Tuesday, October 07, 2014

HUYU NDIO MWANAMKE TAJIRI ZAIDI AFRIKA MASHARIKI: CHEKI PICHA ZAKE HAPA

Charity begins @ home. On a charity day at katanga. Served the shelter with Easter lunch
At work
Party Zari diva always celebrating her life
Zari with her hubby

WABONGO KUNA MUDA HUWA WANAJITAKIA MATATZO WENYEWE,HUFANYA VITU KAMA WAMEKATWA VICHWA

Inapoelekea kwa sasa ni hatari maana kibao kimekataza kufanya biashara lakini yeye anafanya, sasa hapa lawama kwake au kwa waliokiweka? hii nimeipata maeneo ya Njombe jamaa akiendelea kuuza mahindi ya kuchoma

 HABARI ZINGINE BOFYA HAPA 

Rekodi 7 tofauti alizoweka Cristiano Ronaldo baada ya kufunga hat trick dhidi ya Bilbao

Mwanasoka bora wa dunia Cristiano Ronaldo jana usiku alifunga magoli matatu na kutimiza jumla ya magoli 17 katika michuano yote aliyoitumikia Real Madrid.
Magoli hayo yalimfanya Ronaldo aweke rekodi kadhaa kwenye historia ya soka na rekodi hizo zipo kama ifuatavyo:

*3 – Hii ni Hat trick ya 3 ya Ronaldo katika La Liga msimu huu na amefanikiwa kufunga hat tricks hizo katika kipindi cha siku 15 tu.

*111 – Mchezo wa jana usiku ulikuwa wa 111 kwa Ronaldo kuitumikia timu yake ya taifa au klabu na katika mechi hiz zote amefunga zaidi ya goli moja.

*Cristiano amekuwa mchezaji wa pili kufunga hat tricks 3 katika mechi 7 za raundi ya kwanza ya La Liga – baada ya Mariano Martin kufanya hivyo msimu wa 1943-44.

*Cristiano ndio mchezaji wa kwanza kufunga magoli 13 au zaidi katika mechi 7 za kwanza Liga – tangu alipofanya hivyo Echevaria katika msimu wa 1943.

*50 – Cristiano Ronaldo mpaka sasa ameshatoa assists 50 kwa wachezaji wenzie wa Real Madrid.

*190 – Magoli matatu aliyofunga Cristiano Ronaldo jana dhidi ya Athletic Bilbao yalimfanya atimize jumla ya magoli 190 katika mechi 171 alizoichezea Real Madrid kwenye ligi.

*9 – Gareth Bale mpaka sasa amempa Cristiano Ronaldo assists nyingi kwenye La liga tangu mwanzo mwa msimu uliopita – amempata assists 9.

MWANAFUNZI WA MIAKA 17 AMPA MIMBA MWALIMU WAKE MWENYE UMRI WA MIAKA 25.....KAMANDA WA POLISI ASEMA MWALIMU HANA KOSA KISHERIA!

