tangu mwaka 2004 watakapoikaribisha Everton leo, wakati timu nyingine iliyopanda msimu huu, Queens Park Rangers itaikaribisha Hull City Uwanja wa Loftus Road.

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu, Manchester City wataanza kutetea taji lao dhidi ya Newcastle United kesho. Liverpool, iliyozidiwa kete na Man City katika mbio za ubingwa msimu uliopita, wataanza kampeni zao dhidi ya Southampton, ambao wamewauza Adam Lallana, Rickie Lambert na Dejan Lovren kwa Wekundu hao wa Anfield.

Lallana ataukosa mchezo huo kutokana na maumivu ya goti, lakini Lambert na Lovren wote wapo katika nafasi nzuri ya kuichezea Liverpool, ambayo imetoka kumuuza kinara wake wa mabao Luis Suarez kwa Barcelona.

Chelsea ya Mreno Jose Mourinho, ikiongozwa na wachezaji wake wapya, Diego Costa na Cesc Fabregas itaifuata Burnley iliyoapanda msomu huu Jumatatu. Mechi nyingine; Stoke City na Aston Villa, West Bromwich Albion na Sunderland na West Ham United dhidi ya Tottenham Hotspur, wakati kesho Liverpool v Southampton, Newcastle United v Manchester City na keshokutwa Burnley v Chelsea.

Na mdadisiblog/festo saimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI ILI UPATE HABARI KIRAHISI PUNDE ZITUFIKIAPO 

SHILOLE AFUNGUKA SABABU ZA KURUDIANA NA SERENGETI BOY WAKE

Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amesema sababu kubwa ya yeye kurudiana na mpenzi wake waliyegombana, Nuhu Mziwanda ni kuombwa msamaha

Shilole alisema mpenzi wake huyo aligundua kwamba aliteswa na wivu na kusababisha wagombane hivyo alipotambua kosa lake, aliomba msamaha wakarudiana na mambo yakawa swari.

Zuwena Mohamed ‘Shilole’ “Kikubwa ni kwamba ameomba msamaha ndiyo maana na mimi sikuwa na hiyana, nikapatana naye siku chache tu baada ya kugombana,” alisema Shilole.

Hivi karibuni wawili hao waliripotiwa kuwa wamegombana na kila mtu kuchukua hamsini zake.

 KAMA BADO UJAUNGANA NASI BONYEZA HAPA 

Lady Jaydee ajibu tetesi za kuachana na Gadner kwa staili hii

Wanasema picha huongea maneno 1,000. Baada ya kuendelea kwa uvumi kuwa ndoa ya Lady Jaydee na Gadner G Habash imevunjika, muimbaji huyo amepost picha akionesha pete ya ndoa kwenye kidole chake.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook wa Lady Jaydee ameandika ujumba tofauti na picha lakini mashabiki wake wameelewa kuwa ni ujumbe anaoutoa kufuatia tetesi hizo.

“Kucha zimekosa rangi ya OriFlame tu, ili zing’ae zaidi ya hapo,” ameandika Lady Jaydee.

Huu ni baadhi ya ujumbe kutoka kwa mashabiki wake.

Anna Julius

Tetea ndoa yako dada, achana na maneno ya wa2.

Saumu Kinqo

eee tumeona pete bado ipo kutofautiana kwenye ndoa ni jambo lakawaida mnayamaliza na maisha yanaendelea big up

John Sosteni

Assey Inamaana ndoa iko powa jide komaa wewe mkubwa bwana kunamambo mengi sana mnatufundisha

Calvin Mpoto

Jibu la magazeti ya bongo! Hongera J hayo ni mapito tu,kelele za chura hasishindi tembo kunywa maji!

Devotha Kyaruzi

Anamaanisha ndoa yake ipo acheni udaku.she is mrs gadner jamani oneni pete yake ya ndoa.

Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI KIRAHISI 

LOGA AWAZIDI UJANJA SIMBA AJIPATIA MILIONI 27 NDANI YA WIKI TATU

ALIYEKUWA Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic, amewazidi ujanja Simba baada ya kufanikiwa kujipatia sh. milioni 27 kwa muda wiki tatu.

