Saturday, August 16, 2014

Lady Jaydee ajibu tetesi za kuachana na Gadner kwa staili hii

Wanasema picha huongea maneno 1,000. Baada ya kuendelea kwa uvumi kuwa ndoa ya Lady Jaydee na Gadner G Habash imevunjika, muimbaji huyo amepost picha akionesha pete ya ndoa kwenye kidole chake.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook wa Lady Jaydee ameandika ujumba tofauti na picha lakini mashabiki wake wameelewa kuwa ni ujumbe anaoutoa kufuatia tetesi hizo.

“Kucha zimekosa rangi ya OriFlame tu, ili zing’ae zaidi ya hapo,” ameandika Lady Jaydee.

Huu ni baadhi ya ujumbe kutoka kwa mashabiki wake.

Anna Julius

Tetea ndoa yako dada, achana na maneno ya wa2.

Saumu Kinqo

eee tumeona pete bado ipo kutofautiana kwenye ndoa ni jambo lakawaida mnayamaliza na maisha yanaendelea big up

John Sosteni

Assey Inamaana ndoa iko powa jide komaa wewe mkubwa bwana kunamambo mengi sana mnatufundisha

Calvin Mpoto

Jibu la magazeti ya bongo! Hongera J hayo ni mapito tu,kelele za chura hasishindi tembo kunywa maji!

Devotha Kyaruzi

Anamaanisha ndoa yake ipo acheni udaku.she is mrs gadner jamani oneni pete yake ya ndoa.

Na mdadisiblog/festosaimon

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI KIRAHISI 

0 comments:

Post a Comment