Sunday, August 17, 2014

Angalia picha Wasanii walivo wawasili Dodoma katika Kili Music Tour

DJ Choka ingawa hatujui mkoba aliobeba ni wa nani kati ya Mwasiti, Khadija Kopa au Shilole
Shilole akieleza alivyojipanga. Pembeni yake ni DJ Choka
Ben Pol ambaye ni mwenyeji wa wasanii wote akiongea
Joh Makini baada ya kuwasili jijini Dodoma
Joh Makini akisikiliza moja ya maswali toka kwa tangazaji wa Dodoma FM
Izzo Bizness katika interview
Wasanii wakisubiri kuingia studio za ABM FM
Rich Mavoko akifanyiwa mahojiano ndani ya Dodoma FM
Malkia wa mipasho Khadija Kopa akiimba moja ya vibwagizo vya wimbo wake

Hatimaye wakali watakaopanda jukwaani Agosti 16 wamewasili mkoani Dodoma salama salmini.

Wasanii hao waliwasili kwa basi maalum linalotumika katika ziara hiyo mchana na kwenda moja kwa moja katika mahojiano ya moja kwa moja katika vituo vya redio vya mkoani Dodoma. Wakihojiwa kwa nyakati tofauti wasanii hao wamewahakikishia mashabiki kuwa wamejipanga vizuri kulishambulia jukwaa.

Wasanii wanaotarajiwa kupanda jukwaani ni Mwasiti, Khadija Kopa, Shilole, Izzo Bizness, Rich Mavoko, Christian Bella, Madee, MwanaFA na Weusi.

 BONYEZA HAPA KAMA BADO UJAUNGANA NA BLOG HII 

0 comments:

Post a Comment