Kocha huyo alianza kuinoa Simba mwishoni mwa mwaka jana alitokea timu ya Gor Mahia ya Kenya, kwa mkataba wa miezi sita, ambayo ilimalizika baada ya Ligi Kuu Tanzania Bara kumalizika. Hivi karibuni uongozi wa Simba uliamua kuingia mkataba mpya wa mwaka mmoja na kocha huyo, ambao ulidumu kwa wiki mbili kabla ya kusitishwa kwa ajira yake.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba, zilieleza kuwa kocha huyo aliutaka uongozi uliopo madarakani kumpa Dola za Marekani 16,000, sawa na mshahara wa miezi minne. Mtoa habari huyo alisema, kocha huyo alikuwa analipwa dola za Marekani 5,000 sawa na Sh. milioni 8, 492 kwa mwezi, lakini kabla ya kusaini mkataba mpya aliwataka viongozi kumpa dola elfu 16 ambazo ni sawa na 27, 174, 560 halafu wawe wanamkata katika mshahara wake.

Alisema, baada ya kupewa fedha hizo, kocha huyo alianza vituko na kushindwa kufanya kazi yake kwa mujibu wa mkataba wake, kitu kilichopelekea uongozi kukatisha mkataba wake. Alisema, kocha huyo alikuwa hana cha kuidai Simba kwa kuwa alikwishachukua fedha zake mapema baada ya kusaini mkataba.

Kocha huyo raia wa Croatia ameondoka nchini Jumanne usiku kwenda kwao. Hata hivyo, Rais wa Simba, Evans Aveva alikataa kulizungumzia suala hilo na kudai kuwa mkataba wa mwajiri na mwajiriwa ni siri.

Na mdadisiblog/festo saimon
 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI KIRAHISI 

MKWASA AREJEA JIJINI DAR, ASUBIRI KUDAKA DILI JIPYA

Kocha maarufu nchini Charles Boniface Mkwasa amerejea nyumbani na kusema yuko huru kumfundisha timu yoyote inayomhitaji.

Mkwasa amerejea nyumbani baada ya mkataba wake na klabu ya Al Shaollah FC ya Saudi Arabia kuvunjwa ghafla. Mkwasa alikuwa msaidizi wa Hans van der Pluijm na wote mikataba yao ilivunjwa.

Akizungumza jijini Dar, kocha huyo na mchezaji wa zamani wa Yanga amesema yuko tayari ;kudaka’ kazi itakayojitokeza mbele yake. “Nimerejea nyumbani, nitapumzika kidogo ila kama kuna timu itanihitajia kuweza kufanya nao kazi sina tatizo katika hilo, tutafanya kikubwa ni maelewano,” alisema Mkwasa.

Aidha, Mkwasa alisisitiza lijifunza mengi licha ya kufanya kazi Saudi kwa kipindi kifupi.

Na mdadisiblog/festosaimon

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZA HAPA 

RONALDINHO ASHEREKEA MAMBO YAKE KWA KUTUNDIKA JEZI 78 ZIONE HAPA

RONALDINHO AMETUNDIKA JEZI ZAKE 78 KUSHEREKEA ALIKOPITA KISOKA. STAA HUYO ALIYEKUWA NA UWEZO WA JUU SANA, AMECHEZA TIMU KIBAO KWA MAFANIKIO. PAMOJA NA TIMU YA TAIFA YA BRAZIL, BAADHI YA TIMU HIZO NI Gremio, through Paris Saint-Germain, Barcelona, Milan, Flamengo and, latterly, Atletico Mineiro

Na mdadisiblog/festo saimon
 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLIG HII ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI 

SIMBA YATUA KUANZA KAMBI ZANZIBAR BILA YA PHIRI

Simba imetua mjini Unguja tayari kuanza kambi ya kujiandaa na msimu mpya. Hata hivyo, kikosi cha Simba kimetua Zanzibar bila ya kocha wake, Patrick Phiri.