WAKATI ikiwa imezoeleka kuwa baadhi ya walimu wa kiume huwarubuni wanafunzi wao wa kike na hata kuwaharibia kabisa ndoto zao za kielimu kutokana na kuwapa ujauzito, hali imekuwa tofauti mkoani Rukwa ambako mwanafunzi wa Kidato cha Pili anadaiwa kumzalisha mwalimu wake. Mwanafunzi huyo aliyemzalisha mwalimu wake ana umri wa miaka 17, wakati mwalimu huyo anayefundisha katika Shule ya Sekondari ya Umma ya Nkasi, iliyopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, Rukwa, ana umri wa miaka 25. Tukio hilo linalotajwa kuwa la kwanza kutokea wilayani hapa, limekuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Nkasi na wilaya jirani. Hata hivyo, kwa wanafunzi, wamekuwa wakimpongeza mwenzao kwa kujaliwa kupata mtoto katika umri wake huo mdogo, huku mzazi mwenzake akiwa na uhakika wa maisha kutokana na kuwa ni mtumishi serikalini. Imeelezwa kuwa licha ya tukio hilo, mwalimu huyo aliyezaa na mwanafunzi wake bado anaendelea na masomo shuleni hapo, huku `mzazi’ huyo wa kiume akifundishwa na mzazi mwenzake. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Namanyere hivi karibuni, Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkasi mjini Namanyere ambayo ni ya mchanganyiko ya umma, Amiamie Nanga alisema mwalimu huyo alianza kazi shuleni hapo ikiwa ni mara yake ya kwanza kufundisha baada ya kuhitimu mafunzo ya ualimu chuoni. “Yameshatokea, lakini haileti picha nzuri sana, lakini mimi nina uzoefu mkubwa na wakazi wa mwambao wa Ziwa Tanganyika, kwao si ajabu kuwa na uhusiano na watu waliowazidi umri, iwe kwa mtoto wa kike au wa kiume, wote ni sawa tu… alisema. “Lakini katika kisa hiki, inaonesha walimu sasa wanapoteza haiba ya ualimu. Hii kazi ina miiko na maadili yake …kwa mwalimu huyu hii ni ajira yake ya kwanza, nikimaanisha ni kituo chake cha kwanza cha kazi tangu ahitimu masomo yake…” Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema hakuna kosa kwa mwalimu huyo wa kike kwa kuwa tayari ni mtu mzima. “Isitoshe katika kisa hiki ni nadra kumpata mlalamikaji … Mwalimu mwenyewe huyu wa kike hawezi kuwa tayari kujidhalilisha kuwa amebakwa, yalikuwa maamuzi yake.” Aliongeza kuwa, kwa mwalimu huyo kupata ujauzito wa mwanafunzi wake hakuwezi kuathiri ajira yake, tofauti na mwalimu wa kiume akimpatia ujauzito mwanafunzi wake wa kike ambaye huathirika kwa kukatisha masomo. Jitihada za kumpata mwalimu huyo wa kike na mwanafunzi huyo zimegonga mwamba baada ya watu wao wa karibu kumweleza mwandishi kuwa hawako tayari kuuzungumzia mkasa huo. Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliohojiwa na mwandishi wa habari hizi kwa masharti ya kutoandikwa majina yao kwa hofu ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu shuleni hapo, pamoja na kukiri kutambua uhusiano baina ya mwanafunzi mwenzao na mwalimu wao, lakini walisema hivi sasa mwalimu huyo amesitisha uhusiano na mwenzao na kuanzisha uhusiano mpya na mwalimu mwenzao. Walisema pamoja na mambo mengine ni kama mwanafunzi mwenzao ameathirika kisaikolojia baada ya ‘kupinduliwa’ na mwalimu wake wa kiume ambaye kwa sasa ndiye baba mlezi wa mtoto. alisema mmoja wao. “Huyu mwalimu wa kike sisi sasa tunamwita shemeji yetu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwenzetu… penzi lao lilikolea hadi sasa ameweza kumzalia mtoto huyo…, lakini kwa sasa inavyoelezwa ni kwamba penzi limehamia kwa mwalimu mwenzake,“ Baadhi ya watu wa karibu na mwanafunzi huyo wanakiri kuwa mwanafunzi huyo hana uwezo wa kifedha kumudu kumpatia malezi stahiki mtoto wake huyo, hivyo hata mzazi mwenzake alipoanza uhusiano na mwalimu mwenzake hakuwa na jinsi, bali kukubaliana na matokeo. “Usiniandike jina, sisi tunashauri mwalimu huyo wa kike na mpenzi wake huyo wa kiume ambaye ni mwalimu mwenzake wahamishiwe shule nyingine kwa sababu kama kioo katika jamii wameteleza kwa kiasi kikubwa na watashindwa kuwajenga na kuwalea wanafunzi wao kimaadili. Alihoji. “Isitoshe tunajiuliza sheria hapa inasemaje maana kama angekuwa ni mwalimu wa kiume amempatia mwanafunzi wake wa kike ujauzito angeshitakiwa na kufikishwa mahakamani na pengine kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka 30 jela, sasa kwa hili sheria inasemaje?” Baadhi ya wazazi mkoani hapa waliohojiwa na mwandishi kwa nyakati tofauti wameelezea kushangazwa na tukio hilo, na hasa kwa jinsi mwalimu alivyoshindwa kujizuia `kujiachia’ kimapenzi kwa mwanafunzi wake. Credit: Habarileo

