 |
Figo na Karembeu,
wala hawakujivunga
wakiwa na mmoja wa
viongozi wao wa
benchi la ufundi,
wakaweka saini zao
hatua kwa hatua.
Jambo hilo
lilionekana
kumfurahisha zaidi
Julio ambaye
alitumia dakika
kadhaa kuziangalia
saini hizo huku
akitabasamu. |
 |
Baadhi ya wadau waliokuwa eneo hilo walikuwa akimtania kwamba atabaki na kanzu hiyo bila ya kuifua, lakini naye alitia mbwembwe kwa kuwajibu:
“Hii si saini ya kwanza ya Figo, nina jezi pia ameweka saini yake, tena aliweka kule Hispania. Nililetewa na mwanangu Supa.” |
 |
Wachezaji nyota, Luis Figo na Cristian Karembeu wa kikosi cha wakongwe cha Real Madrid, wakiichafua kanzu ya beki na kocha wa zamani wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ kwa kuweka saini zao.
Wakongwe hao wawili wa Real Madrid waliokuwa hapa nchini na kikosi hicho kwa ajili ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Tanzania Eleven, walifanya hivyo wakati Julio alipoomba waweke saini zao kwenye kanzu yake. |
Kama bado ujajiunga nasi>>>>>>>>>>>>>>> Ingia hapa
:picha na salley jembe
0 comments:
Post a Comment