Selemani Matola ambaye ni kocha Msaidizi, ndiye atakiongoza kikosi hicho. Kwa mujibu wa uongozi wa Simba, Phiri ambaye juzi amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuinoa Simba, atawasili Zanzibar leo kuendelea na kazi.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI MBALIMBALI PUNDE ZITUFIKIAPO 

Friday, August 15, 2014

ANGALIA PICHA ZA LUIS SUAREZ AKIFANYA MAZOEZI KWA MARA YA KWANZA NA TIMU YA BARCA

Akijiimarisha na staili ya Barca
Sualez akiwa katika tabasamu alipokuwa anafanya mazoezi na wachezaji wenzake
Kazi imeanza: Luis Suarez akifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa Barcelona leo ijumaa akiwemo nahodha wa klabu, Xavi.

JOSE MOURINHO AGOMA KUANIKA SIRI KAMA ANAHITAJI NYOTA WENGINE

KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amegoma kusema kama bado anahitaji wachezaji wengine Stamford Bridge majira haya ya kiangazi.

The Blues wamewasajili Filipe Luis, Diego Costa, Cesc Fabregas na Didier Drogba kwa dau la jumla la paundi milioni 75 na Thibaut Courtois amerejea klabuni baada ya kumaliza mkataba wake wa mkopo katika klabu ya Atletico Madrid.

Mourinho licha ya kudai kuwa ana furaha na kikosi chake, amemuambia Petr Cech kuwa yupo huru kuondoka. Hata hivyo, kocha huyo amesema bado anaweza kufanya usajili katika dirisha hili la majira ya kiangazi kwasababu muda bado upon a itategemeana na hali halisi.

Aliwaambia waandishi wa habari; “Soko bado lipo wazi na uzoefu unatuonesha kuwa wakati soko lipo wazi huwezi kusema kitakachotokea.

Kama unajua wachezaji wako walikuwa katika kiwango fulani mara ya mwisho mwezi uliopita, hatuwezi kujua timu nyingine zinahitaji kufanya kitu gani kwa wachezaji wetu”. “Lakini ukweli ni kwamba nina furaha na kikosi changu. Nina furaha na timu yangu na mfumo unaniunga mkono” Inafahamika kuwa Chelsea imetuma maombi ya kumsajili mshambuliaji wa QPR, Loic Remy baada ya Didier Drogba kupata majeruhi ya kifundo cha mguu.

Pia dili la kumsajili mlinda mlango kinda Ivan Brkic linaelekea kukamilika. Mourinho alieleza kuwa amevutiwa na wachezaji alionao katika kikosi chake na amekiri kuwa timu yake itakuwa katika mbio za ubingwa msimu wa 2014/2015. “Tumeleta baadhi ya wachezaji muhimu tuliowahitaji katika kikosi chetu. Wachezaji hawa wametufikisha sehemu nyingine”.

“Ndio, sisi ni washindani wa ubingwa. Kama unanitaka nisema kama tutashinda ubingwa, siwezi, kwasababu ninaheshimu ushindani huu”. Chelsea itaanza mbio za ubingwa dhidi ya Burnley katika dimba la Turf Moor siku ya jumatatu.

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZa HAPA 

HIKI NI KIKOSI MAALUM KITAKACHO MENYAMA NA MAGWIJI WA ZAMANI WA REALMADRID AGOSTI 23 UWANJA WA TAIFA

Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM MAKIPA maarufu waliowahi kuwika nchini, Mwameja Mohamed na Manyika Peter wamejumuishwa katika kikosi cha Tanzania All Stars kitakachomenyana na magwiji wa Real Madrid ya Hispania, Agosti 23, mwaka huu.