   HABARI ZINGINE BOFYA HAPA 

ANGALIA PICHA ZA KUWANANGA WENGER, MOURINHO ZILIVYOZAGAA MITANDAO MBALIMBALI

BAADA YA KUSHIKANA WAKITAKA KUZICHAPA KATIKA MECHI YA JUZI KATI YA CHELSEA DHIDI YA ARSENAL, WADAU MBALIMBALI WA SOKA WAMETENEGENEZA PICHA KIBAO NA KUZISAMBAZA KWENYE MITANDAO MBALIMBALI KILA MMOJA AKIJARIBU KUONYESHA HISIA ZAKE PIA KUWANANGA MAKOCHA HAO MAARUFU WA ARSENAL NA CHELSEA. ANGALIE MWENYEWE.

HIKI NDICHO WAZIRI ALICHOWAAGIZA TFF KUKIFANYA KUHUSU 5% YA FEDHA ZA WADHAMINI WA KLABU

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia, leo amekutana na uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na ule wa Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) na kuagiza kusitishwa kwa zoezi la ukatwaji wa asilimia 5. TFF iliiagiza bodi kukata asilimia 5 ya fedha za klabu kutokana na udhamini wa Vodacom na Azam TV, halafu ziwekwe kwenye akaunti yake ili zitumike kwa maendeleo ya soka. Lakini katika mkutano wa leo, Nkamia amewasisitiza TFF, Bodi ya ligi na klabu kukutana, halafu kulijadili hilo suala. TFF wametakiwa kukutana kwa pamoja na wadau hao, halafu wafikie mwafaka kabla ya kurejea serikalini. “Wanatakiwa wakutane, wazungumze na kukubaliana na siku nzuri ya kufanya hivyo nimeona ni Jumamosi. “Baada ya hapo watakachofikia mwafaka, basi watarudi serikalini na sisi tuangalie, lakini suala la kukata fedha hizo kweli nimesitisha na sasa liangaliwe hilo la kukutana kwanza,” alisema Nkamia ambaye kitaaluma ni mwanahabari. Mkutano huo unasubiriwa kwa hamu kwa kuwa pande zote tatu zimekuwa na msimamo wa aina mbili. Bodi ya ligi pamoja na klabu hizo za ligi kuu, zimesisitiza haziwezi kukubaliana na hilo la kukatwa fedha zao za udhamini kwa kuwa mikataba ya Vodacom na Azam Tv iko wazi na haielezi hilo la asilimia tano. Lakini tayari TFF kupitia Rais wake Jamal Malinzi ilishatangaza suala hilo halitakuwa na mjadala na lazima wakatwe. Pia kwa hesabu za kawaida, inaonyesha TFF inachukua fedha nyingi zaidi kuliko hata klabu moja moja kupitia udhamini wa Vodacom na Azam TV.

