Monday, August 25, 2014

JUX AKANUSHA TUHUMA ZILIZOSAMBAA MTANDAONI KUWA ANATOKA NA VANESSA

Jux amekanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzake Vanessa Mdee na kudai kuwa Vanessa ni mshikaji wake tu lakini amekiri kuwa muimbaji huyo wa ‘Come Over’ ana kila sifa ya kuwa mke. Jux ambaye hivi karibuni alionekana kuwa karibu na Vanessa amesema Vanessa ni mtu wake wa karibu anayefanya kazi naye. “No ni mshikhaji wangu tu, tunafanya naye kazi, kuna tabia zinaendana, kama ninavyokuwa na rafiki na Stamina, Mo Music ni kawaida, sema unajua ni mwanamke na ni njia toafuti ndio maana imekuwa hivyo,” alisema Jux. Alipoulizwa kama Vanessa anafaa kuwa wife material Jux alijibu Vanessa ana kila sifa ya kuwa mke. “Ni msichana mzuri, mwonekano wake mzuri, she is smart, yeah she is a wife material, yuko vizuri, lakini na mimi tumeendana sana tabia zetu kama washikaji. Sema nipo naye karibu na kwa sababu mimi sionekanagi na wasichana wengi ndio maana imekuwa hivyo. Lakini sijui labda baadaye kwa sasa hivi ni mapema, vyote anapanga Mungu,” alisisitiza Jux.

Source bongo5

TETESI ZA SOKA ZILIZOSHAMILI KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA ULAYA LEO JUMATATU ZIPO HAPA

Manchester City wameacha kumfuatilia kiungo wa Everton Ross Barkley, 20, baada ya kuambiwa atagharimu pauni zisizopungua milioni 50 (Mirror), Manchester United wanakaribia kumsajili winga wa Real Madrid Angel Di Maria, 26, na huenda atavunja rekodi ya uhamisho ya Uingereza kwa mkataba wa pauni milioni 56 (Sky sports), Manchester United pia wamepanda dau kwa mara ya pili kumwania kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, katika mkataba utakaohusisha Man U kutoa na mchezaji (Star), Mario Balotelli, 24, huenda akawa mchezaji kamili wa Liverpool katika mkataba wa pauni milioni 16 ifikapo Jumatatu, lakini Liverpool wameacha kumfuatilia mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Samuel Eto'o, 33, (Liverpool Echo), Eto'o anadhaniwa kudai mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki kutoka kwa Liverpool, lakini sasa inaripotiwa kuwa anafanya mazungumzo na Everton ingawa kuna timu za Mashariki ya Kati pia zinamtaka (Mirror), Balotelli hatosaini mkataba wenye kipengele cha utovu wa nidhamu. Mwakilishi wa mshambuliaji huyo Mino Raiola amedai kuwa mkataba huo hauna tofauti na mikataba yoyote ya Liverpool na kuwa makubaliano yatafikiwa kabla ya Jumanne (Express), Arsenal wanafikiria kumchukua Toby Alderweireld, 25, kutoka Atlètico Madrid kuziba nafasi ya Thomas Vermaelen aliyekwenda Barcelona (Star), Gunners pia wanamfuatilia beki wa Olympiakos Kostas Manolas, 23, ambaye alichezea Ugiriki katika Kombe la Dunia na ambaye anatazamwa pia na Man U (Express), kipa wa Chelsea Petr Cech, 33, anajiandaa kuondoka Darajani baada ya nafasi yake kuchukuliwa na Thibault Courtois (Mail on Sunday), Lukas Podolski anajiandaa kuondoka Arsenal na kwenda Juventus kwa mkopo (Sunday Express), Arsene Wenger alimkataa mara mbili Mario Balotelli anayekwenda Liverpool. Balotelli angeweza kwenda Emirates kama Wenger angemtaka (Metro), Valencia wanataka kumsajili Alvaro Negredo kutoka Manchester City kabla ya dirisha la usajili halijafungwa, pia wanawafuatilia Fernando Llorente na Anthony Martial (Superdeporte). Zimesalia siku nane kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Credit salim kikeke