Chini ya makocha Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ na Wasaidizi Freddy Felix Minziro na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, Daktari Mwanandi Mkwankemwa na viongozi Mtemi Ramadhani, Hassan Mnyenye, Omar Gumbo na Hamisi Kisiwa kikosi hicho kitaingia kambini Dar es Salaam kujiandaa kwa mchezo huo wa Agosti 23, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wengine walioItwa ni mabeki Nsajigwa Shadrack, Mecky Mexime, Boniface Pawasa, John Mwansasu, Abubakar Kombo, George Masatu, Habib Kondo, Viungo Suleiman Matola, Shaaban Ramadhani, Salvatory Edward, Sabri Ramadhani ‘China’, Yussuf Macho, Abdul Mashine, Abdul Maneno, Mao Mkami, Steven Nyenge, Madaraka Suleiman, Akida Makunda na Mtwa Kihwelo.

Washambuliaji ni Monja Liseki, Iddi Moshi, Dua Said, Emmanuel Gabriel, Said Maulid, Thomas Kipese, Nasor Mwinyi ‘Bwanga’, Edibilly Lunyamila, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Clement Kahbuka, Madaraka Suleiman na Akida Makunda.

Wachezaji waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Real Madrid watakuja nchini Agosti 22.

Katika ziara hiyo, pamoja na kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi maalum cha wachezaji nyota wa Tanzania Agosti 23, pia watafanya utalii katika vivutio mbalimbali, ikiwemo kupanda mlima Kilimanjaro.

Real Madrid inakuja nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Farough Baghozah. Miongoni mwa nyota wanaotarajiwa kuja na Real nchini ni pamoja na Wanasoka Bora wa zamani wa Dunia, Mfaransa Zinadine Zidane, Mreno Luis Figo na Mbrazil, Ronaldo Lima.

Magwiji hao wa Real tayari wamekwishafanya matangazo ya ziara yao nchini wakisema wana hamu mno ya kukanyaga ardhi ya Tanzania.

Kampuni ya Vodacom Tanzania ni miongoni mwa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ziara pamoja na Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake Gas, EFM Radio na Ladger Plaza Bahari Beach. Wito umetolewa kwa makampuni zaidi kujitokeza kudhamini ziara hiyo ya kihostoria nchini.

Na mdadisiblog/festosaimon

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA BONYA HAPA KUHUNGANA NASI 

#BringBackOurWema: Ujumbe wa Diamond umeonesha ni Wema ndiye anayehitaji kubadilika!

Tuseme na ule ukweli… Kila mmoja katika maisha ya uhusiano amewahi kuongea maneno kwa hasira kwa mpenzi wake na baadaye kuja kugundua kuwa yalikuwa makali kiasi cha kumuumiza mwenzi wake. Hii inatokea sana, na after all sisi wote ni binadamu na sijawahi kusikia kuna binadamu aliyewahi kuishi kwenye ulimwengu huu akatajwa kuwa alikuwa mkamilifu.

Udhaifu ni miongoni mwa sifa zetu wanadamu. Udhaifu huo ndio ulimfanya Diamond aandike ujumbe ambao kwa wengi umeonekana kama ni msumari wa moto kwenye moyo laini wa mpenzi wake Wema Sepetu.

Kabla ya kuanza kujudge mimi ni nani hadi niwajudge wawili hawa, naomba nimnukuu Akon ambaye hivi karibuni aliwahi kutoa maoni yake kuhusiana na tetesi za kuvunjika kwa ndoa ya Jay Z na Beyonce. Akon alisema: Ukiwa mtu unayejulikana na una uhusiano, uhusiano wako nao unakuwa wa umma. Hivyo usipofunguka kwa umma, ni kawaida wao kuongea vitu wanavyohisi vinaendelea.”

Akon alimaanisha kuwa uhusiano wowote wa watu wanaojulikana hugeuka kuwa uhusiano unaongaliwa na kila mtu. Mkiwa mastaa hamuwezi kuwa na uhuru tena.

Hivyo kwa muda mrefu mashabiki wa Wema na Diamond wamekuwa wakihisi kuna jambo lisilo sawa katika uhusiano wao. Mashabiki wa Wema waliamua kuanzisha kampeni ya #BringBackOurWema baada ya kuhisi kuwa ni Diamond pekee anayenufaika na uhusiano huo, huku career na CV ya Wema ikiendelea kushuka.