 HABARI ZINGINE BOFYA HAPA 

HARUFU YA SAFARI YA PHIRI KWENDA KUSALIMIA ZAMBIA, INAANZA KUNUKIA

NILIWAHI kuandika makala na kuelezea kuhusiana na suala la Simba kushindwa kufanya kwenye Ligi Kuu Bara kwa mechi mbili mfululizo. Nilichokuwa nakipinga ni kuhusiana na zile hisia za zama za mawe, eti inashindwa kufanya vizuri kwa ajili ya laana ya kundi linalojulikana kama Simba ukawa. Wako mashabiki au waliojiita wanachama wa Simba walihojiwa kwenye vyombo vya habari na kueleza jambo hilo, nikaona wanasambaza hisia ambazo si sahihi kwenye jamii. Vizuri ilikuwa ni kuangalia vizuri mambo kiufundi, tena uwanjani na si kuyaangalia kishabiki kupindukia au kishirikina kwa hisia za kudhani, kitu ambacho si kizuri kwa dunia tunayoishi sasa. Naendelea kupinga hisia hizo zisizo na mashiko za kuwa Simba haifanyi vizuri kwa sababu ya Simba ukawa. Ila nahimiza suala la umoja, kupatana, kurekebisha na kuelewana ni hema kwao kama Wanasimba. Tukirudi kwenye kikosi cha Simba, juzi kimetopata sare ya tatu mfululizo na kuweka reokodi mpya ya kufululizo sare katika mechi za kwanza za ligi. Mbaya zaidi mechi zote tatu iko nyumbani ikianza na sare ya mabao 2-2 dhidi ya Coastal Union, 1-1 dhidi ya Polisi Morogoro na juzi 1-1 ilipokutana na Stand United ya Shinyanga. Usisahau Simba imeweka rekodi mpya ya kutoka sare mbili mfululizo dhidi ya timu mbili zilizopanda daraja, yaani Polisi Moro na Stand United, hii inaonyesha lazima jambo lifanyike. Hali inavyokwenda na hasa katika mechi dhidi ya Stand unaweza ukasoma jambo miongoni mwa wachezaji wa Simba, kuwa kuna presha kubwa nyuma yao inayowasukuma, kwamba lazima wapate ushindi. Kweli, viongozi wanaonekana wamechoka na sasa wanesukuma presha, huenda wanalazimika kwenda mazoezini na mazoezini ili kuhimiza wachezaji wao lazima washinde. Bado utaona, Kocha Patrick Phiri hana raha, baada ya mechi dhidi ya Stand alitikisa kichwa, kuonyesha anaumia na hakubaliani na matokeo hayo. Kutikisa kwake kichwa, kitu ambacho ni nadra kunaweza kutafsiriwa kwa hisia tofauti lukuki. Kwamba huenda amechoka, anashangazwa au anfikiria kuondoka na kurejea nyumbani kwao. Kwani anajaribu kufundisha au kuelekeza kinachotakiwa, lakini inaonekana inashindikana na makosa ya aina moja yanajirudia katika mechi tatu mfululizo, kushindwa kuzitumia nafasi kufunga na kuruhusa mabao ya kusawazisha! Kwa wanaojua rekodi zake, akichoshwa huwa anaanga na kuondoka zake kurejea kwao kimyakimya, hataki makuu. Yote yanawezekana ikawa anapinga presha kutoka kwa uongozi au vinginevyo. Pia inawezekana akawa amechoshwa na malekezo yake kutofanyiwa kazi kama ambavyo amekuwa akitaka na wachezaji wake wamekuwa wakipoteza nafasi nyingi zaidi. Ukipata nafasi rudia kuangalia mechi za Simba dhidi ya Coastal, Polisi Moro na Stand utaona Simba ndiyo timu inayoongoza hadi sasa kupoteza nafasi nyingi zaidi za kufunga. Kuwa na bunduki bila ya risasi unaweza usiwe hatari, ukazidiwa na mwenye kisu. Ndiyo ilivyo Simba, ina uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi, lakini hakuna wenye uhakika wa kuitupia wavuni, ni kupoteza muda. Inaonyesha maelekezo yote anayotoa Phiri yanafanya kazi ndiyo maana Simba imeweza kutengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga mabao, lakini wafungaji hakuna. Kweli wachezaji wanataka wafundishwe kupita kiasi namna ya kuuweka mpira wavunini. Wangekuwa Watanzania pekee tungeingia kwenye hofu labda hatuna shule za kutosha ndiyo maana wanapata shida. Lakini kuna Waganda na Warundi, vipi sasa wanashindwa? Tena rekodi zinaonyesha wako ambao wamefanya vema hapo kabla ya kufunga mabao mengi kama Emmanuel Okwi na Amissi Tambwe, sasa tatizo nini? Nasisitiza, kusema eti Simba ina kikosi kichovu si sahihi, mpira wanaucheza tena mzuri, lakini wanatakiwa kufunga na ndiyo tatizo kubwa walilonalo. Ndiyo maana nasisitiza suala la presha linaweza kuwa zuri lakini pia linaweza kuwa baya kwa Simba. Hivyo namna ya kuwahimiza wachezaji kunatakiwa kuwa na umakini mkubwa sana, la sivyo itakuwa ni kubomoa badala ya kujenga.