MESSI AANZA LA LIGA NA BAO 2, BARCA YASHINDA 3, MASCHERANO AANZA NA KADI NYEKUNDU

BARCELONA IMEITUNGUA ELCHE KWA MABAO 3-0 HUKU MSHAMBULIAJI WAKE NYOTA, LIONEL MESSI AKIPIGA MAWILI. MESSI ALIFUNGA MABAO YAKE KILA KIPINDI AKIANZA LA KWANZA KATIKA DAKIKA YA 42 NA LA PILI KATIKA DAKIKA YA 64. KABLA YA HAPO, KINDA MOHAMMED MUNIR ALIKUWA AMEIFUNNGIA BARCA BAO KATIKA DAKIKA YA 46. BARCELONA IMEICHAPA ELCHE HUKU IKIWA PUNGUFU BAADA YA BEKI WAKE JAVIER MASCHERANO KULAMBWA KADI NYEKUNDU KATIKA DAKIKA YA 44 TU. KWA USHINDI HUO MAANA YAKE, BARCELONA IMEANZA VIZURI LA LIGA CHINI YA KOCHA LUIS ENRINQUE.

VAN GAAL AMTETEA YOUNG, ASEMA HAKUJIRUSHA BANA!

Kocha Louis van Gaal amesema kiungo wake wa pembeni, Ashley Young hakujirusha makusudi kupata penalti katika mechi dhidi ya Sunderland iliyomalizika kwa sare ya mabao 1-1. Beki Wes Brown aliuondoa mguu wake wakati anakutana na Young lakini akaanguka na mwamuzi Martin Atkinson akamlamba kadi ya njano.

HUYU NI LILIAN KUTOKA MBEYA,RASMI AMETUA DAR KWAAJILI YA KUINGIA KWENYE TASNIA!!!

Wadau wa Bongo Movie
Tumpokee!!!

UNAWEZA KUZIELEZEAJE PICHA HIZI!!!! MAKUSUDI AU BAHATI MBAYA?

ANGALIA FIGO, KAREMBEU 'WALIVYOICHAFUA' KANZU YA JULIO

Figo na Karembeu, wala hawakujivunga wakiwa na mmoja wa viongozi wao wa benchi la ufundi, wakaweka saini zao hatua kwa hatua. Jambo hilo lilionekana kumfurahisha zaidi Julio ambaye alitumia dakika kadhaa kuziangalia saini hizo huku akitabasamu.
Baadhi ya wadau waliokuwa eneo hilo walikuwa akimtania kwamba atabaki na kanzu hiyo bila ya kuifua, lakini naye alitia mbwembwe kwa kuwajibu: “Hii si saini ya kwanza ya Figo, nina jezi pia ameweka saini yake, tena aliweka kule Hispania. Nililetewa na mwanangu Supa.”
Wachezaji nyota, Luis Figo na Cristian Karembeu wa kikosi cha wakongwe cha Real Madrid, wakiichafua kanzu ya beki na kocha wa zamani wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ kwa kuweka saini zao. Wakongwe hao wawili wa Real Madrid waliokuwa hapa nchini na kikosi hicho kwa ajili ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Tanzania Eleven, walifanya hivyo wakati Julio alipoomba waweke saini zao kwenye kanzu yake.

Kama bado ujajiunga nasi>>>>>>>>>>>>>>> Ingia hapa 

:picha na salley jembe

Kauli ya Carlo Ancelotti kuhusu Di Maria kuaga wenzake leo hii

Sakata la usajili wa winga wa kimataifa wa Argentina Angel Di Maria kwenda klabu ya Manchester United limechukua sura mpya leo hii. Kwenye mkutano wa waandishi wa habari wa kocha wa Real madrid Carlo Ancelotti amethibitisha mchezaji huyo yupo karibuni kuhama. Di Maria leo hakufanya mazoezi na wenzake na badala yake alienda kuwaaga wachezaji pamoja na viongozi wengine wa Madrid. “Alikuja leo asubuhi, lakini hakufanya mazoezi. Uhamisho wake bado haujakamilika wote ila anakaribia kuhama kabisa. “Tunamshukuru kwa kila alichoifanyia hii klabu na tunamtakia kila kheri huko anapokwenda, uhamisho haujakamilika rasmi, ila kila kitu tumeshakubaliana,” – Ancelotti alisema. Ingawa Ancelotti hakuitaja timu anayoenda Di Maria lakini vyombo vya habari ulaya vinaripoti kwamba DI Maria atakuwa mchezaji mpya wa Man united kwa ada ya £64 million.

JAMANI JAMANI NAMNA GANI TENA??? ANATAKA NINI HUYU?

Sasa tukiposti mnasema tuna
wazalilisha ......