Wengi wanaamini kuwa Diamond amekuwa akitumia nguvu ya Wema kujiimarisha zaidi yeye. Ni kawaida hata hivyo kuwa mastaa wawili wakubwa wanapoungana, huwaangunisha pia mashabiki wao kuwa kitu kimoja. Na kwakuwa wote wawili kwa fani zao wana fanbase kubwa, muunganiko wao umetengeneza super fanbase.

Siku chache zilizopita niliandika makala kuhusu kufanana kwa mienendo ya Kim Kardashian na Wema Sepetu na nikadai kuwa tofauti yao ni jinsi Wema anavyoushusha ustaa wake kwa kukatika jukwaani kama dancer wa Diamond, wakati anatakiwa ‘kubehave’ kama first lady wa mwanamuziki anayependwa zaidi Afrika Mashariki kwa sasa.

PICHA: DIAMOND NA WEMA NI KAMA KANYE WEST NA KIM KARDASHIAN LAKINI…

Hicho, na mengine ndicho kimekuwa chanzo cha kuanzishwa kwa kampeni ya #BringBackOurWema.

Kwakuwa lawama nyingi zimetupwa kwa Diamond kuwa ndiye chanzo cha kuporomoka kwa heshima ya Wema huku wengi wakidhani kuwa staa huyo wa muziki haonekani kutoa msaada wowote kwa mwandani wake, ilikuwa ni lazima Diamond ajibu kwanini hali iko hivyo.

Niliwahi pia kuandika makala ya kumshauri Diamond atumie connection zake kumtafutia mashavu ya kimataifa Wema Sepetu.

KWANINI WEMA SEPETU HATUMII UMAARUFU WA DIAMOND KUTAFUTA FURSA YA KUFANYA FILAMU ZA KIMATAIFA?

Hata hivyo inaonekana Diamond aliuzingatia ushauri huo kwakuwa mwezi June mwaka huu alidai kuanza kumuunganisha na waigizaji wa Ghana.

DIAMOND AMUUNGANISHA WEMA SEPETU KUFANYA FILAMU NA WAIGIZAJI WA GHANA

Kama alivyosema Akon kuhusiana na ukimya wa Jay Z na Beyonce kuhusiana na ndoa yao kiasi cha kuwafanya watu wawe na ‘speculations’ cha kile wachohisi kinaendelea, ndivyo hivyo ingekuwa kwa Diamond kama angeamua kutumia ukimya kama jibu la kampeni hiyo.

Bahati mbaya, majibu ya Diamond kupitia Instagram yamekuwa makali kiasi cha kuwashtua wengi na kuona kama kamkosea heshima mpenzi wake. Kwakuwa sitaki kuonekana kama namhukumu Diamond kwa kile alichoandika, ningependa kuongea kwa lugha ya busara kadri iwezekanavyo, na isitoshe nimegusia suala la ‘udhaifu’ na ‘ubinadamu’ katika aya zangu za mwanzo.

Diamond ametumia kauli nzito na ya hasira kidogo katika kuwajibu vinara wa kampeni hiyo. Si jambo la busara kumuita mtu umpendaye kwa kuandika ‘msanii wenu’ baada ya jina lake, pale alipoanza kwa kuandika: Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Msanii wenu’. Ingekuwa vyema kama angeandika; Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Wema Sepetu’. Again, hizo ni hasira tu na ndio maana aliamua kuifuta post hiyo.

Kwa maelezo aliyoyatoa staa huyo, imebainika wazi kuwa ni Wema ndiye aliyeamua kuishi hivyo na pengine ameridhika na hatua aliyofikia. Inavyoonekana Diamond hapendwezi na muenendo na maisha ya mpenzi wake hasa kwa kudai anaendekeza urafiki na watu wanaopenda anasa na kula bata.