Na salleh ally  HABARI ZINGINE BOFYA HAPA 

Monday, October 06, 2014

WENGER AELEZA KISA CHA UGOMVI WAKE NA MOURINHO, ASISITIZA WALA HAJUTII

Kocha Arsene Wenger amesema wala hatajuta kutokana na kitendo chake cha kumsukuma Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho. Wenger alishikana na Mourinho wakati timu zao zilipokutana kwenye mechi ye Premier League kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na Arsenal ikalala kwa mabao 2-0. “Nini cha kujuta, wala sitafanya hivyo. Nilikuwa ninatoka upande mmoja kwenda mwingine. “Nilipogeuka nikakuta mtu yuko mbele yangu kabisa kanizuia. “Halafu hasemi lolote, sasa unafikiri nitafanya nini,” alisema Wenger. Mwamuzi wa akiba alilazimika kuingia kati kuwatenganisha makocha hao wasifikie kuchapana makonde. Baadaye mwamuzi wa mchezo naye aliwaita na kutoa onyo kali akitishia kuwatoa uwanjani.

HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVOFANYA MAKAMUZI YA NGUVU BIG BROTHER HOTSHOTS

STAA wa Bongo Fleva nchini Tanzania , Nasibu Abdul ' Diamond Platnumz ' usiku huu amefanya makamuzi ya nguvu katika uzinduzi wa shindano la Big Brother Hotshots unaofanyika jijini Johanessburg nchini Afrika Kusini. Katika shindano hilo, Tanzania inawakilishwa na watu wawili mrembo Irene ' La Veda ' na Idriss. Jumla ya washiriki 26 kutoka mataifa 12 ya Afrika watachuana kwa siku 63 kutafuta mshindi atakayejinyakulia kitita cha dola za Kimarekani 300, 000 .

DOWNLOAD NGOMA YA FID Q FT AY - UJIO WA VERSE MOJA

RONALDO AFANYA YAKE TENA REALMADRID IKIICHAPA ATHLETIC BILBAO

null
KLABU ya Real Madrid imeifumua mabao 5-0 Athletic Bilbao katika mchezo wa La Liga jana Uwanja wa Bernabeu. Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo amepiga hat-trick ya 22 katika ligi ya Hispania, wakati Mfaransa Karim Benzema amefunga mabao mawili. Ronaldo alifunga katika dakika ya pili, 55 na 88, wakati Benzema alifunga dakika ya 41 na 69 na sasa Real have imepunguza pengo la pointi dhidi ya vinara, Barcelona hadi kubaki pointi nne KIkosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos/Varane, Marcelo, Modric, Kroos/Illarramendi, Rodriguez, Bale, Benzema/Isco na Ronaldo. Athletic Bilbao: Iraizoz, Laporte, Benat, Iturraspe, De Marcos, Susaeta (López Cabrera), M. Rico, Gurpegi, Muniain/Etxeita, Guillermo/Gomez na Balenziaga.