“Mngemshauri apunguze mashoga wapenda anasa na apunguze starehe zisizo na faida, wenda ingemsaidia pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe,” yanaendelea kusomeka majibu ya Diamond. Maelezo hayo yanaeleweka wazi kuwa Wema amekuwa ni mtu wa starehe na kula raha na marafiki zake (Aunty Ezekiel haikwepi hii sentensi, inamhusu). Kwa kauli ya Diamond, Wema anaonekana kuendekeza ulevi kwa kutumia fedha anayopewa na mchumba wake.

“Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumwezesha mtaji wa kufanyia kazi.”

Sentesi hiyo inamaanisha kuwa, Diamond anatimiza wajibu wake na tayari amempa mtaji mpenzi wake. Kuna taarifa pia kuwa hata filamu yake ya Family aliyoigiza na Aunty Ezekiel ilidhaminiwa na Diamond.

“Waswahili wanasema mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka ng’ombe wake kwenye maji safi, ila yeye ng’ombe mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji,” anaendelea Diamond. “Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ? Nisiende studio nikae dukani nimuuzie mie? Ni juhudi zako kwanza.”

Maneno ya Diamond yanajielezea yenyewe kuwa Wema amejisahau. Maswali ya wengi ni kuwa wao kama wapenzi hawajawahi kuzungumza haya na kushauriana? Diamond hajawahi kumkanya mpenzi wake kuwa mwenendo wake sio? Au ameshamuambia hadi amechoka na ndio maana ameamua kuuambia umma kile kinachoendelea?

Kwa lawama na matusi ambayo Diamond ameyapata kutokana na kampeni hiyo, ilikuwa inahitaji uvumilivu wa hali ya juu kukaa kimya. Nahisi uvumilivu ulimshinda na ndio maana aliamua kuandika alichokiandika ambacho bahati mbaya kinaweza kutia tena doa uhusiano wao. Sijui Wema atasemaje!!

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII UPATE HABARI KIRAISI 

Taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu ugonjwa wa Ebola kuingia Tanzania.

Ugonjwa wa Ebola ambao kwa sasa umeingia kwenye headlines za dunia kutokana na kuripotiwa kwenye nchi mbalimbali za Afrika sasa umeingia kugusa vichwa vya habari na kuihusisha Tanzania.

Waziri wa Afya wa Seif Rashid amesema wagonjwa waliohisiwa kupata maambukizo hayo kutokana na dalili za awali ni kutoka Benin na Mtanzania lakini baada ya vipimo wameonekana hawana maambukizo hayo.

Waziri Seif Rashid amesema kuwa tayari eneo maalumu limetengwa kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wagonjwa wanaotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo ikiwa ni kauli iliyotoka baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa wawili waliohisiwa.

Kupitia ukurasa wake wa facebook, Waziri Seif amesema vifaa maalumu vitakavyotumiwa na watoa huduma katika kuhudumia wagonjwa vimewekwa pia huku wizara ya afya ikiongeza uwezo wa kufanya uchunguzi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere ambao wasafiri wengi kutoka nje huutumia.

Na mdadiblog/festosaimon
 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBONYEZA HAPA 

BEKI MPYA SIMBA APEWA NYUMBA MIKOCHENI

Wakati Coastal Union wakiendelea kumlilia beki Abdi Banda, mchezaji huyo ambaye amesaini mkataba wa kuichezea Simba, amepewa nyumba ya kuishi.

Hatua hiyo imekuja siku chache tangu mshambuliaji wa Simba, Mrundi Pierre Kwizera, kupewa nyumba ya kuishi pia maeneo ya Kunduchi.

Banda amepewa jumba eneo la Mikocheni huku ikikumbukwa kuwa enzi za utawala wa Mwenyekiti Ismail Aden Rage mchezaji aliyeishi sehemu za gharama kubwa alikuwa ni straika Amissi Tambwe ambaye alipangishiwa mitaa ya Sinza.

“Mimi si mwenyeji wa Dar, viongozi wameniambia kuwa tayari wamenitafutia nyumba Mikocheni na ndani ya wiki hii ninaweza kuhamia,” alisema Banda.