SASA NYIE MNAOJICHUBUA AMJUI KAMA MTU MWEUSI NI DILI SASA MCHEKI MZUNGU ALIVOJIBADILISHA KUWA MTU MWEUSI

HIVI NDO JINSI MADADA WAREMBO WANAVOFANYA LAANA KWENYE CLUB ZA USIKU

NI SHEEEDAH.....MTUMISHI AVAMIA ENEO LA MAKABURI NA KUJENGA BAA

Mtaro alijikuta juzi katika wakati mgumu baada ya wananchi wanaodai ni wenye hasira kutaka kumpa kipigo kwa kitendo hicho cha kugeuza sehemu ya makaburi kuwa eneo la burudani . Mfanyabiashara huyo ambaye pia ni mfanyakazi Idara ya Fedha ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, inadaiwa alianzisha biashara hiyo ya vileo katika eneo la Roben Kata ya Mkuti , mjini Masasi wiki mbili zilizopita. Tafrani iliyojitokeza juzi na kudumu kwa zaidi ya saa saba, ilikuwa ni baada ya kundi la vijana kufika eneo hilo kwa ajili ya kuchimba kaburi kwa maziko ya ndugu yao na kukuta hali tofauti . Inadaiwa walikuta baadhi ya makaburi yamejengwa sehemu za kukaa wateja, choo pamoja na banda kubwa la biashara lililosheheni vinywaji. Aidha walikasirishwa na kile kinachodaiwa kwamba ni kukuta pakiti tupu za pombe zikiwa zimetapakaa juu ya makaburi hayo. Inadaiwa pia walikutwa wateja wakipata vinywaji wakati huo saa 4 asubuhi huku baadhi wakiwa wameweka miguu juu ya makaburi; kitendo kilichoibua hasira ya vijana hao walioamua kutoa taarifa Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mkuti . Mmiliki Akizungumza kwa niaba ya mmiliki, Meneja wa ‘ baa ’ hiyo , Gasper Priscus alisema waliamua kujenga kwenye eneo hilo kwa kuwa kiwanja hicho wanakimiliki. Alidai waliuziwa na mkazi wa Kitongoji cha Roben mjini Masasi, Gerald Daudi . Kwa mujibu wa meneja huyo, baada ya kuuziwa waliamua kuanza ujenzi wa baa hiyo kwa haraka kwa madai kuwa aliyewauzia, Daudi ni mgonjwa. Priscus alisema walikuwa na hofu kwamba endapo angefariki kabla ya kujenga baa hiyo , wangenyang’ anywa eneo hilo kwa kuwa limeshazungukwa na makaburi. Alikiri kwamba takribani wiki mbili sasa zimepita tangu waanze biashara hiyo ya vileo kwenye eneo hilo na kwamba wamekuwa wakipata wateja wengi hasa usiku . Akana kuuza Hata hivyo Daudi; anayedaiwa kuuza eneo hilo kwa Mtaro alikana kuliuza . Alisema aliamua kumpa eneo hilo bure kwa jinsi anavyomsaidia katika hali yake ya ugonjwa ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu sasa . Akizunngumzia kuhusu kuondolewa kwa baadhi ya misalaba kupisha ujenzi huo, Daudi aliyekuwa akizungumza kwa taabu akiwa kitandani , alisema walikubaliana ing’ olewe mitatu pekee kutoka kwenye makaburi ya familia yao. Alisema uamuzi wa kung’ oa misalaba mingine zaidi ya 10 ni uamuzi uliofanywa na aliyemkabidhi eneo hilo. Ofisa Mtendaji Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mkuti , Moza Napachili alithibitisha ofisi yake kupokea taarifa za kuwepo kwa mtu aliyejenga baa kwenye eneo la makaburi. Napachili alisema alikwenda kwenye eneo la tukio akiongozana na Mwenyekiti wa mtaa huo kutafuta suluhu ya mgogoro huo . Baadaye kilifanyika kikao baina ya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Masasi, Henry Kagogoro , Mtendaji wa Kata , wa Mtaa, na Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na anayedaiwa kuwa mmiliki wa baa hiyo , Mtaro . Makubaliano yaliyofikiwa na kikao hicho ni kutaifisha eneo hilo. Walikubaliana libaki chini ya Halmashauri kwa ajili ya shughuli za maziko pekee. Hivyo iliamuriwa jengo hilo la baa na vibanda , viondolewe na mhusika, kesho awasilishe taarifa Idara ya Ardhi zinazoonesha kuwa eneo hilo analimiliki kihalali . Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri alisisitiza eneo hilo la makaburi ni mali ya Halmashauri . Wateketeza kwa moto Hata hivyo wananchi waliokuwa wamefika kwenye makaburi hayo kwa ajili ya kuzika ndugu yao, waliteketeza kwa moto vibanda vitano vya kupumzikia vilivyoezekwa kwa makuti . Pia jengo la baa lilibomolewa . Polisi Kwa upande wa Polisi, ilikiri kuwa na taarifa juu ya mgogoro huo . Mkuu wa Polisi, Wilaya, Azaria Makubi alisema wanaendelea na upelelezi kuhusu tukio hilo. MKAZI wa Mtaa wa Misufini, Kata ya Nyasa, Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara , Innocent Mtaro anatuhumiwa kujenga baa katikati ya makaburi.

News Alert: Siri yafichuka: Sababu ya wabunge kucheza "kitorondo" bungeni hii hapa

Baada ya "Rasimu ya Sitta" kupitishwa na Bunge maalumu baadhi ya wabunge walilipuka kwa furaha na wengine wakakata mauno hadharani, huku mbunge wa Njombe kaskazini Deo Sanga akicheza "Kitorondo" na kukata mauno mbele ya halaiki.

Pia kuna wabunge wengine walikua wakicheza kwa kufuatisha milio ya miziki iliyokua ikirindima kupitia simu zao za mkononi.Watu wengi walihamaki kitendo cha wabunge kufurahia Rasimu hiyo hadi kufikia hatua ya kujitoa akili.

Hii hapa siri ya furaha ya Wabunge hao..

RASIMU YA WARIOBA ILIPENDEKEZA:

1. Mbunge akigombea vipindi vitatu basi, awaachie wengine.
2. Mbunge akivurunda ktk utendaji wake, wananchi wana uwezo wa kumuondoa na kuchangua mwingine.
3. Hakuna mbunge kuwa Waziri, Mkuu wa mkoa, m/kiti wa bodi ya shirika etc. (kwanini vyeo vyote mjilundikie nyie?).
4. Elimu ya mbunge iwe angalau stashahada (diploma) na kuendelea.

RASIMU YA SITTA (ILIYOPITISHWA) IMEPENDEKEZA HIVI:1. Ukomo wa Ubunge usiwe vipindi vitatu.. Hata wazee waliokaa bungeni miaka 50 kama Kingunge, waendelee tukugombea. Vijana wanaotaka kuwa viongozi labda wakajaribu kwny SACCOSS sio UBUNGE.

2. Mbunge akivurunda wananchi hawawezi kumfanya kitu chochote hadi miaka mitano iishe na mbunge apewe pensheni yake (Mil.160).

3. Ruksa Mbunge kuwa waziri, Mkuu wamkoa, DC, Mwenyekiti wa shirika, na vyeo vingine kadri anavyoweza kujilundikia. Wanaosema mbunge asiwena vyeo viwili au zaidi, wana "wivu wa kike" (according to Pius Msekwa).

4. Elimu ya Mbunge iwe kama ya Deo Sanga (mbunge Njombe Kask), yaani kujua kusoma na kuandika tu inatosha. Rasimu ya Sitta inasema si lazima mbunge awe na degree, diploma, au cheti.Si lazima mbunge awe na elimu ya sekondari. Si lazima Mbunge awe amemaliza elimu ya msingi. Hata kama alisoma akaishia darasa la 3 lakini anajua kusoma na kuandika RUKSA KUGOMBEA UBUNGE.

Sasa je katika mazingira haya wabunge wataacha kukata mauno na kucheza"kitorondo" kwa Rasimu hii kupita??JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA UKWELI.

Malisa GJ || Your Partner In Critical Thinking.!

HUYU NI MCHEZAJI ALIYEINGIA KWENYE ORODHA YA WACHEZAJI WA MANCHESTER UNITED MUHIMU OLD TRAFORD

KIUNGO wa zamani wa Manchester United, Park Ji-sung ametambulishwa kuwa Balozi wa klabu Old Trafford leo akiungana na aliyekuwa kocha wake, Sir Alex Ferguson. Wawili hao walifanyiwa mahojiano uwanjani kabla ya United kuanza kupepetana na Everton, na Ferguson akazungumzia enzi za Park na umuhimu aliokuwa nao Manchester. Uteuzi huo wa Park unafanya idadi ya Mabalozi wa United kufika sita, baada ya Sir Bobby Charlton, Andrew Cole, Ferguson, Denis Law na Bryan Robson.

HIVI NDO JINSI ARSENAL WENGER ALIVOTAKA KUMCHEZESHEA KICHAPO MOURINHO STARMFORD BRIDGE

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger (kushoto) akimsukuma mpinzani wake, Jose Mourinho wa Chelsea wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya England baina ya timu hizo leo. Chelsea imeshinda 2-0. Wenger ni Mourinho ni wapinzani wa muda mrefu.
Arsene Wenger akimfuata kocha wa Chelsea, Jose Mourinho baada ya Cahil kumchezea rafu Sanchez
Mtafaruku wa makocha huo uliteks hisia za wengi Uwanja wa Stamford Bridge, ingawa mwisho wa mchezo Wenger alikuwa mnyonge baada ya Arsenal kufungwa

HIVI NDO JINSI KICHWA CHA SANCHEZ KILIVOMPELEKA KIPA WA CHELSEA HOSPITALI APO JANA

Kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois aliumia kichwani baada ya kugongana na Alexis Sanchez hapa dakika ya na akashindwa kuendelea na mchezo na kukimbizwa hospitali, nafasi yake akiingia Petr Cech.
Sanchez mara moja alionyesha uungwana kwa kwenda kufutilia hali ya Courtois